uislamu.net inachukuwa juhudi kubwa katika kueneza mambo ya kheri miongoni mwa jamii ya Waislamu Khalisi. Daima tumo na mawasiliano baina yetu na hawa wenye kuwatazama mayatima wa mji wa Shinyanga Tanzania. Na yoyote yule mwenye kutaka kuhakikisha basi hata kanda za vedio tunazo za mayatima hawa. Hawali kitoweo, bali chakula chao ni wali na maharage kama yatapatikana.

Tafadhali wasiliana na uislam.net ili upate maelezo zaidi

admin@uislam.net

Hizi hapa ni baadhi ya picha zinazo onesha unyonge ya mayatima hawa.

ENTER

فأما اليتيم فلا تقهر  * وأما السائل فلا تنهر  * وأما بنعمة ربك فحدث*

Basi yatima usimwonee! Na anaye omba au kuuliza usimkaripie! Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.

MAYATIMA wa SHINYANGA (Tanzania)

Alhamdullilah katika Safari moja za kwenda kuwatembele Waislamu wenzangu huku Tanzania, na ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kabisa kufika. Tulitembelea katika mtaa wa Shinyanga ambapo linojionea maajabu ya kuona Alhamdulilahi kwamba bado kuna wa waja wa Mwenyezi Mungu wanatekeleza Amri na kujitahidi katika jambo hili la kuwalea Mayatima. Tulichukuliwa na wenyeji wetu  ili tukatembee katika nyumba ambyo wanalelewa ndani yake Mayatima Thamanini (80) na mwenye kuwalea ni Mwanamke mmoja jasiri yeye na mumewe. Wamejitolea kuifanya kazi hii mpaka mwisho wa umri wao. Wallahi hali hairithishi. Watoto hali yao ni ya kuhuzunisha na nyumba inahitajia matengenezo, kwa hali ya Wislamu leo na kwa uwezo waliokuwa nao haitakiwi majumba ya mayatimi yawe katika hali hii niliyoinona..Lakini nani wa kumshakia. Niliondoka hapo kwa nia ya kurudi nyumbani na kuwaelezea Waislamu Wenzangu ili nao wafanye mchango tuwasaidie Mayatima hao. Na Alhadulilahi mafanikio si mabaya lakini bado juhidi zinatakiwa. Ndio tukaona kuweke chumba maalumu katika Uislamu.net juu ya hawa Mayatima wa Shinyanga na yoyote  anayetaka kushirikisna na Waislamu wenzake basi anakaribishwa. Alhamdulilah watu wanasaidia na tunayo count tumefunguwa wenye kutaka kutuma misaada yao na kila mwezi huwatumia mayatima hao kiwango maalumu ili waweze kuendesha maisha yao japo kuwa hakiwatoshi.

 

 

Copyright © www.uislamu.net