|
KUSEMANA
Kasema
Mwenyezi Mungu Katika Suratil Hujuraat Aya ya (12):
( íóÇÃóíøõåóÇ ÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇ
ÇÌúÊóäöÈõæÇ ßóËöíÑðÇ ãöäú ÇáÙøóäøö Åöäøó ÈóÚúÖó ÇáÙøóäøö ÅöËúãñ æóáóÇ
ÊóÌóÓøóÓõæÇ æóáóÇ íóÛúÊóÈú ÈóÚúÖõßõãú ÈóÚúÖðÇ ÃóíõÍöÈøõ ÃóÍóÏõßõãú Ãóäú
íóÃúßõáó áóÍúãó ÃóÎöíåö ãóíúÊðÇ ÝóßóÑöåúÊõãõæåõ æóÇÊøóÞõæÇ Çááøóåó Åöäøó
Çááøóåó ÊóæøóÇÈñ ÑóÍöíãñ)
Maana yake:
“Enyi mlioamini jiepusheni sana na kuwadhania watu
dhana mbaya, kwani kuwadhania watu dhana mbaya ni dhambi. Wala musipeleleze
habari za watu. Wala baadhi yenu wasiwasengenye (wasiwaseme) wengine. Jee!
Mmoja wenu anapenda kula nyama ya nduguye aliyekufa? Laa hampendi, basi na
haya musiyapende. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Bila shaka Mwenyezi Mungu ni
mwenye kupokea toba na mwingi wa kurehemu”.
Ndungu
yangu Muislamu tazama ubaya wa kitendo hiki, mpaka Mwenyezi Mungu
akakifananisha na kumla nyama mwenzako. Yaana wewe anapokaa ukamsema
mwenzako kwa ubaya, basi ni sawa na kumla nyama yake mbichi. Kitendo ambacho
kimeharamishwa katika Sheria za Mwenyezi Mungu. Na ni katika madhambi
makubwa yanayochumwa na ulimi. Khasa pale wanapokutana watu katika vikao
vyao. Na Mtume (S.A.W) kabainisha wazi wazi ubaya wa jambo hili, na
akawafafanulia watu ili wajue katika hali gani mtu huwenda akachuma dhambi
hii. Katika Hadithi iliyotolewa na Imam Muslim na Tirmidhi na Ahmad na
wengineo kwa njia ya Abu Hurairah. Kasema Bwana Mtume (S.A.W):
( ÃóÊóÏúÑõæäó ãóÇ ÇáúÛöíÈóÉõ
ÞóÇáõæÇ Çááøóåõ æóÑóÓõæáõåõ ÃóÚúáóãõ ¡ ÞóÇáó: ÐößúÑõßó ÃóÎóÇßó ÈöãóÇ
íóßúÑóåõ ¡ Þöíáó: ÃóÝóÑóÃóíúÊó Åöäú ßóÇäó Ýöí ÃóÎöí ãóÇ ÃóÞõæáõ ¡ ÞóÇáó:
Åöäú ßóÇäó Ýöíåö ãóÇ ÊóÞõæáõ ÝóÞóÏö ÇÛúÊóÈúÊóåõ æóÅöäú áóãú íóßõäú Ýöíåö
ÝóÞóÏú ÈóåóÊøóåõ )
Maana yake:
“Mnajua nini maana ya (Al Ghayba)? Wakasema: Mwenyezi
Mungu na Mjumbe wake ndie Wajuwae. Akasema (S.A.W): Kumsema ndugu yako kwa
yale anayoyachukia. Akaulizwa: Unaonaje ikiwa ndugu yangu anayo kweli yale
ninayomsema. Akasema (S.A.W): Ikiwa kweli anayo unayoyasema juu yake ndio
hiyo ghaiba (ni kumsema) na kama hana yale unayoyasema juu yake ndio utakuwa
umemzuliya uwongo mkubwa.”
Kwa hivyo
hata kama kweli ndugu yako Muislam ana sifa fulani si nzuri, wewe wajibu
wako kumsitiri wala usimfedheheshe mbele za watu. Kwa mfano mtu kilema au
ana upungufu katika maumbile fulani, basi ni haramu kukaa mkamsema kwa sifa
zake hizo alizoumbiwa na Mola wake. Jee wewe unamtoa makosa Muumbaji. Jee
wewe unaweza kuumba?
Katika
Hadithi iliyotolewa na Imam Ahmad ya kwamba: “Mwanamke mmoja aliingia kwa
Mtume (S.A.W) na bibi Aisha yupo. Alipotoka yule mwanamke. Bibi Aisha
akasema: Mfupi! Mtume (S.A.W) akahamaki sana na kumwambia bibi Aisha: (Umeshamsema).
Bibi Aisha akasema: Sikutaja ila sifa aliyonayo. Hapo Mtume (S.A.W) akasema:
Ndio, lakini umetaja ile sifa mbaya aliyonayo.”
Watu lazima
watahadhari na mambo kama haya. Wengi wetu hatujali nini tunachokisema wala
kulifikiria neno. Maisha ya wengi wetu yamejaa maneno kama haya. Kuna
wengine hufungua kinywa asubuhi wanapoamka kwa kula nyama za wenziwao.
Sikilizeni hii Hadithi kutoka kwa Mtume (S.A.W) kisha tujuwe kwamba kweli
wengi wetu wanawasema watu. Hadithi hii iliyopokelewa na Jabir bin Abdillahi
Radhi za Mola juu yake kasema:
“Ulipiga
upepo unao hafuru mbaya wakati wa Mtume (S.A.W). Akasema: Kuna watu
wanafiki wanawasema waumini, kwa hivyo ndio upepo huu wenye harufu mbaya
ukaja”
Waliulizwa
Maulamaa ya kwamba mbona upepo kama huu siku hizi haupo tena. Akasema: Upo
lakini watu hawauhisi, kwa sababu pua zao zimeshakufa. Kama vile unapoingia
katika nyumba inayoanikwa ngozi na kuchunwa. Wewe mgeni utahisi, lakini wale
wenyewe hata habari hawana.
Kwa hivyo
hii inamaanisha wazi wazi ya kuwa watu wamebobea katika kusemana. Roho
zimekuwa chafu. Dhana mbaya imezidi baina ya watu. Waislamu wamekuwa hawana
mapendano baina yao. Kila mmoja anamuona mwenzake kama adui. Kusaidiana
hawataki, kila mmoja anajitenga na wenzake. Ndio tukafika hali ya
kudhalilishwa tukawa wa mwisho hatuna letu moja. Damu yetu imekuwa rahisi
katika mikono ya Mayahudi. Hawasemi kitu wakakubaliana. Mambo yao hayendi
mbele yakadumu. Maisha yao hayana baraka. La hawla wala Quwata ila billahi.
!
Waislamu
amkeni. Rudini katika utukufu wenu aliokutakieni Mola wenu. Msipupe huku na
kule kama mliokuwa hamna muongozo unakuongozeni.
Turudieni
kwa Mola wetu. Tupendane na tuwe kitu kimoja. Ndio tutawashinda Makafiri na
kurudisha haki zetu. Tuwache kusemana na kulana nyama baina yetu.
Ewe mwenye
kula nyama ya mwezio hukusikia Hadithi ya Mtume. Iliyotolewa na Imam Al
Bukhari na Abu Daud. Kasema Mtume (S.A.W):
( áóãøóÇ ÚõÑöÌó Èöí ãóÑóÑúÊõ ÈöÞóæúãò
áóåõãú ÃóÙúÝóÇÑñ ãöäú äõÍóÇÓò íóÎúãõÔõæäó æõÌõæåóåõãú æóÕõÏõæÑóåõãú ÝóÞõáúÊõ
ãóäú åóÄõáóÇÁö íóÇ ÌöÈúÑöíáõ ÞóÇáó åóÄõáóÇÁö ÇáøóÐöíäó íóÃúßõáõæäó áõÍõæãó
ÇáäøóÇÓö æóíóÞóÚõæäó Ýöí ÃóÚúÑóÇÖöåöãú )
Maana yake:
“Nilipopandiswa mbinguni niliwapitia watu wana makucha
na shaba, huku wakijipara nyuso zao na vifua vyao. Nikamuuliza Jibril, nani
hawa? Akasema Jibril: Hawa ni wale watu waliokuwa wakila nyama za watu (wanawasema)
na kuwatukana wenziwao.”
WATU
WANAOFAA KUWASEMA:
Kuwasema
watu ni haramu tena inaleta chuki baina yao. Kwai hatoridhika mwenye kusemwa
kama atasikia. Lakini kuna wakati ni lazima kuwatahadharisha wenzako kama
kuna shari au jambo la kuwadhuru. Kwa hivyo ikiwa kuna mtu kazi yake
kusambaza bidaa au mambo machafu. Lazima watu watahadharishwe na shari ya
mtu huyo ili wapate kumjuwa. Lakini isiwe kumsema huko katika sifa za
maumbile kama sura yake au nguo zake au kitu kinachomuhusu alichoumbwa
nacho. Isipokuwa zisemwe zile sifa zake ili watu waepukane nazo. Na walisema
wanavyuoni ya kwamba watu watatu inafaa kuwasema nao ni: Kila mfalme mwenye
kudhulumu. Na Mtu aliye Fasik mtenda maasi mbele za watu. Na mwenye kuzuwa
bidaa. Katika Hadithi iliyopokelewa na Imam … Kasema Mtume (S.A.W):
(ÃÐßÑæÇ ÇáÝÇÌÑ ÈãÇ Ýíå áßí
íÍÐÑå ÇáäÇÓ)
Maana yake:
“Mtajeni mtu mbaya kwa yale mabaya yake. Ili watu
watahadhari naye”.
Na kuna
Maulamaa wengine wamesema ya kuwa inaruhusiwa kumsema mtu ikiwa
mutashitakiana ikiwa kakudhulumu haki yako, kwa hivyo inajuzu kumsema mbele
ya hakimu au mfalme kwa ile dhulma aliyokufanyia ili upate haki yako.
Ndugu zangu
Waislamu hebu kila mmoja kati yetu ajiulize mara ngapi tunawasema watu au
tunashirikiana katika kuwasema watu. Na unatakiwa uwondoke katika vikao kama
hivyo, kwani kukaa kwako ndio kusikiliza. Lazima watu watahadhari. Haya ni
maradhi makubwa yamewapata Waislamu. Tunamuomba Allah atuondoshee maradhi
haya mabaya na izipatanishe nyoyo za waja wake wema wawe wanapendana na
kusikilizana katika kila jamabo lao (Amin).
|