MAANA YA SAUMU

Saumu imehusiwa jambo muhimu ambalo halipo katika ibada nyinginezo kuwa ukweli wa hiyo Saumu kwa mwenye kufunga hakuna anaoujua isipokuwa Mwenyezi Mungu (Subhanahu Wa Taalah) kwa hivyo Amesema Subhanahu Wa Taalah:

( الصوم لي وأنا أجازي به الجنة )

“Saumu ni yangu mimi na mimi namlipa (huyo anaefunga) kwa hiyo (Saumu) Pepo”.

Na juu ya kuwa Ibada zote ni zake yeye tu Mwenyezi Mungu (Subhanahu Wa Taalah) (lakini imestitiziwa kwa daraja kubwa iliyopewa kwani mtu aweza kudai amefunga lakini akiwa peke yake huenda akala au akanywa kwa hivyo ukweli wake anaujua Subhanahu Wa Taalah pekee). Na katika hekima zake kuwa inaondoa maradhi na inasafisha akili na hutia nuru katika undani wa mwili (yaani moyo ukipata nuru anaepukana mtu ni riyaa, hasadi, chuki, kibri etc) na humpa mtu nguvu ya kufanya ibada na huizowesha nafsi kuhimili njaa ili iweze kusubiria mashaka ya maisha, na kadhalika Saumu humfanya mtu aweze kupigana vita na magonjwa ya nafsi na kumtakasa nayo na kumfanya awe na huruma juu ya mafakiri na wenye shida. Kuhusishwa Saumu na Mwezi wa Ramadhani ni kwa ajili ya kuhuyisha kumbu kumbu ya kuteremka kwa Qur'an ili iwe uongozi kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongozi na upambanuzi (wa baina ya haki na batili) na ni kitu cha tabia kwa watu wa Qur'an kuisherehekea kumbu kumbu hii na kujikaribisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kuishukuru neema hii yenye kulinda mabaya.

Saumu maana yake katika lugha ni kukamata (kuzuia) na maana yake katika Sheria ni kuzuiya yafikayo ndani ya mwili kutoka nje yake na jimaa na madhambi makubwa kwa kutiya niya kutoka Al-Fajiri mpaka kuzama jua (Magharibi) kwa kauli ya Mwenyezi Mungu (Subhanahu Wa Taalah) :-

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ (183) أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ وَأَن تَصُومُواْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ (184)  شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلاَ يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُواْ الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُواْ اللّهَ عَلَى مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ (185)

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ فَلْيَسْتَجِيبُواْ لِي وَلْيُؤْمِنُواْ بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ (186)

أُحِلَّ لَكُمْ لَيْلَةَ الصِّيَامِ الرَّفَثُ إِلَى نِسَآئِكُمْ هُنَّ لِبَاسٌ لَّكُمْ وَأَنتُمْ لِبَاسٌ لَّهُنَّ عَلِمَ اللّهُ أَنَّكُمْ كُنتُمْ تَخْتانُونَ أَنفُسَكُمْ فَتَابَ عَلَيْكُمْ وَعَفَا عَنكُمْ فَالآنَ بَاشِرُوهُنَّ وَابْتَغُواْ مَا كَتَبَ اللّهُ لَكُمْ وَكُلُواْ وَاشْرَبُواْ حَتَّى يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ ثُمَّ أَتِمُّواْ الصِّيَامَ إِلَى الَّليْلِ وَلاَ تُبَاشِرُوهُنَّ وَأَنتُمْ عَاكِفُونَ فِي الْمَسَاجِدِ تِلْكَ حُدُودُ اللّهِ فَلاَ تَقْرَبُوهَا كَذَلِكَ يُبَيِّنُ اللّهُ آيَاتِهِ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَّقُونَ (187)   سورة البقرة

(Aya ya 183 – 187 ya sura Al-Baqarah)

Enyi Mlioamini mmelazimishwa kufunga (Saumu) kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu (183) Siku chache tu (kufunga huko). Na atakayekuwa mgonjwa au katika safari (akafunga baadhi ya siku) basi atimize hisabu katika siku nyingine. Na wale wasioweza, watoe fidia kwa kumlisha masikini. Na atakayefanya wema kwa radhi ya nafsi yake, binafsi ni bora kwake. Na huku kufunga ni bora kwenu ikiwa mnajua (haya sasa basi fuateni) (184) (Mwezi huo mlioambiwa mfunge) ni Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa katika (mwezi) huo hii Qur'an ili iwe uongozi kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongozi na upambanuzi (wa baina ya haki na batili). Atakayekuwa katika mji katika huu mwezi (wa Ramadhani) afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi (atimize) hisabu (ya siku alizowacha kufunga) katika siku nyingine. Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, na pia (anakutakieni) kumtukuza Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongozeni, ili mpate kushukuru (185) Na waja wangu watakapo kuuliza hakika yangu (waambie kuwa) Mimi niko karibu nao. Naitika maombi ya mwombaji anaponiomba. Basi na waniitikie na waniamini, ili wapate kuongoka (186) Mmehalalishiwa usiku wa Saumu kuingiliana na wake zenu. Wao ni (kama) nguo kwenu (zilizokugandeni mwilini) na nyinyi ni (kama) nguo kwao. Mwenyezi Mungu anajua kwamba mlikuwa mkizihini nafsi zenu. Kwa hivyo amekukubalieni toba yenu na amekusameheni. Basi sasa changanyikeni nao na takeni aliyokuandikieni Mwenyezi Mungu. Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa Alfajiri katika weusi wa usiku. Kisha timizeni Saumu mpaka usiku. Wala msichanganyike nao, na hali mnakaa Itikafu msikitini. Hiyo ni mipaka ya Mwenyezi Mungu, basi msiikaribie. Namna hivi Mwenyezi Mungu anabainisha hoja zake kwa watu ili wapate kumcha (187).

Na anasema Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) :

( من صام رمضان إيمانا واحتسابا غفر له ما تقدم من ذنبه و من قام رمضان إيمانا و احتسابا و من قام ليلة القدر غفر له ما تقدم من ذنبه )

Anaefunga Ramadhani hali yakuwa anaamini (wajibu wa kufunga Mwezi huu na kuwa ni faradhi juu yake) na atarajia malipo mazuri (kwa Mwenyezi Mungu) basi hughufiriwa madhambi yake yote yaliyopita, na anaesimama (kusali Sala za usiku katika mwezi wa) Ramadhani hali ya kuwa anaamini na atarajia malipo mazuri na anaesimama (kufanya ibada) usiku wa Al-Qadar (Laylatu Al-Qadari) hughufiriwa madhambi yake yote yaliyopita.

Maana ya إيمانا  yaani anaamini kuwajibika kwa kitendo hicho alichokifanya (hapa ni Saumu).

Maana ya  احتسابا  yaani atiye niya kuwa anafanya kitendo hichi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu atarajia kwa kitendo hicho thawabu yake tu bila ya kuwa na lengo lingine.

Na iwapo atachanganya niya hiyo pamoja na niya nyingine haitakuwa احتسابا  kwa mujibu ya kauli yake Subhanahu Wa Taalah katika hadithi Qudisiy:-

( من عمل عملا أشرك فيه غيري فهو له و أنا أغنى الشركاء )

Mwenye kufanya jambo akamshirikisha ndani yake aliyekuwa mwengine sie mimi (Mwenyezi Mungu (Subhanahu Wa Taalah)) basi hilo (jambo) ni lake yeye (huyo aliyemshirikisha) na mimi sina haja na washirika (mwenye kutohitajia washirika) na hili ni shuruti la kwanza na shuruti la pili la kughufiriwa madhambi (masharti haya mawili yanayomuwajibikia anayefunga na anaye simama usiku mwezi wa Ramadhani ili aghufiriwe madhambi yake yote aliyoyafanya kabla) ni kuwa mwenye kufunga na mwenye kusali usiku asiwe anaendelea kufanya dhambi kubwa katika haki za Mwenyezi Mungu (Subhanahu Wa Taalah) (kama kuacha kusali, kutoa Zaka au kunywa pombe etc) au kuwadhulumu waja wake kwani wako wanaofunga na kusali Qiyamu alleyl na hali bado ameshikilia kufanya madhambi makubwa na kwadhulumu waja wa Mwenyezi Mungu (binaadamu wenzake) basi hadithi hiyo juu ya kughufuriwa madhambi haimkhusu yeye kwa sababu hadithi hii siyo kwa kila anayefunga na kufanya ibada usiku na ikiwa hivyo itakuwa kinyume na aqiida ya Kiislamu ili sahihi.

Na katika hadithi nyingine inayotoa dalili ya kuwajibika kwa Saumu ya Ramadhani ni ile hadithi aliyoitoa Salman Al-Faarisiy R.A. amesema: Ametuhutubia Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) katika siku ya mwisho wa Mwezi wa Shaabani akasema:-

 (يا أيها الناس قد أظلكم شهر عظيم شهر مبارك شهر فيه ليلة خير من ألف شهر جعل الله صيامه فريضة و قيام ليلة طوعا و من تقرب فيه  بخصلة من الخير كان كمن أدى فريضة و من أدى فريضة فيه كان كمن أدى سبعين فريضة فيما سواه و هو شهر الصبر , و الصبر ثوابه الجنة , و شهر المواساة و شهر يزاد فيه رزق المؤمن , من  فطر فيه صائما  كان مغفرة لذنوبه و عتق رقبته من النار , و كان له مثل أجره من  غير أن ينقص من أجره شئ , قلنا يا رسول الله ليس كلنا يجد ما يفطر به الصائم فقال رسول الله صلى الله عليه و سلم يعطي الله هذا ثواب من فطر صائماً على مذقة  لبن أ, تمرة أو شرب من الماء , و من أشبع صائما سقاه الله من حوضي شربه لا يظمأ حتى يدخل الجنة و هو شهر أوله رحمة و أوسطه مغفرة و أخره عتق من النار و من خفف عن مملوكه فيه غفر الله له ما و أعتقه من النار

“Enyi Watu kimewafunika kivuli cha mwezi mtukufu, mwezi wenye baraka, mwezi ndani yake kuna usiku ulio bora kuliko miezi elfu (yaani “Laiylatul Qadri”), Mwenyezi Mungu amejaalia kuufunga (huo mwezi) ni faradhi na kusali Sala za usiku (Qiyaamul leyl) jambo la kujitolea kulifanya (lina malipo mazuri) na anaejikaribisha kwa jambo la kheri ni kama aliefanya faradhi na aliyefanya faradhi katika mwezi huu ni kama aliyefanya faradhi sabiin katika miezi mingine, nao ni mwezi wa subira na subira thawabu yake ni Pepo (Al-Jannah) na ni mwezi wa maliwaza, mwezi inaongezwa ndani yake riziki ya Muumini, anaemfuturisha ndani yake mwenye kufunga hughufiriwa madhambi yake na hukombolewa shingo yake (yaani yeye mwenyewe) kutoka Motoni na hupata malipo kama malipo yake (huyo aliyefuturishwa) bila ya kupungua kitu katika malipo yake, tukasema ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu sio kila mmoja wetu anacho cha kumfuturishi aliyefunga akasema Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) : Anampa Mwenyezi Mungu thawabu hii anaemfuturisha aliyefunga kwa muonjo wa maziwa au tembe ya tende au funda la maji na anaemshibisha aliyefunga Mwenyezi Mungu atamnywesha katika Hodhi langu kinywaji ambacho (kitamfanya) hatapata kiu mpaka aingie Peponi, na mwezi mwanzo wake ni Rehema na kati kati yake ni Maghufira na mwisho wake ni kukombolewa Motoni na yule anaempunguzia mtumwa wake Mwenyezi Mungu humghufiria na kumkomboa Motoni”.

Sababu ya kuileta hadithi kwa kirefu ni kupata faida na huenda Mwenyezi Mungu (Subhanahu Wa Taalah) akajaalia (miongoni mwa wasomaji) atakayetekeleza yaliyomo humo na nitapata mimi sehemu katika hayo malipo kwa sababu anayeionyesha kheri ni kama yule aliyoifanya kheri hiyo.