Hukumu ya kuvuta Sigara

Watu wengi wanajua makatazo ya sigara na wazipuuza dalili (zinazothibitisha madhara na hatari yake), tunaomba utubainishie katika Qurani na Sunna na nini hukumu ya anayesali nyuma ya (imamu) anayevuta sigara baada ya udhu…?

Sigara ni sumu ambayo inayoathiri kidogo kidogo na kusababisha mauti ya kufa mamilioni ya watu kila mwaka kwa ajili ya sigara, na kabla ya miaka miwili imekadiriwa kufikia kiasi ya watu milioni tatu (wanaokufa) kila mwaka, na inaendelea kuzidi kwa haraka kuongezeka idadi yake, mpaka wamekadiria kwamba baada ya myaka michache itafikia mpaka idadi ya watu watakaokufa (kwa ajili ya sigara) milioni kumi kila mwaka.  Na madhara yake (sigara) hapana khitilafu yoyote baina ya madaktari (wote wameafikiana (kwamba madhara yake ni makubwa sana) kwahiyo madaktari wameafikiana kuipiga vita sigara na imewabainikia kwamba inasababisha tafauti ya maradhi ya kensa inayoua, na kadhalika inasababisha maradhi ya moyo na mishipa ( ya mwilini aina nyingi) na kukwaruzika ngozi, na kukwaruzika mishipa kwa ndani ni kuziba njia za damu ndani ya mwili, na anayetumia sigara basi aelewe kuwa antaumia sumi inayompeleka katika mauti na anaiua nafsi yake mwenyewe.

Amesema Allah (katika Qurani Surat Annisaa aya na. 29/30): “wala msiziue nafsi zenu, hakika mwenyezi Mungu ni mwenye kukuhurumieni – na atakayefanya hivyo kwa uadui na dhulma, basi huyo tutamwingiza motoni, na hayo ni mepesi kwa Mwenyezi Mungu:… Na bila shaka hiyo sigara ni kitu kibaya kabisa na athari yake mbaya kabisa kwa mwenye kuitumia na wengineo pia (inawadhuru ukiwapata moshi wake), na kila kibaya basi ni haramu kama alivyosema Allah.  Na Mtume (S.A.W) ameamrisha awakataze (hata hao) watu wa kitabu mayahudi na manasara mabaya yaliyotajwa katika vitabu vyao Taurat na Injili… Kasema Allah (katika Qurani Suratul-Aaraaf aya na 157: “…Anahalalishia vilivyo vizuri na anawaharamishia vilivyo vibaya..” Na hakuna kitu kibaya kama sumu hii (ya sigara) inayoangamiza, anaye nusa harufu ya moshi wake tu ataumwa kichwa, vipi tena anayeitumia? … anapata madhara  katika koo, na kikoromeo cha sauti, na katika kaakaa la kinywa ndani ya ulimi, na katika mrija (unyasi), na katika ini, na mapafu, na katika mwili wote unaathirika, na… na…

Na kama inavyojulikana kwamba afya na mali ni neema mbili katika neema za Allah (alizowaneemesha waja wake) amesema Allah (katika Qurani Suratul-Baqarah aya na. 211: “…Na mwenye kubadili neema za Mwenyezi Mungu baada ya kufikia basi hakika Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.” Jee! Mwenye akili atatia shaka kwamba anayetumia sigara ni miongoni mwa wenye kubadili neema ya Mwenyezi Mungu? Basi yeye (mvuta sigara) anaiharifu afya yake na anaungamiza mwili wake na akili yake, na anaangamiza mali yake katika kuvuta kwake sigara, utaona mtu anachukua sehemu maalumu katika mali yake anaitupa katika moto kwa ajili ya sigara, Jee! Haingii huyu mtu katika hukumu ya wapumbavu na mwovu kwa kuitumia mali yake katika jambo la kipumbavu la madhara?…. na hali Mwenyezi Mungu amekataza kuipoteza mali (katika mambo ya kuiumbavu na yenye madhara) na wala asiyapeleke maisha yake katika hatari?… basi vipi watu wanatumia mali kwa kuzipoteza ovyo na kuharibu afya yao na maisha yao kuwa katika hatari, Jee! Hii si kubadili kukubwa kwa neema za Mwenyezi Mungu?

Na kama tulivyosema kwamba sigara ni sumu inayoua mtu, na anayevuta sigara anajuiua nafsi yake, katika hadithi iliyopokewa na Ibn Murdawih kwa njia ya Abu Hurairah ®, kasema Mtume (S.A.W.): “Atakayejiua nafsi yake kwa (silaha ya) chuma, basi ataletwa na chuma chake kakishika mkononi mwake anajichoma nacho tumboni mwake siku ya kiyama na kutupwa katika moto wa Jahannam akae humo milele, na anayejiua nafsi yake kwa sumu, basi atakuja na sumu yake mkononi mwake anakwenda nayo kuila humo katika moto wa Jahannam milele”

Ama kuhusu Imamu anayevuta sigara baada ya kutia udhu, haijuzu kusali nyuma yake, na yoyote anayefanya hivyo basi sala yake batili.

 

Copyright ©2004  Uislam.net