|
Shukrani Zote Ni Za Mwenyezi
Mungu Na Rehema Na Amani Ziwe Juu Ya Bwana Wetu Mtume Wa Mwenyezi Mungu Na
Watu Wake Na Masahaba Wake Na Waliomtii.
Ama Baada: Kwa Yakini
Nimeangalia Juu Ya Huku Kupekua Na Kutafuta Kuhusu Ndoa Ya Mwanamme
Aliyezini Na Mwanamke Na Ambayo Nasema Kwamba Yaliyokubalika Kwenye Dhehebu
La Wanavyuoni Wetu Waliyorehemewa Na Mwenyezi Mungu, Nayo Ni Kauli Ya Jambo
La Ukweli Kabisa Linalo Sababisha Mizizi Ya Uharibifu, Na Dalili Kwamba
Imepokewa Na Jumla Ya Masahaba Radhi Za Allah Ziwe Juu Yao, Miongoni Mwao Ni
Mama Wa Waislamu (Mke Wa Mtume S.A.W. Bibi Aisha Na Ibn Masoud Na Al-Barraa
Bin Azib, Imepokewa Miongoni Mwa Wote Hao, Kwamba (Mwanamme Yeyote Yule)
Atakayezini Na Mwanamke Kisha Akamwoa Basi Wote Wawili Ni Wazinifu (Ni Wenye
Kuzini) Daima (Katika Maisha Yao). Na Hii Inakubalika Kwa Kawaida Ya Yeyote
Yule Anayefanya Haraka Juu Ya Jambo Kabla Ya Wakati Wake Inakuwa Hii Ni
Adhabu Kwake Ya Kuharamishwa Juu Yake (Mwanamke Aliyezini Naye Iwe Haramu
Kwake). Na Hii Inaafikiana Kwa Yale Yaliyotajwa Katika Kitabu Kitakatifu
Kuhusu Uhusiano Wa Maisha Ya Kuoana, Kasema Allah Mtukufu (Katika
Surat-Arruum Aya Na. 21): “Na Katika Alama Zake Ni Kuwa Amekuumbieni Wake
Zenu Kutokana Na Nafsi Zenu Ili Mpate Matulivu Kwao..” Na Uhusiano Wa Ndoa
Kuoana Ni Makao Na Kupata Matulivu Ya Nyoyo, Na Wapi Moyo Utatua Na Kupata
Matulivu Kwa Mwanamme Au Mwanamke Kwa Chanzo Cha Kuipeleka Nafsi Yake
Kutenda Machafu (Zinaa)? Ataelekea Mmoja Kati Yao Wakati Huo Ambao
Anajitumbukiza Na Kuzama Katika Chombo Kichafu Cha Tabia Mbaya Kabisa Na
Kupeana Ndani Yake Vikombe Vya Upuuzi Mbaya Ili Kumwitika Mwito Wa Shetani?
Jee! Haiwezekani Kuwa Baina Ya Mmoja Kati Yao Na Baina Ya Mwengine Walikuwa
Na Tabia Hiyo Ya Matamanio Mabaya Tangu Zamani? Jee1 Hautawaingia Ndani Ya
Killa Mmoja Baina Yo Wasi Wasi (Wa Shetani) Ukwatawala Na Kuwafanya Wakeshe
Mchana ? Naam! Na Mara Elfu Naam!
Bila Shaka Huyo Anajiangamiza, Na Hayawi Haya Ila Kwa Aliyepotoka.
Hapana Shaka
Kwamba Ruhusa (Inayotolewa) Kuozesha Ndoa Ya Wawili Waliyozini Inafungua
Mlango Wa Kuzidisha Machafu (Huu Wa Zinaa) Madamu Jambo Hili Limekuwa Jepesi
Mpaka Kufika Hali Hii, Na Kwamba Kijana Mwanamme Na Msichana Wa Kike
Wanaweza Kukutana Kwa Urahisi
Katika Kivuli Cha Kutenda Machafu Kisha Wakakamilisha Kurasa Ya Machafu Yao
Kwa Kuoana. Na Mbwa Mwitu Wa Kibinadamu Wangapi Waliowavamia Kuwaharibu
Wasichana (Watoto Wanawari Wa Kike) Kwa Njia Ya Kuwadanganya Kwamba
Watawadwa (Na Baada Ya Kuwaharibu) Wanawapiga Teke Kuwaachilia Mbali Na
Kutafuta Wasichana Wengine. Ambapo Hapo Mwanzo Walikuwa Na Tamaa Ya Kuolewa
Na Kupata Mshirika Mwenzake Wa Kuishi Naye, Na Mara Tu Ndoto Yake Inakuwa
Kinyume Na Aliyoyatamani, Inabadilika Hali Yake Msichana Kuwa Chungu
Inayomuumiza Na Kumjaa Huzuni Kifuani Iliyokubwa Isiyokuwa Na Mfano Baada Ya
Kuvunjiwa Hishima Yake Msichana Na Kumbebesha Mimba Tumboni Mwake, Wakati
Huo Tena (Anakuwa Na Aikabili Katika Hali Mbili): Ima Abakie (Na Mimba Yake)
Aikabili Fedheha Na Kuwa Ametupwa Kwa Kudharauliwa Duniani Na Kupuuzwa, Au
Mwisho Wake Ni Ahangaike Kutafuta Madawa Ya Kutoa Mimba. Jee! Hii Si Mfano
Wa Maneno Makali, Nayo Ni Sawa Na Dawa Inayozuia Sumi Ya Kupata Manufaa Ya
Mfano Huu Wa Kuchezea Na Kuwaharibu Wasichana Wa Watu Wenye Mfano Wa Hawa
Wasichana Wanaongamia Kwa Mambo Haya. Khasa Wakati Huu Ulionunua Dawa Ya
Kuzidi Uharibifu Kuiharibu Hishima Na Kuua (Kuondoa) Tabia (Njema).
Na Haya Inapasa Yasiwe Mbali Na Kufikiria Na
Kujua Ya Kwamba Mafungamano Ya Ndoa Ni Mafungamano Matakatifu, Yamewajibika
Yasiingie Ndani Yake Uchafu Wowote Na Yasigandane Na Shaka Yoyote. Na
Katika Msimamo Wa Waja Wema Waliopia (Wa Zamani) Katika Mambo Mengi
Wanahakikisha Hayo (Machafu Ya Kuzini Kisha Kuoana). Na Tika Fiqhi Ya Imamu
Maalik Kwamba Umar Bin Khattaab ® Aliwatenganisha Mwanamme Na Mwanamke
Walioana Kabla Ya Kukamilika Eda Ya Mwanamke, Akasema (Umar): “Wasikutane
Tena (Maisha)”… Na Amechukulia Imamu Malik Katika Madhehebu Yake Na (Pia)
Alleyth Na Al-Awzai Na Wakataja Katika Fiqhi Hiyo Hukumu Ya Umar Bin
Khattaab ® Kuhusu Jambo Hili Kutokana Na Ibn Shihaab Naye Kutokana Na Said
Bin Musayyib Naye Kwa Suleiman Bin Yassaar Kwamba Bibi Taliihah Al-Asadiyyah
Alikuwa Mke Wa Rashid Al-Thaqafy Akamwamcha (Akampa Talaka) Akaolewa Katika
Wakati Wa Eda Yake (Hajakwisha Muda Wake) Basi Umar Bin Khattaab Akampiga (Yule
Mwanamke) Na Pia Akampiga Mumewe Kwa Mpini Na Akawatenganisha Baina Yao,
Kisha Akasema Umar Bin Khattaab ®: “Mwanamke Yoyote Yule Akiolewa Katika Eda
Yake (Kabla Ya Kukamilika) Kama Mumewe Hajawahi Kumwingilia Watenganishwe
Baina Yao Kisha Akae Kumaliza Eda Yake Kwa Mume Wa Mwanzo, Kisha Huyo Mume
Wa Pili Ende Kuposa Upya Kwa Wanaohusika (Kama Hajamwingilia) Na Kama Kawahi
Kumwingilia Basi
Watendanishwe
Kisha Amalize Eda Ya Mume Wa Mwanzo Kisha Akae Eda Ya Mume Wa Pili (Aliyetenganishwa
Naye) Kisha Wasikutane (Kuoana) Maisha Yao).
Na Akasema
Mwanachuoni Abul-Waliid Al-Baaji Katika Kitabu Chake “Al-Muntaqaa” Kwa Fiqhi
Ya Imamu Maalik Kwa Kuharamishwa Kabisa Maisha Kwa Kumwingilia Manamke Naye
Yumo Katika Eda. (Pia) Haya Kayasema Ahmed Bin Hambal Vile Vile, Akatoa
Dalili Hii Al-Baaji Kwa Hukumu Ya Umar®. Na Hukumu Ya Mambo Haya Yaliendelea
Na Kutawanyika Na Kupeana Katika Miji Mingi, Na Wala Hakuna Aliyepinga Na
Kwamba Wamekubaliana Wote.
Na Mfano Wa
Haya Kasema Kadhi Abu Muhammed (Kwamba): Imepokewa Pia Kutokana Na Ally Bin
Abi Taalib ® Na Wala Hakuna Aliyepinga Umashuhuri Wa Hukumu Hii Na Wote
Wamekubalian.
Na Sio Hivi Tu,
Bali Kwa Kauli Ya Imamu Maalik Kwa Kumharamisha Mwanamke Juu Ya Mwanamme
Walaukuwa Kamwingilia (Hata Kama) Baada Ya Kwisha Eda Yake (Ikiwa Kafunga
Akdi Wakati Wa Eda) Nayo Yametajwa Katika Kitabu (Cha Fiqhi Yake) Bali (Pia)
Amesema Ibn Jallaab Kutokana Naye (Imamu Malik) Kwamba Mwanamke Anaharamika
Juu Yake Kwa Kufunga Aqdi Ya Ndoa (Kabla Ya Kumwingilia), Ameyanakili Hayo
Al-Qurtuby Hata Kama Imekuwa Hukumu Hii Katika Muingilia Imejengwa Kwa Aqdi
(Ya Ndoa), Na Hata Kama Si Kweli Hasa (Na Mwanamke) Sio Haki Zaidi Kuwa
Haramu Kabisa (Ndoa Hiyo) Na Kuwa Lazima Apate Adhabu Ya Sheria Juu Yake?
Na Kwa Yakini
Umejua Kuwa Umar ® Hakutoa Adhabu Ya Sheria Kwa Wale Ambao (Waliooana Katika
Eda) Aliowatenganisha Kabisa Baina Yao Maisha Kwa Kuoana Kwao Katika Wakati
Wa Eda, Bali Alitosheleza Kwa Kuwalaumu Ili Kuepuka Na Shubuha.
Na Kwamba Imethibitika Kwa Mtume (S.A.W) Kwa
Wawili Waliolaaniwa, Kasema: “ Hawawi Pamoja Mpaka Siku Ya Kiyama” Na Ikiwa
Hukumu Hii Ya Waliolaaniwa (Yaani Mwanamme Akimwingilia Mkewe Nyuma Wote
Wawili Wamelaaniwa) Imekuwa, (Vipi Tena) Iwe Mwanamke Hana Kosa (Kwa
Kuingiliwa Nyuma) (Ikabidi Lazima Atenganishwe Na Mumewe Iwe Haramu Kabisa
Kuwa Pamoja Mpaka Siku Ya Kiyama) Vipi Basi Isiwe Haramu Kwa (Ndoa Ya) Zinaa?
Ama Yaliyopokewa Kwamba: “Mwanzo Wake Uzinzi Na Mwisho Wake Ndoa”
Yaliyosemwa Na Ibn Abbas ® Sio Kutokana Na Bibi Aisha Ukweli Wake Anaujua
Mwenyezi Mungu Kwa Uhakika Wake (Hadithi
Hiyo) Na
Ama Ya Mwanzoni Yanachukulia Kwamba Lau Mwanamme Na Mwanamke Wamezini Katika
Ujahili (Kabla Ya Uislamu) Basi Zinaa Yake Hawi Mwanamke Haramu Kwake Katika
(Baada Ya) Uislamu, Maana Uislamu Unafuta (Makosa) Yaliyokuwa Kabla Yake, Na
Kwa Vyo Vyote Vile Kauli Hiyo Imesimamishwa Juu Ya Sahaba (Aliyeitaja) Na
Kupingwa Na Masahaba Wengi Wengine, Na Kwa Hiyo Haisimami Kuwa Ni Hoja (Ya
Kuoana Waliozini).
Na Hadithi (Iliyosema):
“Asiozeshwe Aliyepigwa Bakora (Kwa Kuzini) Ila Kama Yeye “Hii Haimaanishi
Kuwa Aoe (Mwanamke) Aliyepigwa Bakora Kwa Sababu Hiyo (Ya Zinaa) Hata Iwe
Dalili Ya Kuruhusu Ndoa Ya Aliyezini Naye Mwanamke, Bali Ina Maana Kwamba
Huyo (Haaminiki) Wala Hategemeki Bila Ya Mipaka. (Yaani Aliyezini Akapigwa
Bakora Haifai Kumwozesha Mwanamke Mwenye Hishima Aliyejilinda Na Machafu).
Ama Kiasi
Kukisia Jambo Zinaa Kwa (Kukisia Iwe Sawa Na) Wizi Katika Shamba, Basi
Haharamishwi Mwizi Kununua Shama Alilokwiba Ndani Yake Iwe Sawa Na Kuowa
Mwanamme Kwa Mwanamke Aliezini Naye, Hiyo Ni Kiasi Ya (Mfano) Usiofaa
Ulioharibika Uharibifu Mkubwa Baina Ya Shina Na Tawi. Na Mtu Haharamishwi
Kununua Shamba Alilokwiba Ndani Yake Baba Au Mtoto Wake Na Anaharamishwa
Kuoa Mwanamke Aliyezini Naye Mmoja Wao. Na Inajuzu Kununua Shamba Lililokuwa
La Baba Yake Au Mwanawe, Na Wala Haijuzu Kuoa Mke Wa Yeyote Katika Wao. Na
Mwenyezi Mungu Ndiye Ajuaye.
|