KUIPOKEA
RAMADHAN
Hakika hamna kosa
katika anuani hii,kwani watu wanagawanyika katika makundi mengi katika
kuuaga mwezi mtukufu wa ramadhani kwa walivyo chukulia umuhimu wa mwezi wa
ramadhani juu yao:
1)
Kundi la mwanzo wana uaga mwezi huu mtukufu kwa moyo ulio na huzuni na
nafsi yenye kuogopa. Watu hawa wana mategemeo kuwa huenda ALLAH
atawakubalia amali zao zote nzuri walizo zifanya katika mwezi huu.
2)
Kundi la pili wanamajuto kwa muda walio upoteza katika mwezi huu bila ya
kuutumia katika kufanya ibada na kufanya kheri kama vile wao walivyokuwa
wakitegemea.
3)
Kundi la tatu ni kundi la watu waliofurahi kwa kumalizika mwezi wa
ramadhani, ili warudi katika matamanio ya nafsi zao na maasi waliokuwa
wamezuilika kuyafanya katika mwezi wa ramadhani.
4)
Kundi la nne ni kundi ambalo kuingia kwa ramadhani au kwisha kwake ni kama
mchezo kwao hawajali na wala hawalindi mipaka ya ALLAH katika mwezi huo
hawafuati walioamrishwa wala hawa achi waliokatazwa.
JE
WEWE UKO KATIKA KUNDI GANI UKIJIPIMA NA RAMADHANI YA MIAKA ILIYOPITA?
NA JE UNACHAGUA UWE KATIKA
KUNDI GANI KATIKA RAMADHANI INAYOKUJA?
Ndugu waislamu, suala
la kujiuliza ni:
JE, SISI TUNAUJUA KWA UHAKIKA HUU
MWEZI WA RAMADHANI NI NINI NA KWA NINI TUNA UFUNGA?
Watu
wengi hawajafahamu makusudio ya mwezi huu wa ramadhani ni nini. Watu wengi
wame ubebesha mwezi huu mambo ambayo umeshindwa kuyabeba. Waka upa uhai
usiku wake kwa mambo ambayo hayamridhishi Mola na wakaupa uhai mchana wake
kwa mambo ambayo hayatakikani kuyafanya, na huku ALLAH anasema katika
kitabu chake kitukufu Qur'aan katika Surat Al-Baqara (aya#183 mpaka 185):
*
قال الله تعالى:
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ
عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ
لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ*
أَيَّامً
مَّعْدُودَاتٍ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ
عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ وَعَلَى الَّذِينَ
يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ
فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ
وَأَن تَصُومُواْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ
تَعْلَمُونَ
*
شَهْرُ رَمَضَانَ
الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى
لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ
فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ
عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللّهُ بِكُمُ
الْيُسْرَ وَلاَ يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ
وَلِتُكْمِلُواْ الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُواْ
اللّهَ عَلَى مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
.
Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Saumu,
kama waliyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kuchamngu (183).
Mfunge siku maalumu za kuhisabika. Na atakaye kuwa miongoni mwenu mgonjwa
au yumo safarini basi atimize hisabu katika siku nyengine. Na wale wasio
weza, watoe fidiya kwa kumlisha masikini. Na atakaye fanya wema kwa
kujitolea, basi ni bora kwake. Na mkifunga ni bora kwenu, kama mnajua
(184). Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa ni uwongofu
kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi.
Basi ataye kuwa mjini katika mwezi huu
naafunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika
siku nyengine. Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni
yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa
kuwa amekuongoeni ili mpate kushukuru (185).
Ndugu zangu waislamu: Mwezi wa ramadhani ni nguzo ya nne
katika nguzo za uislam, na ni jambo la kumuabudu Mola. Mwenyezi Mungu
akatufanyia mwezi huu kuwa ni faridha juu yetu, anasema Mtume (SAW):
{بني
الإسلام على خمس: وصوم رمضان}
Saumu inatufundisha
kumuogopa Mola na kuwa na ikhlas katika kufanya amali (ibada) kwa ajili
saumu ni siri baina ya mja na Mola wake:
{الصيام لي و أنا
أجزي به – حديث قدسي شريف}
Saumu ni kinga
inayotukinga tusifanye maasi na inatengeneza tabia zetu na inalinda nafsi
zetu na matamanio:
{الصيام
جُنة فإذا كان يوم صيام أحدكم فلا يفسق و لا يرفث، و إن سابّه أحد أو شاتمه
فليقل إني امرؤ صائم – حديث شريف}
Saumu
ni afya ya mwili na pia inaipa mwili nguvu:
{صوموا
تصحوا – حديث شريف}
Saumu
ni mapumziko ya mwaka mzima ya tumbo, kwani tumbo ni mfanyakazi anaeipenda
kazi yake katika mwaka mzima. Basi ni haki ya huyu mfanyakazi maskini
apate mapumziko angalau mchana wa mwezi mmoja katika mwaka. Basi ni juu
yetu tupunguze kula ili tulipumzishe hili tumbo na machofu ya kazi nzito
ya mwaka mzima.
{ما ملأ
ابن آدم وعاء شرّ من بطنه – حديث شريف}
Saumu ni chakula bora cha roho: Kupunguza kwetu kula, kunakupa nafasi
roho (moyo) kupata nguvu na kulainika baada ya kupata chakula cha roho
amabcho ni kufanya ibada tofauti kama vile sala,kufunga,kusali
usiku,kusoma Qur'aan na kutembelea wazazi na arhaam. n.k
Saumu ni rehama na
kuoneana huruma na kukamatana na kuzidisha udugu kwa kuhisi vipi watu
wanaohitajia au waliofukuzwa makwao au wanaokosa chakula mwaka mzima. Vipi
wanaweza kuishi ikiwa sisi tunaokosa chakula mchana wa ramadhani tu tuna
kuwa kama hivi.
Saumu
ni ushindi na kuwa izza ya nafsi na karama ya mtu, kwani katika mwezi huu
waislamu walishinda vita vingi na uislamu ukapata jina katika mwezi huu.
Saumu
inayo faida nyingi nyingine, kutoka kwenye faida ya kimwili na ki
imani (roho) mpaka kufikia faida ya kiafya na kimali na economic.
FAIDA GANI
ZINAPATIKANA KATIKA MWEZI HUU WA RAMADHANI AMBAZO SI RAHISI KUPATIKANA
KATIKA MIEZI MINGINE YA KAWAIDA:
Thawabu
za amali njema katika mwezi huu zinakuwa mara dufu:
{الصيام
لي و أنا أجزي به }
{من صلى فيه نافلة كان
كمن صلى فريضة و من صلى فريضة كان كمن صلى 70 فريضة )
Kutaarishwa roho kiibada na kumtii Mola na kuiweka nafsi tayari kuongeza
juhudi na kufanya ibada kwa wingi.
Usiku wa LAILAT AL-KADR: usiku ambao ni bora kushinda miezi elfu. Na ujira
wa kusali na kuamka usiku na kusoma Qur'aan na dua katika usiku huo
unakuwa ni sawa na ujira wa zaidi ya miaka 83:
{ليلة
القدر خير من ألف شهر}
Umra katika
mwezi huu ni sawa na Hajj
{العمرة في رمضان
تعدل حجة معي – حديث شريف}
Kufunguliwa milango ya
pepo na kufungwa milango ya moto na kufungwa kwa mashetani:
{إذا جاء
رمضان فتحت أبواب الجنان و أغلقت أبواب النيران و صفدت الشياطين – حديث شريف}
Kurahisishwa njia ya toba na kuacha maasi, kama vile kuvuta sigara,kulewa
ulevi na kutumia madawa ya sumu, kupoteza sala, kutizama mambo ambayo
hayafai, kusikiliza nyimbo na michezo ambayo haina maana(karata) n.k
Urahisi wa kuacha baadhi ya tabia mbaya kama vile kulala sana, kula
sana,kutokuwa na bashasha kuchelewa kusali na kupoteza nyakati zake,
kudhereu kazi n.k
kukamatana jamaa na majirani na kuwa kitu kimoja na kukamatana kwa taqwa
na amali njema na wakawa ni wenye kutiana nguvu katika kutekeleza ibada za
mchana na za usiku.
VIPI
TUJITAARISHE KUOPOKEA MWEZI WA RAMADHANI UNAOKUJA NA NINI TUNAWEZA
TUKAFANYA KATIKA MWEZI HUO:
Hakika mtu yeyote akitaka kupasi mtihani ni lazima ajitaarishe kwa makini
juu ya mtihani huo kwa kusoma usiku na mchana. Kwani wanafunzi wengi
wanajitaarisha na mitihani hiyo kwa kusoma na kuhifadhi masomo yao nyakati
za usiku ili wapate kujitaarisha vyema na mtihani huo ndio maana wanapasi
vizuri mwisho wa mwaka. Na tukitaka kuchambua zaidi jambo hili hembu
tutizame timu za mipira vipi zina jitaarisha na mechi zao mpaka inafika
kusafiri nchi mbali mbali ili wajitaarishe vizuri kimwili na kifikra na
mechi hizo na wapate kushinda na kupewa vikombe na kama hawatafanya hivyo
basi watashindwa na kikombe kuchukuliwa na timu nyingine. Ikiwa haya ndiyo
masharti muhimu kwa mwanafunzi au timu ya mpira wayatekeleze ndio
watafuzu kwenye mitihani ya masomo au mechi zao za mipira hapa duniani.
Vipi pepo ya ALLAH je haitaki mataarisho na kukesha usiku na mchana ili
tufaulu na tuingie peponi ambayo upana wake ni baina ya mbingu na ardhi
iliyotaarishwa kwa wenye kumuogopa ALLAH.
Basi ni mashindano gani yanayostahiki kujitaarisha nayo,
mashindano ya kidunia au ya kiakhera. Basi ni bora tuamue lipi ni la
mwanzo kulitenda na nini tufanye ili tupasi katika mwezi huu mtukufu wa
ramadhani unaokuja.
Imethibiti kuwa Mtume (SAW) alikuwa akizidisha kufunga katika mwezi wa
SHAABAN na ikafika hadi masahaba wakawa hawajui lini Mtume(SAW) ameamka
amefunga na lini ameamka hajafunga kwa kuthirisha kwake kufunga katika
mwezi huu wa Shaaban. Na Mtume (SAW) alikuwa akizidisha kutembelea arhaam
zake na kutoa sadaka na kufanya kila aina ya mambo mema. Alikuwa akifanya
yote haya kwa kujitaarisha na mwezi mtukufu wa ramadhani, ili iwe ni
rahisi kwake kufanya haya mambo unapoingia mwezi mtukufu wa ramadhani.
{ولكم في
رسول الله أسوة حسنة – القرآن الكريم}
Ndugu zangu waislamu:
Hizi ni baadhi ya fikra kwa uwezo wa ALLAH zitatuwezesha kuufunga mwezi wa
ramadhani unaokuja kwa ukamilifu. Anza kujizowesha kufanya mambo haya na
itaarishe nafsi yako kuyafanya kuanzia mwezi huu wa Shaaban:
*
Weka azima kuwa mwezi wa ramadhani unaokuja uwe ndio mwezi bora
utakaofunga kushinda miezi yote ya ramadhani iliyopita maishani mwako.
* Weka plan
yenye uhakika itakayo kufanyisha uweze kufaulu katika mwezi huu. Mfano,
andika baadhi ya vitu vya kheri ambavyo utaweza kuvifanya katika mwezi huu.
Ujuwe ikiwa huweki plan ya kufaulu basi unaweka plan ya kutofaulu.
* Jizoweshe
kufunga nafila anza kujizowesha kufunga baadhi ya siku katika mwezi huu wa
Shaaban kama vile nafila ili uizoweshe nafsi yako.
* Jikaribishe
zaidi na Qur'aan: Anza kujizowesha kusoma Qur'aan katika mwezi wa shaaban
na uweke wakati maalumu wa kuhifadhi na kutekeleza amri zake.
* Jizoweshe
kusali sala za usiku katika mwezi huu kwa kusali sala fupi kabla huja lala
au kabla sala ya al-fajiri au ukiweza nusu ya usiku.
* Ongeza
nyakati na rakaa za sala za usiku na usijilazimishe kuamka muda mrefu
usiku ili usichoke na kumbuka kuwa wewe unapata ujira kwa haya
unayoyafanya.
* Tembelea
wazee wako na arhaam zako katika mwezi huu wa shaaban.
* Jizoweshe
kutoa ulichokuwa nacho na kutoa sadaka. Na weka baadhi ya mali ili utoe
sadaka katika mwezi wa ramadhani na kumbuka jamaa zako wa karibu ndio bora
kuwafanyia umaarufu (wema)
{و ما
تنفقوا من خير فلأنفسكم، و ما تنفقون إلا ابتغاء وجه الله، و ما تنفقوا من
خير يوف إليكم و أنتم لا تظلمون - البقرة}
{ما نقص
مال من صدقة – حديث شريف}.
*
Futarisha watu waliofunga: Jitahidi ualike mtu aliyefunga nyumbani kwako.
{من فطّر مسلما كان
له أجر صيامه من غير أن ينقص من أجره شيئا}
-
Chagua nani utamualika na weka siku ya
kumualika.
-
Unaweza kualika watu wako wa karibu au jirani zako au waislamu wenzako au
wanafunzi wageni wanaoishi mtaani kwako.
-
Unaweza kualika ndugu zako waislamu wageni katika nchi yako ili
uwapunguzie unyonge wa kuwa mbali na familia zao na wapate kujuwa umoja wa
waislamu na udugu wao.
-
Pia unaweza kuwaalika wasiokuwa waislamu ili wajuwe vipi waislamu
wanafunga na kwa nini waislamu wanafunga huwenda wakapata imani na
wakaingia ndani ya dini kwa walio yaona, ukawa wewe ni sababu ya wao
kuingia katika uislamu:
{لأن يهدي
الله بك رجلا خير لك من الدنيا و ما فيها}.
*Linda
wakati wako: Jaribu kulinda wakati wako katika mwezi wa ramadhani
usipoteze hata sekunde katika mwezi huu isipokuwa kwa kufanya ibada na
kumtaja Mola (Tasbih au tahlil)
* Mwezi wa
Qur'aan: kwa ajili mwezi wa ramadhani ni mwezi ulioshushwa ndani yake
Qur'aan basi ni juu yako kila wakati ujitahidi kusoma Qur'aan:
- Weka
wakati maalumu wa kuhifadhi Qur'aan.
- Weka
wakati wa kufahamu maana ya aya za Qur'aan na kutekeleza maamrisho yake na
kuwacha makatazo yake.
-
Weka wakati wa kujifundisha kusoma Qur'aan kwa Tajwid na kuisoma sawa bila
ya makosa.
- Weka
wakati uwasomeshe wasiojuwa kusoma Qur'aan.
-
Nunuwa Tafsiri ya Qur'aan kwa lugha yeyote ile na mpe muislamu asiyefahamu
kiarabu
{بلغوا عني و لو آية
– حديث شريف}
- Jiunge katika vikundi vya
watu wanaosoma Qur'aan kila siku au wiki mara moja
* Toba weka
nia ya kutubu kwa ALLAH kwa kujitahidi kuwacha madhambi uliyokuwa
ukiyafanya kabla kwa kujishughulisha na kufanya mema na kuusemesha moyo
wako.
* Tafuta
rafiki mwema ili akupeleke katika mema na epukana na rafiki wabaya.
* Jaribu
kuzishinda tabia zako mbaya kwa kuzikusanya tabia hizo na kuzitafutia dawa
na kuzibadilisha na tabia nyingine njema. Mfano:
-
Kula kwingi kwa israf na kununua vivazi ambavyo si muhimuàß
kula kiasi na kutofanya israf katika kula na kivazi.
-
Kujizowesha kuishi bila ya kunywa kahawa na vinginevyo ambavyo ni halaliàß
kutosheka na kidogo hata kama ni halali.
-
Kuvuta sigara na maasi mengineàßKutubu
juu ya ALLAH kwa kutorejea kuvuta sigara na kufanya tena hayo maasi.
-
Kulala sana na uvivuàß
Lala mapema ili uamke mapema na kuwa na hima katika maisha yako.
-
Kukesha usiku na kutizama TVàß
Lala mapema na amka usiku ili usali sala za usiku na usome Qur'aan.
-
Kupuuza sala na kukithirisha kuunga salaàß
Jitahidi kusali sala katika nyakati zake na kungojea sala baada ya sala.
-
Kusengenya na kusema uongo na kusema hovyoàß
Kumuogopa ALLAH na kukithirisha kumtaja ALLAH na kutosheka kusema
yanayofaa kusema.
*Kuomba msaada
na kujikinga kwa ALLAH na kutawakul juu yake
والــســلام عـلـيـكـم ورحـمـة اللّه وبـركــاتــ