|

SAUMU YA SIKU SITA SHAWALL
Ndugu
zangu waislamu:
Asalamu Aleikum Warahmatu llahi Wabarakaatu:
Anasema Mtume (SAW): Mngelikuwa mnajuwa yaliyokuwemo katika mwezi wa ramadhani
basi mngelitamani ramadhani iwe mwaka mzima).
Haya ni maneno ya Mtume (SAW), je si kweli kuwa ramadhani imekwisha na sisi tuko
katika kusheherekea EID na huku tunatamani kuwa laiti ramadhani ingalikuwa
haikumalizaka. Haya majonzi (huzuni) ya kuondokewa na ramadhani anayajuwa yule
anayejuwa nini hasa saumu si kila mtu anaweza kuwa na fikira hiyo ya kuwa na
huzuni ya kuondokewa na mwezi wa REHMA-MAGHFIRA-ITQU MINA NAAR(Kuepushwa na
jahanam). Ni kama vile mpenzi ikiwa kweli anajuwa nini maana na faida ya
mapenzi, basi anahuzunika akiondokewa na mpenzi wake. Hivi ndivyo inavyotakikana
tuwe leo baada ya kuondokewa na mwenzi mtukufu ambao uongozi wa maisha yetu
umeshushwa katika mwezi huu.
Lakini Mtume alijuwa kuwa kutakuwepo na watu ambao watakuwa na majonzi (huzuni)
kupita kiasi kwa kuondokewa na mwezi wa ramadhani, ndio maana Mtume (SAW)
akasema:
(ãä ÕÇã ÑãÖÇä
Ëã ÃÊÈÚå ÓÊÇð ãä ÔæÇá ßÇä ßÕíÇã ÇáÏåÑ)
(Atakae funga ramadhani kisha akafuatilia kufunga siku
sita za SHAWAAL anakuwa ni kama amefunga mwaka mzima).
Ama
kweli Mtume anahikma ambayo haina kifani vipi alijuwa kuwa katika mwaka kuna
siku 365, na mwezi una siku 30. Na kila jema unalofanya katika siku ALLAH
anakulipa mara 10. Sasa fanya hesabu ifuatayo:-
1) Mwezi wa Ramadhani unasiku 30.
2) funga ya SHAWAAL ni siku 6.
3) Kila jambo jema ukifanya linakuwa thawabu zake mara 10.
Kwa hiyo (30+6)X10= 360 days.
Hapa ndio nyoyo za Waumini zikapowa kidogo baada ya kujuwa kuwa ukifunga mwezi
wa ramadhani kisha ukafunga siku sita za SHAWAAL ni kuwa ni kama umefunga siku
365 (mwaka mzima). Lakini mbona katika hesabu ya juu zimepunga siku tano? i.e
365 days-360 days= 5 days.
Hizi siku tano ni nyongeza yako ili upate kuwa katika ibada ya saumu mpaka kufa
kwako, na hizi siku ni funga ya Jumatatu na Al-Khamis(2days) katika kila wiki
pamoja na funga ya siku tatu katika kila mwezi (funga ya siku za ayaam al-biidh,
tarehe 13,14 na 15).
FUNGA YA MAWAKA= (30days+6days)X10+5days =
(360days+5days)=365days.
Sasa JAZA mwenyewe?
Shukraan,
æÇáÜÜÓÜÜáÇã ÚÜáÜíÜßÜã æÑÍÜãÜÉ Çááøå æÈÜÑßÜÜÇÊÜÜå
|