HATARI YA KULA RIBA

 

Shukurani ni zake Mola Muumba, Mfalme anayesifika kwa kila sifa za ukamilifu, aliyetakasika na kila sifa za upungufu, Mmiliki na mwenye uwezo wa kila kitu, na ambaye akikiambia kitu kuwa kinakuwa. Kisha rehma na amani zimshukie Mbashiri Muonyaji, Mhitimishi wa Manabii na Mitume, pamoja aali zake, na sahaba zake, na waliowafuatia kwa wema hadi Siku ya Malipo.

Mwenyezi Mungu (SWT) anatwambia katika suratul-Baqarah aya ya pili :

(Ðóáößó ÇáúßöÊóÇÈõ áÇó ÑóíúÈó Ýöíåö åõÏðì áøöáúãõÊøóÞöíäó) 

“Hiki ni Kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uwongofu kwa wamchao Mwenyezi Mungu” (Albaqara, aya-2) 

Ndani ya Qur’an upo uwongofu ulio kamilika kwa walioamini, wakawa tayari kuitafuta kweli, na wakajikinga na adhabu ya Mwenyezi Mungu Duniani na Akhera.

 Ndugu muislamu:

Ukitaka kujua kama wewe kweli unakiamini Kitabu cha Mwenyezi Mungu, basi naomba ujiulize nafsi yako: Qur’ani imetuamrisha tufanye kadha na kadha na imetukataza kufanya kadha na kadha.  Je mimi nayafuata hayo kwa ukamilifu? au nafuata baadhi yake na mengine nayadharau au najiletea hoja mbali mbali?       

AFA LA RIBA

Miongoni mwa maafa makubwa ambayo yamewafika wengi katika waisilamu mpaka wamekuwa hawana raha katika maisha yao ni kosa la Riba¹ - deni (lililo-laaniwa), nalo ni katika Madhambi Makubwa (Kabair).                                            

  ►NINI MADHAMBI MAKUBWA (KABAIR)?

Dhambi kubwa ni kosa lolote ambalo kama mwenye kulifanya hakuliacha na kutubia hutosha kuwa sababu ya yeye kunyimwa neema ya kuingia Peponi na badala yake kuadhibiwa Motoni.

Mwenyezi Mungu ametupa dhamana katika kitabu chake kitakatifu kuwa mtu atakae jiepusha na madhambi makubwa basi atamfutia madhambi madogo (Saghair) na atamuingiza Peponi. Dalili ya hilo ni kauli yake Subhaanahu:

(Åöä ÊóÌúÊóäöÈõæÇú ßóÈóÂÆöÑó ãóÇ Êõäúåóæúäó Úóäúåõ äõßóÝøöÑú Úóäßõãú ÓóíøöÆóÇÊößõãú æóäõÏúÎöáúßõã ãøõÏúÎóáÇð ßóÑöíãÇð)

“Mkiyaepuka makubwa mnayo katazwa, tutakufutieni makosa yenu madogo, na tutakuingizeni mahali patukufu” (An-nisaa, aya - 31)

Aya imetuwekea sharti moja kwa mambo mawili: (1) kufutiwa makosa madogo na (2) kuingizwa mahali patukufu. Sharti moja lenyewe ni kuepuka makubwa tunayokatazwa. Na mahali patukufu si pengine ila ni Peponi.

RIBA NI DHAMBI KUBWA; YAINGIZA MOTONI

Katika Qur’ani Mola amesema :

( ÇáøóÐöíäó íóÃúßõáõæäó ÇáÑøöÈóÇ áÇó íóÞõæãõæäó ÅöáÇøó ßóãóÇ íóÞõæãõ ÇáøóÐöí íóÊóÎóÈøóØõåõ ÇáÔøóíúØóÇäõ ãöäó ÇáúãóÓøö Ðóáößó ÈöÃóäøóåõãú ÞóÇáõæÇú ÅöäøóãóÇ ÇáúÈóíúÚõ ãöËúáõ ÇáÑøöÈóÇ æóÃóÍóáøó Çááøåõ ÇáúÈóíúÚó æóÍóÑøóãó ÇáÑøöÈóÇ Ýóãóä ÌóÇÁåõ ãóæúÚöÙóÉñ ãøöä ÑøóÈøöåö ÝóÇäÊóåóìó Ýóáóåõ ãóÇ ÓóáóÝó æóÃóãúÑõåõ Åöáóì Çááøåö æóãóäú ÚóÇÏó ÝóÃõæúáóÜÆößó ÃóÕúÍóÇÈõ ÇáäøóÇÑö åõãú ÝöíåóÇ ÎóÇáöÏõæäó)

Wale wanaokula riba hawasimami ila kama anavyosimama aliye pandwa na Shet'ani kwa wazimu.  Hayo ni kwa kuwa wamesema: ‘Biashara ni kama riba tu’, wakati Mwenyezi Mungu ameihalalisha biashara na kaiharamisha riba. Hivyo aliyefikiwa na mawaidha kutoka kwa Mola wake akaacha [kula riba], basi ni chake kilichotangulia, na hukumu yake iko kwa Mwenyezi Mungu. Ama wenye kurudia basi hao ndio watu wa Motoni, humo watadumu (Albaqara, aya-275)

Wenye ilmu wanasema aya inatupa taswira ya wanaokula riba watapokuwa wanatoka makaburini mwao siku ya kiyama ya kwamba watakuwa wakitapatapa, wanasimama wakianguka kama mtu aliyeingiwa na shetani.

MLA RIBA HAWI MUUMINI :

Mwenyezi Mungu amebainisha kuwa kula riba na imani hayakubaliani:

(íóÇ ÃóíøõåóÇ ÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇú ÇÊøóÞõæÇú Çááøåó æóÐóÑõæÇú ãóÇ ÈóÞöíó ãöäó ÇáÑøöÈóÇ Åöä ßõäÊõã ãøõÄúãöäöíäó)

”Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na acheni kilichobaki katika riba, ikiwa nyinyi ni Waumini” (Albaqara, aya-278)

Kwa hivyo ikiwa sisi ni waumini kweli basi tumche¹ Mwenyezi Mungu na tuache riba.

SIYEACHA RIBA KATANGAZIWA VITA NA MWENYEZI MUNGU :

Mwenyezi Mungu amesema baada ya aya iliyotangulia:

 

.( ÝóÅöä áøóãú ÊóÝúÚóáõæÇú ÝóÃúÐóäõæÇú ÈöÍóÑúÈò ãøöäó Çááøåö æóÑóÓõæáöåö æóÅöä ÊõÈúÊõãú Ýóáóßõãú ÑõÄõæÓõ ÃóãúæóÇáößõãú áÇó ÊóÙúáöãõæäó æóáÇó ÊõÙúáóãõæäó)

“Na kama hamtafanya [hivyo], basi jueni kwamba mtakuwa na vita na Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mkitubu, basi haki yenu ni rasilmali zenu. Msidhulumu wala msidhulumiwe” (Albaqara, aya-279)

Vita vya Mwenyezi Mungu si vya risasi au mabomu, lakini vita vya Mwenyezi Mungu hapana mtu ambaye anaweza kuvikimbia.  Miongoni mwa vita vya Mwenyezi Mungu ni kupatwa na maafa mengi kama vile dhiki au mtu kutokuwa na raha katika maisha yake hata akiwa na mali nyingi. Kwani Mwenyezi Mungu huondoa baraka katika mali ya riba::

 (íóãúÍóÞõ Çááøåõ ÇáúÑøöÈóÇ æóíõÑúÈöí ÇáÕøóÏóÞóÇÊö æóÇááøåõ áÇó íõÍöÈøõ ßõáøó ßóÝøóÇÑò ÃóËöíãò)...

Mwenyezi Mungu huifutia baraka [mali ya] riba, na huzibariki [mali zinazotolewa] sadaka. Na Mwenyezi Mungu hampendi kila mwenye kukana [amri Zake], mtenda dhambi” (Albaqara, aya-276)

 Huwenda ukamuona mtu masikini lakini akawa yumo katika furaha kuliko huyo anayekula riba. Sababu ya huyu kuwemo katika furaha ni ahadi ya Mwenyezi Mungu aliyoahidi ya kuwa Mu’umini yeyote atakaetenda mema (mke au mume) basi atamhuisha maisha mazuri na atamlipa malipo mazuri akhera:

(ãóäú Úóãöáó ÕóÇáöÍÇð ãøöä ÐóßóÑò Ãóæú ÃõäËóì æóåõæó ãõÄúãöäñ ÝóáóäõÍúíöíóäøóåõ ÍóíóÇÉð ØóíøöÈóÉð æóáóäóÌúÒöíóäøóåõãú ÃóÌúÑóåõã ÈöÃóÍúÓóäö ãóÇ ßóÇäõæÇú íóÚúãóáõæäó)

“Mwenye kutenda mema, mwanamume au mwanamke, naye akawa ni Muumini, tutamhuisha maisha mema; na tutawapa ujira wao kwa bora ya waliyo kuwa wakiyatenda (An Nah’l, aya-97)

 

Lakini atakae pinga amri za Mwenyezi Mungu basi atakuwa na dhiki hapa duniani na siku ya kiyama atafufuliwa kipofu:

 

 (æóãóäú ÃóÚúÑóÖó Úóä ÐößúÑöí ÝóÅöäøó áóåõ ãóÚöíÔóÉð ÖóäßÇð æóäóÍúÔõÑõå íóæúãó ÇáúÞöíóÇãóÉöÃóÚúãóì)

Na atakayeacha kufuata mawaidha yangu, basi kwa yakini atakuwa na maisha ya dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa kipofu” (Ta’ha, aya-124).

 

Bila ya shaka hapana mtu aliye tayari kufufuliwa kipofu, kisha aingizwe motoni.  Kwa hivyo hapana budi ila tuyapokee mawaidha ya Mola wetu.              

►Na katika hadithi za mtume Muhammad (SAW): 

 (áóÚóäó Çááøóåõ Âßöáó ÇáÑøöÈóÇ þ þæóãõæßöáóåõ æóÔóÇåöÏóíúåö æóßóÇÊöÈóåõ ÞóÇáó æóÞóÇáó ãóÇ ÙóåóÑó Ýöí Þóæúãò ÇáÑøöÈóÇ æóÇáÒøöäóÇ ÅöáøóÇ ÃóÍóáøõæÇ ÈöÃóäúÝõÓöåöãú ÚöÞóÇÈó Çááøóåö ÚóÒøó æóÌóáø)ó   

“Mwenyezi Mungu amemlani mwenye kula riba (mwenye kuchukua ziada juu ya deni), na mwenye kuitoa iliwe (k.v. anayekopa akalipishwa zaidi ya alichokopa), na mashahidi wake wawili na mwenye kuiandika (mkataba wake), na akasema (SAW) haitaenea riba na zina kwa watu isipokuwa watajisababishia kushukiwa na adhabu ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka”.

 

Na kutoka kwa Jabir bin Abdullahi (Radhi za Mola zimfikie) amesema:-   

(áóÚóäó ÑÓæá Çááøóåáì Çááå Úáíå æÓáã) Âßöáó ÇáÑøöÈóÇ þþæóãõæßöáóåõ æóÔóÇåöÏóíúåö æóßóÇÊöÈóåõ, óÞóÇáó"åã ÓæÇÁ").

Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amemlani¹ mwenye kula riba, na mwenye kuitoa iliwe, na mashahidi wake wawili na mwenye kuiandika (mkataba wake), na akasema: “hao wote ni sawa” yaani katika dhambi.

 

 Na Abu Bakar (Radhi za Mola zimfikie) amesema:

(ÇáÒÇÆÏ æÇáãÓÊÒíÏ Ýí ÇáäÇÑ )

“Muengezaji na mwenye kuengezewa wote motoni.”  Makusudio yake kuwa mwenye kukopesha (kwa faida) na mwenye kukopeshwa (akalipa kwa faida) basi wote ni sawasawa na malipo yao ni kuingizwa motoni

Kuna watu wanasema hii ni sharia ya nchi, sisi hatuna budi kuifuata; wenye kuchukua jukumu hilo ni wakubwa wa nchi (serikali) walioweka sharia hii.  Na wengine husema huwezi kuishi bila ya mkopo wa Benki n.k.  Ewe ndugu yangu hebu turudiye katika Qur’an ili tuone onyo la Mwenyezi Mungu:

 

(íóæúãó ÊõÞóáøóÈõ æõÌõæåõåõãú Ýöí ÇáäøóÇÑö íóÞõæáõæäó íóÇ áóíúÊóäóÇ ÃóØóÚúäóÇ Çááøóåó æóÃóØóÚúäóÇ ÇáÑøóÓõæáÇ)

Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungali mt'ii Mwenyezi Mungu, na tungali mt'ii Mtume!”(Al-Ahzaab, aya-66).

(æóÞóÇáõæÇ ÑóÈøóäóÇ ÅöäøóÇ ÃóØóÚúäóÇ ÓóÇÏóÊóäóÇ æóßõÈóÑóÇÁäóÇ ÝóÃóÖóáøõæäóÇ ÇáÓøóÈöíáÇ)

Na watasema: Mola wetu! Hakika sisi tuliwat'ii bwana zetu na wakubwa wetu; nao ndio walio tupoteza njia” (Al-Ahzaab, aya-67).

(ÑóÈøóäóÇ ÂÊöåöãú ÖöÚúÝóíúäö ãöäó ÇáúÚóÐóÇÈö æóÇáúÚóäúåõãú áóÚúäÇð ßóÈöíÑÇð).  

Mola wetu! Wape wao adhabu mara mbili, na uwalaani laana kubwa” (Al-ahzaab, aya-68).

Siku hiyo udhuru huo na dua hizo hazitatusaidia kitu, na Mwenyezi Mungu atatwambia:

(Èóáóì ÞóÏú ÌóÇÁÊúßó ÂíóÇÊöí ÝóßóÐøóÈúÊó ÈöåóÇ æóÇÓúÊóßúÈóÑúÊó æóßõäÊó ãöäó ÇáúßóÇÝöÑöíäó).

"Bali ndio! Bila ya shaka zilikujia aya zangu, nawe ukazikadhibisha, na ukajivuna, na ukawa miongoni mwa makafiri!” (Azzumar, aya-59)....

►Nasiha: Ndugu yangu Muislamu kama umejizamisha katika riba basi rudi kwa mola wako na tubia haraka kabla wakati haujapita, kwani Mwenyezi Mungu anasema: 

(æóÇáøóÐöíäó ÅöÐóÇ ÝóÚóáõæÇú ÝóÇÍöÔóÉð Ãóæú ÙóáóãõæÇú ÃóäúÝõÓóåõãú ÐóßóÑõæÇú Çááøåó ÝóÇÓúÊóÛúÝóÑõæÇú áöÐõäõæÈöåöãú æóãóä íóÛúÝöÑõ ÇáÐøõäõæÈó ÅöáÇøó Çááøåõ æóáóãú íõÕöÑøõæÇú Úóáóì ãóÇ ÝóÚóáõæÇú æóåõãú íóÚúáóãõæä)

Na ambao pindi wafanyapo uchafu [kwa kutenda dhambi kubwa] au wakajidhulumu nafsi zao [kwa dhambi ndogo] humkumbuka Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha kwa dhambi zao - na nani anaye futa dhambi isipokuwa Mwenyezi Mungu? - na wala hawaendelei na waliyo yafanya na hali wanajua” (Al-Imran, aya-135).

(ÃõæúáóÜÆößó ÌóÒóÂÄõåõã ãøóÛúÝöÑóÉñ ãøöä ÑøóÈøöåöãú æóÌóäøóÇÊñ ÊóÌúÑöí ãöä ÊóÍúÊöåóÇ ÇáÃóäúåóÇÑõ ÎóÇáöÏöíäó ÝöíåóÇ æóäöÚúãó ÃóÌúÑõ ÇáúÚóÇãöáöíäó)

       “Hao   malipo yao ni msamaha kwa Mola wao, na Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo, na ni mwema ulioje ujira wa watendao [mema]” (Al-Imran, aya-136).

►UTANABAHISHO MUHIMU: Elewa ndugu muislamu kuwa faida itolewayo na benki ya riba kwa rasilimali ya mteja ni riba. Hii ni kwasababu rasilimali za wateja huingia katika mikopo ya riba itolewayo na benki hio na riba ya mikopo hio hugawiwa kwa wateja.

►UKUMBUSHO: Kumbuka kuwa kitu chochote cha halali kina tabu kukipata na kinataka subira na jitihada, lakini jambo la haramu ni wepesi na rahisi sana kulipata.  Hii yote ni mitihani ya Mwenyezi Mungu kwetu sisi waja wake ili wapate kujulikana nani ni wacha Mungu (wenye kumuamini, kumtii na kumuogopa).  Mwenyezi Mungu amewaahidi wale wamchao kuwa atawafungulia njia na atawaletea riziki kwa namna ambayo hawakuitarajia:

 (æóãóä íóÊøóÞö Çááøóåó íóÌúÚóá áøóåõ ãóÎúÑóÌÇð. æóíóÑúÒõÞúåõ ãöäú ÍóíúËõ áÇ íóÍúÊóÓöÈõ æóãóä íóÊóæóßøóáú Úóáóì Çááøóåö Ýóåõæó ÍóÓúÈõå)

.              ....................................  “Na mwenye kumcha Mwenyezi Mungu [akashika amri zake na akaepuka makatazo yake] atamjaalia njia ya kutokana na kila dhiki. Na atamtengezea sababu za kupata riziki kwa pande ambazo hata hazimpitikii katika fikra zake. Na mwenye kumwachia mambo yake yote Mwenyezi Mungu basi Yeye ni Mwenye kumtosha, [hana haja ya mwengine]” (Al-talaaq, aya-2&3).

Pia kasema:( æóãóä íóÊøóÞö Çááøóåó íóÌúÚóá áøóåõ ãöäú ÃóãúÑöåö íõÓúÑÇð)     

“Na mwenye kumcha Mwenyezi Mungu, [akatimiza hukumu zake] Mwenyezi Mungu atayawepesisha mambo yake” (Al-talaaq, aya-4).

    Na amewaahidi wacha Mungu kuwafutia madhambi yao na kuwalipa ujira mkubwa akhera:

(æóãóä íóÊøóÞö Çááøóåó íõßóÝøöÑú Úóäúåõ ÓóíøöÆóÇÊöåö æóíõÚúÙöãú áóåõ ÃóÌúÑÇð)

“Na mwenye kumcha Mwenyezi Mungu [akahifadhi hukumu zake] humfutia makosa yake, na atampa ujira mkubwa” (Al-talaaq, aya-5).

Suala:-

             Nifanyeje ili na mimi nimiliki halali?

Jawabu:-

               Dunduliza (changa) pesa zako au shirikiana na ndugu zako wa Kiisilamu mufanye upatu ili lengo lenu liwe la kusaidiana, na Mwenyezi Mungu atakuwafikisheni kwa fadhila zake, kwa sababu mutakuwa miongoni mwa wale walio mcha Inshaallah.

 

Mwisho, namalizia kwa shairi la (Imam Shaafi):                     

Ewe binaadamu Ulizaliwa na mama yako  na huku unalia  na  watu wamekuzungukia wamefurahi wanacheka.

Basi ifanyie nafsi yako ili wakikulilia  Siku ya mauti yako  unacheka na umefurahi.

 

  Çááåã ÃÍííäÇ Úáì ÇáÅÓáÇã æÃãÊäÇ Úáíå ¡ Çááåã æÇÑÒÞäÇ ÚãáÇð ÕÇáÍÇð ãÊÞÈáÇð ¡ æÇáÊæÈÉ ÞÈá ÇáãæÊ ¡ æÇáÔåÇÏÉ ÚäÏ ÇáãæÊ ¡æÇáÚÝæÉ æÇáÊíÓíÑÚäÏ ÇáÍÓÇÈ ¡ æãÑÇÝÞÉ ÇáÃäÈíÇÁ æÇáÕÇáÍíä Ýí ÇáÌäÇä íÇ ÃÑÍã ÇáÑÇÍãíä ¡æÕáì Çááå æÓáã Úáì äÈíäÇ ãÍãÏ æÚáì Âáå æÕÍÈå ÃÌãÚíä

 

Ndugu yenu: Masoud Al Gheithy.

 

Copyright ©2004  Uislam.net