NGUZO YA ZAKA:
Zaka imewajibishwa kuwa ni nguzo ya
Uislamu kwa wale wote wenye uwezo, na ALLAH ndiye aliyewapa huwo uwezo. Elimu
yake ALLAH haina mipaka, kwa hivyo inawafikia wote. Pia kwa hikima yake ALLAH
(S.W.T) amejaalia waja masikini na fukara. Kwa hakika zaka imetajwa mara
nyingi katika Qur-aan kama ilivyotajwa sala ili tufahamu umuhimu wake.
JUKUMU LA JUMUIYA YA
ISTIQAMA:
Kwa kuwa Jumuiya Istiqaama Al-Khairiya,
na shughuli zake zote zimejifunga na sheria zote za Kiislamu, imeamua
kushughulikia suala la zaka kikamilifu.Tayari Jumuiya inao uwezo na uzoefu wa
muda mrefu katika kugawa zaka.
FAIDA YA KULETA ZAKA
ISTIQAMA:
Inajulikana kuwa kila mwenye kutoa zaka
anakuwa na jamaa zake na watu wake wa karibu nay eye. Lakini pia kama atagawa
sehemu ya zaka yake na kupitisha Istiqama atapata faida kubwa, kwani
zitachanganywa pamoja na watu wengi zaidi, na kurejea kwa faida kwa mtoaji
kutatokea kila pembe.
Tunatanguliza na kutaraji mashirikiano
mema katika kutimiza wajibu wetu na kupata malipo mema kutoka kwa ALLAH KARIMU.