LENGO NA MADHUMUNI YA  JUMUIYA

 

Lengo kubwa la Jumuiya ni kujenga na kuendeleza sekta zake ili kufikia kwenye dhamira yake ya kujenga Taifa imara.

Kwa kutekeleza jukumu hilo, Jumuiya ya Istiqama International imepania kutumia uwezo wake wote kutekeleza:

a.    Kujenga itiqadi na upeo wa elimu ya utamaduni na silka njema.

b.    Kutilia mkazo umuhimu wa elimu pamoja na kuongeza viwango vya elimu.

c.    Kusidia na kubuni njia za kuongeza ajira kwa wananchi.

d.    Kusaidia hali mali kuendeleza sekta za afya kwa jumla na hasa kwa mama na watoto.

e.    Kupunguza umasikini.

f.     Kumuendeleza mwanamke katika jamii.

 

Madhumuni ya Jumuiya:

Pia Jumuiya Ina madhumuni mengine kama ifuatavyo:

1. Kueneza (kufanya daawa) taaluma juu ya ukweli wa dini ya kiislamu. 

2. Kuwaita watu katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa kuwaelimisha juu ya dini yao.

3. Kushirikiana na Jumuiya nyengine za kiislamu katika kuwasaidia maskini na wahitaji:

"Kushirikiana na kusaidiana katika kumcha na kumuogopa Mwenyezi Mungu"

 

Copyright ©2004  Uislam.net