|
Mwenye kutaka kuhiji anatakiwa afanye mambo
kadha kabla kuingia safarini, nayo ni:
1.
Kumtakasia nia Allah
aliyetukuka na kutakasika; kwani Allah hapokei ila kilichokuwa kwa ajili
yake pekee.
)
وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا
اللَّهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاء وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا
الزَّكَاةَ وَذَلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ(
{Wala hawakuamrishwa ila
kumuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia dini, waache dini za upotofu, na
wasimamishe sala na kutoa zaka, na hiyo ndiyo dini iliyo sawa} [Albayyinah,
5]
)
أَلَا لِلَّهِ الدِّينُ الْخَالِصُ(
{Mwenyezi Mungu ndiye wa
kutakasiwa dini bila kushirikishwa} [Az-zumar, 3]
2.
Toba ya kweli kutokana na kila
kosa alilofanya ili aje kwa Mola wake akiwa msafi wa moyo.
3.
Awaachie wanaomlazimu matumizi ya
lazima hadi kurudi kwake. Mtume - rehema za Allah na amani zimshukie -
anasema: “Ni kosa la kumtosha mtu
kuwatupa waliomlazimu.” Ameipokea Bukhari.
4.
Ajichukulie mahitaji ya safari ya
kutosheleza ili abaki katika tabia ya kupendeza. Kutoka kwa Ibnu Abbas –
Allah awaridhie – amesema: Watu wa
Yemen
walikuwa wakihiji na hawachukui mahitaji ya safari, na wakisema: Sisi ndio
tunaomtegemea Allah. Wakifika Maka huwaomba watu. Allah Mtukufu akateremsha
kauli Yake: “Na jichukulieni mahitaji ya safari, kwani mahitaji bora ya
safari ni ucha-Mungu.” Ameipokea Bukhari na Abu
Daud.
5.
Alipe madeni yake, arudishe alivyoazima
na amana za watu, na atokane na kila jukumu lililo juu yake; kutokana na
kauli ya Mtume - rehema za Allah na amani zimshukie:
“Nafsi ya Muumini (aliyekufa) imewekwa rehani”
– na katika riwaya moja “imetundikwa -
kwa deni
lake mpaka alipiwe.” Ameipokea Tirmidhi
akaihasanisha na Ibnu Majah.
6.
Aandike wasia wake na haki
zilizomlazimu. Mtume - rehema za Allah na amani zimshukie anasema:
“Si halali kwa mtu Muislamu aliye na kitu cha
kuusia kulala siku mbili ila na wasia wake umeandikwa, uko kichwani kwake.”
Ameipokea Rabiu, Bukhari na Muslim.
7.
Awatake radhi watu wa nyumbani
kwake, jamaa zake, jirani zake na wenzake, na awaage anapoondoka.
8.
Ajifunze vipi kuhiji; kwani
ibada haisihi kwa asiyeijua. Akichukua kitabu kilichokusanya yanayohusu hija
ni bora.
9.
Afuatane na watu wema
watakaomsaidia kutekeleza ibada za hija.
10. Ajitahidi matumizi yake yawe ya
halali yasiyo na shaka.
11. Inapendelewa safari yake iwe siku ya Alkhamisi;
kwani imekuja kwenye Sahihi Mbili kutoka kwa Kaab bin Malik - Allah amridhie
– amesema:
“Mara chache Mtume - rehema za Allah na amani zimshukie –
aliingia safarini siku isiyokuwa Alkhamisi; ikiwa imempita basi ni siku ya
Jumatatu; maana ndiyo siku aliyohama Mtume wa Allah - rehema za Allah na
amani zimshukie – kutoka Maka.”
12. Wamempendelea baadhi ya
wanazuoni anaposafiri aiage nyumba yake kwa rakaa mbili na aombe dua ya
safari.
|