|
Kuoga kwa ajili ya ihramu na kutawadha, na yote ni katika yanayopendelewa.
Kusali rakaa mbili za sunna ya kuhirimia; ama ikiwa sala ya fardhi imewadia
basi itatosheleza.
Kutamka talbia:
"لبيك
اللهم لبيك،
لبيك لا شريك لك لبيك إن الحمد والنعمة لك والملك لا شريك لك"
“Labbayka-LLahumma labbayk. Labbayka laa
shariika laka labbayk. Innal-`hamda, wan-ni`imata laka wal mulk. Laa
shariika lak”
(Nakuitika tena na tena ewe Allah. Nakuitika
tena na tena, huna mshirika, nakuitika tena na tena. Hakika shukrani na
neema ni Zako pamoja na ufalme; huna mshirika)
Na baadhi ya wakati utaongeza:
"لبيك
بعمرة"
“Labbayka bi`umrah”
(Nakuitika tena na tena kwa umra)
Utaendelea na talbia hii mpaka uingie Al-Masjid
Al-Haraam (Msikiti Mtakatifu wa Maka), na inapendelewa uingie kwa Mlango wa
Salaam (Baabu-ssalaam) na useme:
"اللهم
أنت السلام ومنك السلام وإليك يرجع السلام فحينا ربنا بالسلام وأدخلنا الجنة
دار السلام تباركت ربنا يا ذا الجلال والإكرام"
“Allahumma Antas-salaam, wa minkas-salaam, wa
ilayka yarji`us-salaam, fa`hayyinaa Rabbanaa bis-salaam, wa
adkhilnal-jannata daaras-salaam, tabaarakta Rabbanaa yaa Dhal-jalaali wal
ikraam”
(Ewe Allah! Wewe ndiye Uliyesalimika [na kasoro],
na kwako Wewe hupatikana salama, na kwako Wewe ni marejeo ya salama, basi
tuamkie Mola wetu kwa salama, na utuingize Peponi - Nyumba ya salama;
umetukuka Mola wetu, ewe Mwenye utukufu na ukarimu)
Utakapoiona
Nyumba Takatifu sema:
"اللهم
زد بيتك هذا شرفا وتعظيما وبرا وتكريما وزد من حجه أو اعتمره هداية وفضلا وبرا
وتقوى"
“Allahumma zid baytaka haadha sharafan
wata`adhiimaa, wa birran wa takriimaa, wa zid man hajjahu au i`itamarahu
hidaayatan wa fadhlaa, wa birran wa taqwaa”
(Ewe Allah! Izidishie Nyumba Yako hii utukufu
na uadhimisho, na ihsani na kuhishimika, na mzidishie mwenye kuihiji au
kuifanyia umra uongofu na fadhila, na wema na ucha-Mungu)
Tawafu: ukianzia
kwa kulibusu Jiwe Jeusi ukiweza; usipoweza utaligusa na kubusu mkono wako
baada ya kuligusa, na isipowezekana utaliashiria kwa mkono wako. Kisha
utatufu ukiijaalia Nyumba Takatifu kushotoni kwako, na utasoma ‘Albaaqiyaatu
Assaalihaatu’ (yaani: “SubhaanaLLah walhamduliLLah, walaa ilaaha illa-LLah
waLLahu akbar”) na kuomba utakayo.
Unapofika sawa na Pembe ya Yamani utaigusa ikiwezekana na kusema:
"ربنا
آتنا في الدنيا حسنة وفي الآخرة حسنة وقنا عذاب النار"
“Rabbanaa aatinaa fid-dun`ya `hasanatan wa fil
aakhirati `hasanatan wa qinaa `adhaaban-naar”
(Ewe Mola wetu! Tupe duniani mema, na akhera
mema, na tukinge adhabu ya Moto)
Utaendelea kutufu hivi hivi mpaka tawafu itimie
kwa mizunguko saba.
Kusali nyuma ya Maqamu ya Ibrahiim rakaa mbili na kuomba utakayo.
Kunywa maji ya
Zamzam na kujirushia usoni na kichwani.
Kisha unaondoka kuelekea kwenye Safa. Ukishapanda juu ya Safa utakabir mara
tatu au mara saba na utasema:
"لا
إله إلا الله وحده لا شريك له الملك وله الحمد وهو على كل شيء قدير، لا إله إلا
الله وحده أنجز وعده ونصر عبده وهزم الأحزاب وحده"
“Laa ilaaha il-la-llaahu wa`hdahu laa shariika
lahu, lahul-mulku walahul-`hamdu wa huwa `alaa kulli shay’in Qadiir. Laa
ilaaha il-la-llaahu wa`hdah, anjaza wa`adah, wa nasara `abdah, wa
hazamal-a`hzaaba wa`hdah”
(Hapana anayestahiki kuabudiwa ila Allah peke
Yake hana mshirika. Ufalme ni wake na Yeye ndiye wa kushukuriwa na Muweza
juu ya kila kitu. Hapana anayestahiki kuabudiwa ila Allah peke Yake.
Ametimiza ahadi Yake, akamnusuru mja Wake na akayashinda makundi ya
washirikina peke Yake).
Na utamsalia Mtume - rehema za Allah na amani
zimshukie - na kuomba utakavyoweza.
Kisha utateremka
utembee na huku unasema:
"اللهم
اجعل هذا المشي كفارة لكل
مشي
كرهته مني ولم ترضه مني"
“Allahumma ij`al haadhal-mashya kaffaaratan
likulli mashyin karihtahu minniy walam tardhahu minniy”
(Ewe Allah! jaalia mwendo huu uwe wenye kufuta
makosa ya kila mwendo uliouchukia kutoka kwangu na usiouridhia kwangu)
Na utaomba utakayo.
Ukifika kwenye
alama ya taa za rangi ya kijani utatembea kwa mwendo wa kasi mpaka ufike
kwenye alama ya pili nawe unasema:
"رب
اغفر وارحم وتجاوز عما تعلم إنك أنت العلي الأعلى وأنت الأكرم وأنت الرب وأنت
الحكم"
“Rabbi-ghfir war-`ham, watajaawaz `amma ta`alam,
innaka Antal-`aliyyul-a`alaa wa Antal-akram wa Antal-`hakam”
(Mola wangu samehe na urehemu, na usiyahisabu
unayoyajua; hakika Wewe ndiye Mtukufu wa juu kabisa, na Wewe ndiye Mkarimu
wa wakarimu, na Wewe ndiye Mola na Wewe ndiye Hakimu)
Baada ya alama ya pili utatembea mwendo wa
kawaida mpaka ufike Marwa na utafanya juu yake kama ulivyofanya juu ya Safa.
Kisha utarudia hivyo hivyo baina ya Safa na Marwa mpaka itimie mizunguko
saba.
Kisha
kutokana na ihramu, kwa kunyoa au kupunguza nywele.
MAZINGATIO
Umra ni wajibu (fardhi)
kutokana na kauli Yake Aliyetukuka:
)وَأَتِمُّواْ
الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلّهِ(
{Na timizeni hija na
umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu} [Albaqara, 196], vilevile kutokana
na hadithi ambazo zimetaja kwa uwazi kuwa umra ni fardhi kama hija.
_ Mwenye kukusudia umra baada
ya hija asifanye umra siku za tashriq (tarehe 11, 12, na 13 Dhul-hija), bali
afanye siku ya terehe 14 Dhul-hija.
_
Kufanya umra hakuwezi kuwa badala ya hija ya fardhi hata kukikaririwa; mtu
hana budi kutekeleza fardhi ya hija.
_
Inajuzu kukariri umra isipokuwa katika miezi ya hija.
|