|
NAMIMA
Namima maana yake ni
kuchukua maneno ya huyu na kuyapeleka kwa yule kwa kusudi ya kuwagombanisha.
Na hii ni katika sifa mbaya ambayo imepingwa na Uislamu. Na mwenye kuwa na
sifa kama hii ni mtu anayechukiza sana mbele ya Allah, ndio akabashiriwa
moto na akaharamishiwa na Pepo hapa hapa Duniani kama hakutubia na akawacha
sifa kama hiyo. Katika Hadithi iliyotolewa na Imam Al Bukhari na Muslim kwa
njia ya Abu Hurairah. Kasema Mtume (S.A.W):
( Åöäøó ÔóÑøó ÇáäøóÇÓö Ðõæ
ÇáúæóÌúåóíúäö ÇáøóÐöí íóÃúÊöí åóÄõáóÇÁö ÈöæóÌúåò æóåóÄõáóÇÁö ÈöæóÌúåò )
“Kwa hakika watu wabaya kabisa ni wale wenye nyuso
mbili. Anawajia watu hawa kwa uso huu. Na Huwendea wengine kwa uso mwengine”.
Na kawaidi
ya Mtu mwenye sifa kama hii ni yule munafiki. Ndio hata Mwenyezi Mungu
akatutahadharisha nao watu kama hawa tusikae nao wala tusiwatii. Kasema
Mwenyezi Mungu katika Surat Nuun Aya ya (8-11):
( ÝóáóÇ ÊõØöÚú
ÇáúãõßóÐøöÈöíäó*æóÏøõæÇ áóæú ÊõÏúåöäõ ÝóíõÏúåöäõæäó*æóáóÇ ÊõØöÚú ßõáøó
ÍóáøóÇÝò ãóåöíäò*åóãøóÇÒò ãóÔøóÇÁò Èöäóãöíãò)
“Basi usiwatii
wanaokadhibisha* Wanapenda ungalikuwa laini kwao* Wala usimtii kila muapaji
sana, aliye dhalili* Msengenyaji (msemaji watu) aendae akitia fitina”.
Mara moja
Mtume (S.A.W) alipokuwa yumo safarini alipita katika makaburi ya watu wawili
bado ni mepya. Akasimama akasema: Hakika ya maiti hawa wanateswa. Na sababu
ya mateso yao si kubwa. Ama mmoja kati yao alikuwa hajilindi na mkojo. Na
wa pili alikuwa anatembeza namima.
Kwa hivyo
mtu kama huyo huanza kuadhibiwa tokea kaburia kwa sababu ya dhambi kama hiyo
iliyochumwa na ulimi wake mwenyewe. Na katika Hadithi iliyotolewa na Imam
Ahmad kwa njiya ya Asmaa bint Yazeed (Radhi za Allah ziwe juu yake). Kasema
Mtume (S.A.W):
( ÃóáóÇ ÃõÎúÈöÑõßõãú ÈöÎöíóÇÑößõãú ÞóÇáõæÇ Èóáóì ÞóÇáó ÝóÎöíóÇÑõßõãö
ÇáøóÐöíäó ÅöÐóÇ ÑõÁõæÇ ÐõßöÑó Çááøóåõ ÊóÚóÇáóì ÃóáóÇ ÃõÎúÈöÑõßõãú
ÈöÔöÑóÇÑößõãú ÞóÇáõæÇ Èóáóì ÞóÇáó ÝóÔöÑóÇÑõßõãõ ÇáúãõÝúÓöÏõæäó Èóíúäó
ÇáúÃóÍöÈøóÉö ÇáúãóÔøóÇÁõæäó ÈöÇáäøóãöíãóÉö ÇáúÈóÇÛõæäó ÇáúÈõÑóÂÁó
ÇáúÚóäóÊó).
“Je! Nikwambieni wale waliobora miongoni mwenu.
Wakasema: Ndio. Akasema Mtume (S.A.W): Waliobora miongoni mwenu ni wale
wanapopata matatizo humkumbuka Mwenyezi Mungu.** Kisha Mtume (S.A.W)
akauliza tena. Je! Nikwambieni wale walioshari baina yenu. Wakasema: Ndio.
Akasema (S.A.W) Walioshari baina yenu ni wale wanaofisidisha baina ya
wapenzi na kwenda na namima”
Na Mtume (S.A.W)
katika Hadithi nyingi alikuwa akiwatahadharisha Masahaba zake na sifa hii
mbaya ya namima. Mpaka ilifika hadi ya kusema: “Hatoingia Peponi mtu mwenye
sifa ya namima.”
Ewe mwenye
kuwa na sifa kama hii. Umepata lipi kubwa pale ulipowagombanisha watu.
Huogopi adhabu kali Kesho Akhera. Una nguvu gani za kuweza kusubiri Moto wa
Jahannam. Wallahi nyumba nyingi zimebomolewa kwa sababu ya maneno ya uwongo
na fitina. Wangapi wameachana baada ya kuishi uzuri. Wangapi waliokuwa
wakipendana kama ndugu na kusaidiana. Akaja mleta namima akayavunja mapenzi
yao wakawa kila mmoja anamkimbia mwenzake.
Ndugu yangu
Muislamu chuki ni katika maradhi makubwa ambayo watu wanaumwa nayo. Mara
nyengine huchukiwa mtu bila ya sababu, au huwenda ikawa katika sababu za
kijinga. Waislamu haifai kuwa na chuki baina yao. Lazima wawe wanapendana
lao liwe moja. Sio kila mmoja anamuona mwenzake kama nyoka. Imefika hadi
Waislamu wawili wanakutana pahala basi hata salamu hawatoleani. Kila mmoja
anajiona kuwa yeye ni bora zaidi. Eti tunatafuta sababu ya kutokukubaliwa
dua zetu, na kumbe tunayoyafanya ni makwubwa kwa Mola wetu. Mfano mzuri wa
kuufata ni Masahaba. Hebu tuwatazame vipi yalikuwa maisha yao. Walikuwa kama
hawakumuona mwenzao katika Sala moja ya Jamaa hakuja, basi upesi hukimbilia
kwake kumtazama labda anaumwa. Lakini leo anakufa jirani yako habari huna.
Unashtukia janaza tu linatolewa ndani ya nyumba. Waislamu amkeni na ghafla
kama hii. Kuna kisa kizuri kilitokezea zama za Bwana Mtume
(S.A.W)
kinachomaanisha kwamba Muislamu anatakiwa asiwe na bughdha wala chuki wala
hasadi juu ya Muislamu mwenziwe.
Mara moja
Mtume (S.A.W) alikuwa kakaa na Masahaba zake Msikitini akawaambia: Ataingia
Mtu hivi sasa katika watu wa Peponi. Baada ya muda kidigo akaingia bwana
mmoja kishatoka kutia udhu na kungojea Sala. Siku ya pili Mtume alipokuwa
kakaa tena na Masahaba zake, akawaambia tena maneno yale yale ya kuwa
ataingia mtu hivi sasa katika watu wa Peponi. Baada ya muda kidogo akaingia
bwana yule yule wa jana. Siku ya tatu Mtume (S.A.W) akasema yale yale
yaliopita na akatokezea tena bwana yule yule. Sahaba mmoja anaeitwa
Abdillahi bni Omar (mtoto wa Sayyidna Omar bni Lkahataab) akataka kujua kitu
gani kikubwa huyu anachokifanya mpaka Mtume (S.A.W) akambashiria Pepo mara
tatu. Akasema Inshaala nitakifatilia nami nikijuwe ili nami nifanye. (Hapo
bila ya kuwa na hasadi wala choyo, isipokuwa ni kutaka kushindana katika
mambo ya kheri). Huyu Bwana Abdillahi bni Omar akatoka mpaka katika nyumba
ya yule sahaba aliyebashiriwa Pepo mara tatu, na inasemekana ya kwamba jina
lake alikuwa anaitwa (Hurquus bin Zayd Al Saadi).
Bwana Ibn
Omar akafunguliwa mlango na kuingia. Kisha akaomba ombi la kutaka awe mgeni
muda wa siku tatu katika nyumba ya (Hurquus) kwa sababu ya maatizo nyumbani
kwao baina ya yeye na baba yake. (Hila hii aliitumia sahaba huyu ili apate
kukaa mle ndani ya nyumba ili aone amali gani nzuri mtu hufanya mpaka
akabashiriwa Pepo mara tau. Bwana Abdillahi akakaa humo siku ya kwanza huku
akichunguza. Muda wa siku tatu hakuona kubwa linalotendeka ili ifike daraja
ya kubashiriwa Pepo. Hapo tena ilimbidi amuulize mwenyewe kwa kumwambia (Ewe
Hurquus ndugu yangu) mimi nilikuwa sina shida ya kukaa kwako ila kwa jambo
moja tu, ni kutaka kujua amali gani nzuri unayoifanya mpaka Mtume (S.A.W)
akakubashiria Pepo mara tatu. Hebu niambie nami nipate kunufaika. Bwana
Hurquus akajibu (Wallahi hakuna jengine ila hayo uliyoyaona. Lakini mimi
kawaida yangu ninapoingia kulala huwa moyo wangu kama karatasi nyeupe, sina
chuki wala bughdha na Muislamu yoyote katika ulimwengu huu.
Subhana
Llaah! Leo hii ukitaka kuwahisabu unaowaonea chuki ni wengi sana. Mtu
anaingia kulala na moyo wake umejaa hasadi na chuki. Hili ni somo watu
lazime wachukuwe riwaza katika maisha yao. Waliogombana warudi na wapatane.
Walioachana warudiane. Kwani hakuna bainaadamu aliyekamilika katika
Ulimwengu huu. Kila mmoja wetu ana ila yake lakini wajibu wetu ni
kustahamilina na kusameheana.
Tukibakia
bado katika mlango wa namia nadhani msomaji atakuwa pamoja nami ya kuwa kila
mwenye sifa ya namima huwa na chuki katika moyo wake. Ndio akataka
kuuburudisha moyo wake kwa kuwafitinisha watu. Na mwenye sifa ya namima
huwenda ukaka naye lakini humjuwi. Mbele yako hukupa maneno matamu lakini
ukiondoka tu, huyabadilisha yakawa mengine mabaya ya kufedhehesha. Kuna kisa
kilitokezea hapo zamani. Kinachobainisha ya kuwa mwenye sifa kama hii ya
namima lazime tuepukane naye. Tena tumuogope wala tusimtolee siri zetu.
Hapo zamani
palikuwa kuna bwana mmoja akiishi na mkewe. Lakini Mwenyezi Mungu hakuwapa
neema ya watoto. Akaamua ende akatafute mtumishi kijana mdogo ili aishi naye
humu nyumbani yeye na mkewe. (Kama mnavyojuwa zamani watoto walikuwa
wakiuzwa kama watumwa). Bwana akenda sokoni akatafuta kijana mpaka akampata.
Kabla ya kumnunua akamuuliza muuzaji. Vipi sifa za kijana huyu? Muuzaji
akajibu. Hodari lakini ana sifa moja tu! Ya namima. Bwana mnunuwaji akaiona
hiyo ni sifa ndogo tu haina madhara kwake, basi akamnunuwa. Kijana huyo
akaishi muda katika nyumba ile. Ilipofika taimu ya kuanza na tabia yake
mbaya ya kupeleka namima, akamuanzia bibie kwa kumwambia: Huyu mumeo ana
mwanamke mwengine nje na karibu hivi atakuwa hakujali tena. Bibie baada ya
kuyasikia maneno hayo roho ilimruka (kama ilivyo tabia ya wanawake wa siku
hizi wanaposikia waume zao wanataka kuengeza mke). Bibie akawa tayari afanye
kitu chochote kile ili bwana ampende yeye tu, akamuuliza yule kijana. Sasa
jee kuna dawa yoyote ya kuifanya. Kijana akajibu akasema: Ndio, dawa ipo.
Wewe nipatie ndevu za mumeo za nchani leo anapoingia kulala nenda na kiwembe
umkate kisha uniletee. Nitakufanyia dawa. Baada ya muda mdogo tu akatoka
kwenda kwa bwana wake ili amueleze yaliyo shari kuliko yaliyopita. Akasema
kumwambia bwana wake: Una habari ya kuwa huyu mkeo ana mwanamme mwengine na
wameshaamua wakuuwe ili waishi kwa raha yao. Na usiku wa leo kuwa na hadhari
kubwa huwenda ukauliwa. Bwana akawa hana raha. Ulipofika usiku kila mmoja
ana khofu ya ajabu. Bwana anaogopa kuuliwa na mke anataka ndevu. Bwana
akaingia chumbani kulala. Lakini hakulala kajitia tu kulala anamngojea huyo
atakaekuja ili apambane naye. Huku bibie kaona hivi sasa bwana tayari
kishalala niende nikazikate zile ndevu. Akachukuwa kiwembe chake
alipokurubia tu, bwana akaamka akamuona mkewe ana kiwembe kikali mkononi
akajuwa kwamba haya ni mauti na maneno aliyoambiwa ni ya kweli. Papo hapo
akamnyan’ganya mkewe kiwembe akakichukuwa kisha na kumchinja mkewe shingoni.
Watu wa mwanamke waliposikia mtoto wao kauliwa hawakukubali wakataka
kuchukuwa kisasi wakenda kumuuwa yule mume. Vile vile watu wa Mume nao
hawakukubali wakataka kuchukuwa kisasi. Ikabidi makabila mawili yapigane
siku nyingi kwa sababu ya kijana mwenye sifa ya namima.
Subhana
Llaah! Nadhani ndugu msomaji baada ya kisa hiki sina haja ya kurefusha sana
katika mada hii. Hayo ndio madhara ya namima. Kheri yote huondoka katika
nyumba yenye mtu kama huyo. Waislamu tahadharini na watu kama hawa. Ewe
Mwenyezi Mungu tuepushe nao na utulinde kwa nguvu zako (Amin). |