|

ITIKAFU
Maana ya Itikafu
katika lugha:
Kushikilia kitu.
Maana ya Itikafu katika Sheria:
Ni kukaa msikitini na kubaki humo kwa mkalifiwa kwa namna
maalumu, ili kujikurubisha kwa Allah Mtukufu hali ya kuwa anaepuka
yanayopingana na hilo.
Itikafu
ilikuwapo katika Sheria za Allah zilizotangulia. Kasema Mwenyezi
Mungu katika Suratil Baqarah aya ya 125:
)æóÚóåöÏúäóÇ
Åöáóì ÅöÈúÑóÇåöíãó æóÅöÓúãóÇÚöíáó Ãóäú ØóåøöÑóÇ ÈóíúÊöíó
áöáØøóÇÆöÝöíäó æóÇáúÚóÇßöÝöíäó æóÇáÑøõßøóÚö ÇáÓøõÌõæÏö(
“Na
tulimwusia Ibrahimu na Ismaili kuwa: "Itakaseni nyumba yangu kwa
ajili ya wanao izunguka kwa ku'tufu, na wanaobaki humo kwa ibada, na
wanao rukuu na kusujudu”.
HUKUMU YA ITIKAFU:
Asili ya
itikafu ni kuwa sunna inayopendelewa, hasa katika kumi la mwisho la
Ramadhani kutokana na mafundisho ya Mtume S.A.W, tena ina fadhila
kubwa. Na inawezekana itikafu kuwa wajibu - kama ikiwa ya kutekeleza
nadhiri.
PAHALA PA ITIKAFU:
Inapendelewa iwe katika Msikiti wa Ijumaa, ili isimbidi kutoka kwa
ajili ya sala ya Ijumaa. Ikishindikana hivyo basi iwe katika msikiti
unaosaliwa Sala ya Jamaa. Isipokuwa mwanamke; yeye hukaa itikafu
pale alipopafanya pa kusalia katika nyumba yake. Na inamjuzia kukaa
itikafu msikitini na Mumewe, kwa sharti awe kwenye pahala
palipowekwa kwa ajili ya wanawake.
MASHARTI YA ITIKAFU:
1-
Niya:
Akusudie kwa kukaa itikafu kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu S.W. na
kufuata Sunna ya Mtume S.A.W pamoja na kutaraji thawabu.
2-
Saumu:
Kwani itikafu haisihi bila ya kufunga.
3-
Kubaki
msikitini:
Kwasababu Mtume S.A.W alikuwa akikaa itikafu msikitini na haingii
nyumbani kwake ila kwa haja ya kibinaadamu.
AMALI ZA MWENYE KUKAA ITIKAFU:
Kwa vile mwenye
kukaa itikafu niya yake ni kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, basi
anatakiwa atumie wakati wake kwa kufanya ibada maalumu kama sala,
kusoma Qur’ani, kujifunza elimu zenye manufaa, kumdhukuru Allah na
kuomba dua na maghfira. Na hakuna ubaya kwa aliye katika itikafu
kuzungumza yale ambayo hayana makosa. Kwani imepokewa kwamba Mama
Safia R.A mkewe Mtume S.A.W alimtembelea Mtume S.A.W msikitini akiwa
katika itikafu, akazungumza naye muda, kisha akainuka arudi, Mtume
akamsindikiza mpaka mlangoni mwa msikiti.
WAKATI WA ITIKAFU:
Mwenye kutaka kukaa
itikafu usiku na mchana, basi aingie msikitini kabla ya magharibi
(kabla ya kutua jua), na vile vile kwa mwenye kutaka kukaa itikafu
siku kadha au mwezi. Ama akitaka kukaa itikafu mchana tu, basi
aingie msikitini kabla ya kuchomoza alfajiri, na mwisho wa itikafu
yake ni kutua kwa jua; asitoke kwenye itikafu kabla ya magharibi.
Na mwenye kutaka
kukaa itikafu katika kumi la mwisho la Mwezi wa Ramadhani, ataingia
msikitini kabla ya magharibi ya usiku wa kuamkia tarehe ishirini na
moja, na atatoka baada ya kutua jua la siku ya mwisho ya Mwezi wa
Ramadhani.
Inakatazwa kukaa
itikafu katika siku zilizokatazwa kufunga, kama siku ya idi (siku
kuu) na siku ya Shaka. Kwani katika masharti ya itikafu ni kufunga
kama ilivyotangulia kutajwa.
YANAYOHARIBU ITIKAFU:
1-
Kufanya kitendo cha ndoa (Jimai) hata ikiwa usiku
baada ya futari. Kasema Mwenyezi Mungu katika Suratil Baqarah aya
ya: 187:
)æóáÇ
ÊõÈóÇÔöÑõæåõäøó æóÃóäúÊõãú ÚóÇßöÝõæäó Ýöí ÇáúãóÓóÇÌöÏö(
(Wala msiwaingilie na hali mnakaa itikafu msikitini).
Kujitoa
manii kwa makusudi pia hupewa hukumu hii; kwa hiyo mwenye
kusababisha kutokwa na manii hubatilisha itikafu yake.
2-
Kuharibu Saumu: kwa kula au kunywa, au kufanya maasi
– kwa kauli iliyo sahihi, au mengineyo yanayobalitisha saumu kama
kutia dawa ya macho, kujitapisha kwa makusudi, n.k.
3-
Kutoka msikitini bila dharura: mwenye kufanya hivyo
huharibu itikafu yake; na kuna kauli kwamba arudi na aendelee kisha
alipe kwa kukaa msikitini muda kama aliotoka.
4-
Kutoka bila dharura na kuto kurudi tena.
MASUALA TOFAUTI YANAYOHUSU ITIKAFU:
1-
Mwanamke mwenye kukaa itikafu, akipatwa na hedhi
mchana, basi itikafu ya siku hiyo huharibika, na atatoka msikitini
mpaka akisha tahirika atarudi na kuendeleza itikafu yake.
2-
Mwenye kukaa itikafu akijiwekea sharti ya kufanya
jambo ambalo itikafu hailiruhusu, kama kwenda mazikoni au kulala
nyumbani kwake, basi sharti yake hiyo ni batili kwa kauli ya wengi
wa maulamaa; na kwa hiyo akilifanya itikafu yake huharibika.
3-
Hakuna neno kwa mwenye kukaa itikafu kumtuma mtu
mwengine amtekelezee haja zake na yanayohusu maslahi ya maisha yake.
Vile vile anaweza kufungisha ndoa, kujitia manukato na kujisafisha
mwili.
|