Madhambi ya ulimi

KUSEMA UWONGO

Kusema uwongo ni katika sifa mbaya itakayomfanya mwenyewe atoke katika kundi la watu waumini. Kwani huwenda Muumini akawa na fisa nyengine kama za ubakhili au woga. Lakini akishakuwa ni muwongo basi si Muumini tena. Imani hutoka katika moyo wake akawa miongoni mwa kundi jengine la wasemao uwongo. Yote haya yamebainishwa katika Quraan na Hadithi za  Bwana Mtume (S.A.W). Kasema Mwenyezi Mungu katika Suratin Nahal Aya ya (105):

(ÅöäøóãóÇ íóÝúÊóÑöí ÇáúßóÐöÈó ÇáøóÐöíäó áóÇ íõÄúãöäõæäó ÈöÂíóÇÊö Çááøóåö æóÃõæúáóÆößó åõãú ÇáúßóÇÐöÈõæäó)

Maana yake: “Wanaozuwa uwongo ni wale wasioziamini Aya ya Mwenyezi Mungu, na hao ndio waongo”.

Na akasema tena katika Sura hiyo hiyo ya Nahal  Aya ya (116):

( æóáóÇ ÊóÞõæáõæÇ áöãóÇ ÊóÕöÝõ ÃóáúÓöäóÊõßõãú ÇáúßóÐöÈó åóÐóÇ ÍóáóÇáñ æóåóÐóÇ ÍóÑóÇãñ áöÊóÝúÊóÑõæÇ Úóáóì Çááøóåö ÇáúßóÐöÈó Åöäøó ÇáøóÐöíäó íóÝúÊóÑõæäó Úóáóì Çááøóåö ÇáúßóÐöÈó  áóÇ íõÝúáöÍõæäó ).

Maana yake: “Wala msiseme, kwa sababu ya uwongo usemao ndimi zenu. (Hii ni halali na hii ni haramu), msije mkamzuliya Mwenyezi Mungu uwongo. Hakika wale wanaomzulia Mwenyezi Mungu uwongo hawatafaulu.”

Na katika Hadithi iliyotolewa na Imam Malik na Adarami:

 ( Þöíáó áöÑóÓõæáö Çááøóåö Õóáøóì Çááøóåã Úóáóíúåö æóÓóáøóãó Ãóíóßõæäõ ÇáúãõÄúãöäõ ÌóÈóÇäðÇ ÝóÞóÇáó äóÚóãú ÝóÞöíáó áóåõ Ãóíóßõæäõ ÇáúãõÄúãöäõ ÈóÎöíáðÇ ÝóÞóÇáó äóÚóãú ÝóÞöíáó áóåõ Ãóíóßõæäõ ÇáúãõÄúãöäõ ßóÐøóÇÈðÇ ÝóÞóÇáó áóÇ )

Maana yake: “Aliulizwa Mtume (S.A.W) jee eti mtu Muumini huwa moga? Akasema ndio. Akaulizwa tena eti Muumini huwa bakhili, akasema ndio. Kisha akaulizwa tena, mtu Muumini huwa muwongo. Akasema Laa. (Muumini hawi muwongo)”.

Kwa hivyo akishakuwa mtu ana sifa ya kusema uwongo, basi hata ushahidi wake haukubaliwi. Tena itabidi watu waepukane nae, kwani huyo ni mtu wa hatari. Na Akhera ana adhabu kali kama alivyoeleza Mwenyezi Mungu katika Suratil Baqarah Aya ya (10):

( Ýöí ÞõáõæÈöåöãú ãóÑóÖñ ÝóÒóÇÏóåõãú Çááøóåõ ãóÑóÖðÇ æóáóåõãú ÚóÐóÇÈñ Ãóáöíãñ ÈöãóÇ ßóÇäõæÇ íóßúÐöÈõæäó)

Maana yake: “Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi, na watakuwa na adhabu iumizao kwa sababu ya kule kusema kwao uwongo”.

Na Mtume kaeleza hayo hayo katika Hadithi iliyotolewa na Imam Al Bukhari na wengineo:

( Åöäøó ÇáÕøöÏúÞó íóåúÏöí Åöáóì ÇáúÈöÑøö æóÅöäøó ÇáúÈöÑøó íóåúÏöí Åöáóì ÇáúÌóäøóÉö æóÅöäøó ÇáÑøóÌõáó áóíóÕúÏõÞõ ÍóÊøóì íóßõæäó ÕöÏøöíÞðÇ æóÅöäøó ÇáúßóÐöÈó íóåúÏöí Åöáóì ÇáúÝõÌõæÑö æóÅöäøó ÇáúÝõÌõæÑó íóåúÏöí Åöáóì ÇáäøóÇÑö æóÅöäøó ÇáÑøóÌõáó áóíóßúÐöÈõ ÍóÊøóì íõßúÊóÈó ÚöäúÏó Çááøóåö ßóÐøóÇÈðÇ)

Maana yake: “Kwa hakika ukweli unapeleka katika ucha Mungu. Na ucha Mungu unapeleka Peponi. Na mtu husema ukweli mpaka aandikwe kuwa yeye ni Mkweli.  Na hakika uwongo unapeleka katika upotofu (madhambi) na madhambi hupeleka Motoni. Na mtu huzoweya kusema uwongo mpaka aandikwe kwa Mwenyezi Mungu kuwa yeye ni Muongo.”

Tunamuomba Mola atuepushe na sifa kama hii. Ukishaandikwa mbele ya Mwenyezi Mungu ya kuwa wewe ni msema uwongo unataka nani tena akusaidie. Hakuna ila kuwacha tu sifa kama hiyo na kurudia upesi kwa Allah na kufanya tawba na kuomba msamaha kwake

Na kusema uwongo ni katika sifa kubwa za watu wanafik., ambao hawana bahati yoyote katika Uislamu. Bali wao wanaitwa watu wenye nyuso mbili. Katika Hadithi iliyotolewa na Imam Al Bukhari na Muslim. Kasema Mtume (S.A.W):

( ÃóÑúÈóÚñ ãóäú ßõäøó Ýöíåö ßóÇäó ãõäóÇÝöÞðÇ ÎóÇáöÕðÇ æóãóäú ßóÇäóÊú Ýöíåö ÎóÕúáóÉñ ãöäúåõäøó ßóÇäóÊú Ýöíåö ÎóÕúáóÉñ ãöäó ÇáäøöÝóÇÞö ÍóÊøóì íóÏóÚóåóÇ ÅöÐóÇ ÇÄúÊõãöäó ÎóÇäó æóÅöÐóÇ ÍóÏøóËó ßóÐóÈó æóÅöÐóÇ ÚóÇåóÏó ÛóÏóÑó æóÅöÐóÇ ÎóÇÕóãó ÝóÌóÑó )

Maana yake: “Mtu mwenye hizi sifa nne huwa ni munafiki wa kweli. Na atakaekuwa na sifa moja tu kati ya hizi basi huwa na sifa ya unafiki mpaka aiwache. Atakapo pewa amana hukhuni. Na atakaposema husema uwongo. Na atakapotowa ahadi hatekelezi. Na atakapogombana huzidisha ugonvi ukawa hawishi (wakapatana)”.

Je uko tayari ufufuliwe na wanafiki siku ya Kiama. Kwani ukifa na sifa hizi basi utafufuliwa na wenzako wenye sifa kama hizi za unafiki. La hutaki na unaogopa basi jirekebishe kabla wakati haujesha.

Na Uislamu kama ulivyokazata sifa hii mbaya, basi ukaamrisha kusema ukweli katika kila jambo. Kwani kusema ukweli ni katika sifa kubwa za Waumini. Basi lazima kila Muislamu aulazimishe ulimi wake katika kusema ukweli ili awe miongoni mwa wanaosifika na sifa kama hii tukufu.  Mtume (S.A.W) alikuwa akiwafundisha wazazi kusema ukweli hata katika malezi ya watoto wao wadogo. Katika Hadithi iliyotolewa na Imam Ahmad ya kuwa huyu bawana Abdillahi bni Amir kasema: “Sikumoja nilipokuwa bado mdogo alinita mama yangu na Mtume (S.A.W) alikuwepo akishuhudia. Mama yangu akaniambia njoo nikupe kitu. Mtume (S.A.W) akamuuliza mama yangu. Ulitaka kumpa nini? Mama yangu akajibu: nilitaka kumpa tende. Basi hapo Mtume (S.A.W) akamwambia: Ama lau kaja na hukumpa kitu basi ungeliandikiwa kuwa umesema uwongo.”

Kwa hivyo hata mtoto mdogo asizoweshwe hadithi za uwongo na udanganyifu. Bali azoweshwe mambo mema na kusema ukweli.

Na uwongo uko wa ina nyingi kila mmoja ana njia yake ya kudanganya watu. Na zote ni haramu, haifai kusema uwongo katika hali yoyote ile. Japo kuwa ruhusa ipo ikiwa kuwasuluhisha watu waliogombana ili mapenzi yao yarudi. Na vile vile katika kuulinda Uislamu ikiwa kuna vita baina ya Waislamu na makafiri, basi hujuzu uwongo kama kutumia hila mbele ya maaduwi.

Lakini kukaa vikaoni ukawachekesha watu kwa uwongo. Hayo ni haramu. Mtume (S.A.W) kasema katika Hadithi iliyotolewa na Imam Ahmad:

 ( áóÇ íõÄúãöäõ ÇáúÚóÈúÏõ ÇáúÅöíãóÇäó ßõáøóåõ ÍóÊøóì íóÊúÑõßó ÇáúßóÐöÈó Ýöí ÇáúãõÒóÇÍö æóÇáúãöÑóÇÁó æóÅöäú ßóÇäó ÕóÇÏöÞðÇ )

 Maana yake: “Hatokuwa na Imani kamili mja mpaka awache uwongo katika maskhara na awache kujadiliana hata katika ukweli.

Sifa hizo mbili hazimpendezi Muislamu, anatakiwa aziwache na kujepusha nazo katika maisha yake. Ndugu zangu Waislamu tuchukuwe mifano mizuri katika wale waliotangulia ambao wamesifika na kila sifa njema. Mpaka wakawa wakutajwa katika Qura’an. Huyu Sayyidna Abu bakar Radhi ya Mwenyezi Mungu zimfikie. Akisifika na sifa ya ukweli mpaka akaitwa (Sidiyq) yaani ni Mkweli.

Mara moja Bwana huyu na Mtume (S.A.W) walipokuwa wakikimbia kutoka Makkah na kuelekea Madina. Wakati ambo Makafiri wa Kikureshi wanamtafuta Mtume (S.A.W) wamuuwe. Bali walitoa ngamia mia moja atakaekuja na kichwa cha Bwana Mtume (S.A.W) lakini Mola alimlinda. Wakati wapo njiani wanakwenda, aliwatokea mtu fulani ambaye anamjua Abu Bakar lakini hamjui Mtume. Yule mtu akamuuliza Abu Bakar, nani huyu unayefuatana naye? Hapa Sayidina Abu Bakar akisema kuwa huyu ni Muhammad, huwenda yakawa matatizo. Lakini kwa hekima akasema: “Huyu ni muongozi ananiongoza njia.” Yule bwana kafahamu kuwa ni nji ya Madina. Lakini Abu Bakar anakusudia njia iliyonyooka ya kwenda Peponi. Nayo ndio kazi ya Mtume (S.A.W). Hivi ndivyo Waislamu khalisi walivyokuwa wakiishi katika maisha yao, amani na usalama ukawepo na Mwenyezi Mungu akawafungulia milango ya kila kheri.

Ewe Mwenyezi Mungu zitoharishe ndime zute na kusema uwongo (Amin).

 

Copyright ©2005  Uislam.net