|
|
HUKUMU YA KUVAA
NGUO NDEFU KWA MWANAMME |
Imethibiti katika Hadithi
nyingi sana za Mtume (S.A.W) kwamba kasema:
“Nguo
ya Mwislamu mwanamume mpaka nusu ya miguu, na hapana ubaya kuwa baina ya
magoti na baina ya vifundo vya miguu. Na Mwenyezi Mungu hamtazami mwanamme
anayeburura nguo yake kwa majivuno”
Pia akasema Mtume (S.A.W)
katika Hadithi nyengine:
“Kila
nguo inayogusa chini (kwa urefu wake basi katika moto”
Na akasema (S.A.W):
“Ionekane miguu katika
kuvaa kikoi (nguo)”.
Na kwa hakika Mtume (S.A.W)
alimuona mwanamme anaburura nguo akamkataza kufanya hivyo, na akasema yule
kijana: “Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Hakika mimi miguu yangu ni myembamba
iliyokonda sana (ninaificha isionekane). Mtume (S.A.W) akasema: “Kila umbo
la Mwenyezi Mungu ni zuri”.
Na Hadithi kuhusu jambo hili
(la kukatazwa kuvaa nguo refu) ni nyingi sana na ahadi ya kupata adhabu
ngumu kwa kuvaa nguo ndefu. Na Mtume (S.A.W) alimuona mwamame anasali naye
amevaa nguo ndefu akamwamrisha arudie kutia udhu mara mbili, akaulizwa Mtume
(S.A.W). Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mbona umemwamrisha kutia udhu mara
mbili? Akasema Mtume (S.A.W):
“Hakika amesali na nguo yake ndefu na
Mwenyezi Mungu haikubali sala ya mwenye nguo ndefu”.
Pia akasema Mtume (S.AW):
“Mwenye
kusali na nguo ndefu basi sala yake si chochote kwa Mwenyezi Mungu."
Yaani sala yake haikubaliwi. Na kwa haya inatosha kuwa ni
dalili kubwa ya kuwa kuvaa nguo ndefu ni katika madhambi makubwa na sala ya
mwenye nguo ndefu haikubaliwi na haijuzu asalishe au kuwa ni Imamu.
Na Allah ndie ajuwae zaidi.
|