|
Unguja na Pemba zimefunguliwa madarasa za
kiarabu na dini. Kiasi ya madrasa 95, na zaidi ya walimu 100 wote wanataka
kulipwa. Kila mwalimu analipwa kiasi ya dola 30 kwa mwezi hivyo msaada wenu
tunauhitaji asikose mmoja wenu kumdhamini mwalimu mmoja.
Ujenzi wa Maahad ya Istiqaama ushafika nusu
mpaka hivi sasa, bado nusu ya pili na kumaliza kwake ni kheri yetu sote, kwa
hivyo unaombwa utowe mchango wako kadiri ya uwezo wako ili ikamilike na wewe
upate kuandikiwa sadaka jaria.
Maahad ya Istiqaama iliofunguliwa Unguja Iko
Tunguu inaendelea kuchukuwa wanafunzi kutoka kila Mkowa wa Tanzania na pia
nchi jirani . Pesa zinazohitajika kila mwezi zinakaribia dola elfu kumi na
nne ( $14000/-) .
Katika hiyo Maahad imefunguliwa skuli ya
kisasa ambayo wanafunzi watasoma masomo yote ya kiserekali na pia mafunzo ya
kiarabu na dini kwa jumla. Tumeanza kuchukuwa wanafunzi kutoka chumba cha
kwanza na itakua imefunguliwa kwa ajili ya wanafunzi wa kiislamu kutoka
Tanzania na nchi karibu. Mwanafunzi anatakiwa kulipa fees ambayo hatakuwa
kubwa.
Fees kwa kila mwanafunzi ni $35/-kwa kila
mwezi
Ukitaka kutuma mchango wako wa kumsponsa
mwanafunzi au kuchangia katika ujenzi tumia Banki ya OIB Al-Istqaama Al-khairiya
A/C 12-057808-03 Madinat Al-Nahdha Branch.
Pia mwelekeo wa sasa ni kufunguwa shule kama
hii kila Mtaawi ya Istiqaam kama:
Pemba: Karibu tutaanza katika ujenzi wa shule
na ukitaka kuchangia katika ujenzi, tumia Banki ya OIB Al-Istqaama Al-khairiya
A/C 12-057808-02 Madinat Al-Nahdha Branch. Pesa zitatumika katika
ujenzi, mishahara ya walimu wa madaris za Qur'n na ujenzi wa shule na
mengineo.
Uganda Bugiri: Karibu tutaanza katika kuanza
ujenzi wa secondary na ukitaka kuchangia katika ujenzi, tumia Banki ya OIB
Al-Istqaama Al-khairiya A/C 12-057808-01 Madinat Al-Nahdha Branch.
Pia katika akaunti hii tunapokea mchango wenu
kwa ajili ya mishahara ya walimu, kusponsa mwanafunzi, uchimbaji wa visima
huko Uganda na mengineo.
Ujenzi wa skuli ya secondari Mpanda Mkowa wa
Rukwa pia ushafika mbali wanaomba msaada wetu kifedha na pia anaetaka
kuuzuru mradi huu halmashauri ya Istiqaama ilioko huko iko tayari kumpokea
yeye na rai zake.
Ujenzi wa primary school ya Chumbageni Tanga
karibu itaanza lakini pesa za ujenzi bado hazijakamilika, tinaomba msaada
wenu.
Ukitaka kutuma mchango wako tumia akaunti ya
Al-Istiqama Al-Khaiyriya Alukhwer branch A/c 08-440661-01
Maendeleo ya madaris na misikiti katika
mikoa ya Bukoba na Tabora zinaendelea vizuri sana na imebidi kufungua hesabu
za benki kwa ajili ya tawi hizo mbili nazo ni:
Mkua wa Tabora:
Akaunti yake ya benki ni: Al-Istiqama Al-Khaiyriya
Alukhweir branch A/c 08-440661-02
Mkoa wa Kagera:
Akaunti yake ya benki ni: Al-Istiqama Al-Khaiyriya
Alukhweir branch A/c 08-440661-03
Pia Jumuiya hii ishaanza kupeleka wataalamu
katika baadhi ya Matawi ya jumuiya ili kufanya study ya kujenga primary
schools kwa ajili ya maendeleo ya watoto wetu kielimu na kupata akhlaki za
kiislamu.
Maendeleo ya madrasa za dini na kiarabu
Mikoani Bara zinaendelea vizuri mchango wenu unangojwa ili yapatikane
mafanikio mazuri.
2.Jumuiya ya waarabu wa KI OMANI Burundi na
matawi yake: ROMONGE KITEGA,KIRUNDO,NGOZI NA RUYIGI. Jumuiya hii inadhamiria
kujenga primary na secondari school na sisi tunatakiwa sote tushirikiane nao
kifedha. Wanachama wa Jumuiya hiyo wamejitahidi kujenga maduka ni mradi wa
kuingiza pesa za kuendeshea kazi za msikiti wao, na pia wemejenga maktaba
kubwa na vitabu pamoja na mahitajio mengine vimepelekwa na Jumuiya.
Ujenzi wa maktaba katika Tawi la Gitega
imesimama kutokana na upungufu wa pesa, kwa hivyo tunaombwa sote
tushirikiane nao.
3.Jumuiya ya waarabu wa KIOMANI RWANDA na
matawi yake: BUTARE, RWAMAGANA na KIGALI . Ndugu zetu hawa wanania ya
kujenga misikiti mitatu mmoja Kigali, mmoja Butari na mwengine Ruwamagana
Pamoja na madarasa ya kusomesha Dini na Lugha wanaomba msaada wenu.
4. Jumuiya ya Istiqaama Ghana na matawi yake
Acra, Wenchi, Kumasi, Wa, Bandankwanta, Budu, Subinsu, Sinyani, Kintanbu
zinaendelea kuimarisha kazi za Istiqaama na Jumiya imeweza kuwasaidia katika
ujenzi wa misikiti miwili na madarasa ya dini na lugha ya kiarabu na skuli
ya primary na secondary na Maktaba na kufundisha ushoni kwa wanawake, pia
imewezekana kuwanunulia Ardhi ya ziraa ili waweze kuiamirisha kwa ajili ya
chakula ya wananchi masikini.
5. Jumuiya ya Istiqaama Mali na matawi yake
Wanahitaji misikiti miwili kila msikiti utagharimu $35000/- pia shule
itagharimu $40000/-
Angalia: -
Hii juhudi tunayochukuwa kwa upande wa pili
ni kupigana na Mayahudi na Manasara, ambao wanaingia kwa juhudi kubwa katika
jamii ya Kiislamu . Mfano wahayo ni kuanzisha skuli za malezi (nursery)
ambao wanawafundisha watoto wa kiislamu kuwa yesu ni bora kuliko Nabii
Muhammad na mengineo ya upotefu.
Pili wananunuwa ardhi za Waislamu kwa bei
kubwa na kujenga makanisa.
Tatu wanatoa misaada kwa masikini kama
kuwalea wazee na kujenga spitali kwa malipo madogo sana.
Nne wanatoa vipindi vya mafunzo ya dini yao
katika radio na TV.
Ili Waislamu waweze kujilinda na dhamiri zao
hizi ni jukumu letu kuwaokoa ndugu zetu huko kwa hali na mali , na kujiokoa
nafsi zetu siku ya hesabu.
|