§ Mwenye
kusafiri kwa ndege atahirimia toka uwanja wa mwisho anaopandia ndege ili
kuchukua hadhari asije akavuka miiqati ila amehirimia, na hapana ubaya
kwake akitamka talbia baada ya kuondoka na ndege; muhimu ahirimie kabla
ya kuvuka miiqati.
§ Inamjuzia
muhrimu kuoga na kubadili nguo za ihramu alizovaa kwa nguo nyingine za
ihramu akiepuka yaliyozuiwa katika ihram.
§
Inachukiwa kuifunga
ihramu kwa pini kwa kuwa hilo linafanana na
nguo iliyoshonwa.
§
Kuhirimia na kuvaa
ihramu hakumlazimu mwenye kuingia Makka
kama hajakusudia kufanya umra au hija.
§ Mwenye
kuhirimia hija katika miezi isiyo ya hija ihramu yake hugeuka ya umra,
na kuna kauli kwamba hubatilika.
§ Hakuna
nia ya matamshi inayomlazimu mwenye kuhiji au mwenye kufanya umra
anapohirimia, lakini inamlazimu kufanya talbia kwa kutamka na sio kwa
kuileta moyoni.
§ Muhrimu
asivae ukanda ila kwa dharura ya kufunga shuka aliyovaa na kuhifadhi
pesa zake, na la hadhari zaidi ni kutovaa saa.
§
Kauli
inayofuatwa kwetu na madhehebu nyingi ni kwamba manukato kabla ya
kuhirimia hayakatazwi ikiwa yataoshwa.
§
Muhrimu
inamharamikia kujitia manukato akiwa katika ihramu.
§ Muhrimu
haruhusiwi kuondoa vinavyokamata taka mwilini
kama kunyoa nywele, kukata kucha, kunyonyoa kwapa, kunyoa
nywele za siri na nyinginezo, isipokuwa kwa dharura ya ugonjwa n.k.
§
Ni haramu kwa
muhrimu maingiliano ya kijinsia baina mume na mke na kushikana kwa
matamanio k.m. kulala pamoja katika nguo moja, kubusiana n.k.
§ Muhrimu
hafungi ndoa wala hafungishi ndoa kutokana na kauli yake - rehema za
Allah na amani zimshukie:
“Muhrimu hafungi ndoa wala hafungishi ndoa wala
haposi.” Imepokewa na Rabiu na Muslim.
§
Ni haramu kwa
muhrimu kuwinda kiwindo cha nchi-kavu kutokana na kauli Yake Aliyetukuka:
)
وَحُرِّمَ عَلَيْكُمْ صَيْدُ
الْبَرِّ مَا دُمْتُمْ حُرُماً(
{Na
mumeharamishiwa viwindo vya nchi-kavu maadamu mumo kwenye ihramu}
[Al-maida 96]. Ama viwindo vya
bahari havikatazwi.
§ Muhrimu
hafuniki kichwa chake kwa cho chote ila kwa dharura
kama matibabu, joto au baridi, ambapo itamwajibikia fidya.
§
Muhrimu anakatazwa
kubishana kunakosababisha ghadhabu, kutokana na kauli Yake Aliyetukuka:
)
الْحَجُّ أَشْهُرٌ مَّعْلُومَاتٌ
فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ الْحَجَّ فَلاَ رَفَثَ وَلاَ فُسُوقَ وَلاَ جِدَالَ
فِي الْحَجِّ(
{Hija ni miezi maalumu;
anayekusudia katika miezi hiyo kufanya hija basi hakuna kusema maneno
machafu wala kufanya maasi wala kubishana katika hija}
[Albaqarah 197].
§
Hakatazwi muhrimu kupiga msuwaki hata
kama utakifanya kinywa chake kitoke damu.
§
Mwanamme
atakayerefusha shuka yake zaidi ya vifundo vya miguu akiwa katika ihramu
itamlazimu kuchinja.
§
Maneno machafu
yanapingana na tabia za muislamu, na katika ihramu huwa yanachusha zaidi.