|

KUWATEMBLEA
WAISLAMU
Kwa uwezo wake
Allahu Subhana Wataala, Jumuiya ya Istiqama imeweza kuwafikiwa
Waislamu katika sehemu mbali mbali ili kutaka kujua hali zao na
kuwafikishia ujumbe wa Daawa katika njia ya Allah kwa kuwapelekea
Walimu na Mashekhe, moja katika safari hizo ni hii mnayoiona katika
picha hii. Kuwatembelea kabila moja la Kimasai liloingia katika
uislamu. |
Jumuiya ya Istiqama
huchukuwa juhudi hizi kwa ajili ya kufikisha ujumbe wa Allah katika
kuitangaza Dini yake. Na alhamdulilah faida zinazopatika zinaonekana
na kila mtu, Na kama mnavyojua juhudi hizi husimamishwa na misaada ya
Waislamu.
Kwa hivyo musiwache
kujitolea katika njia za kheri kama hizi, Jiunge na Waislamu wenzako
na Isaidie Jumuiya ya Istiqama katika kutangaza Dini ya Allah na
kuwasaidia Waislamu.
 |
| |
|

KUCHIMBA VISIMA
VYA WAQFU
Vile vile moja
katika juhudi za Jumuiya ya Istiqama ni kuwachimbia Waislamu visima
katika sehemu zinazokuwa na shida ya kupata maji ya kunywa na kutumia.
Alhamdulilah jumuiya
imeweza kuchimba zaidi ya visima 50 vya maji katika sehemu mbali mbali
kama Unguja, Pemba, Bara, Uganda Mali na Ghana. |
Ndugu Muislamu
unaweza kusaidia au kutowa mchango wako katika juhudi hii ya kuchimba
visima vya maji. Na taklifa yake si ghali kuanzia Dola 300 - hadi 2000
hutegemea na sehemu ilivyo. Mara nyengine huwa ni vigumu kuyafikia
maji, lakini alhamdulilah kwa uwezo wake Allah hupatikana.
 |
| |
|

MADRASA ZA
QURAAN
Kuwasomesha watoto
kitabu cha Mwenyezi Mungu Qura'an ni katika jambo la kwanza liloanzwa
na Jumuiya ya Istiqama. Madrasa hizi idadi yake inazidi 150 katika
sehemu mbali mbali za unguja zanzibar na kisiwani Pemba na Bara katika
wiliya zake nyingi na Uganda na Mali na Ghana na Ruwanda na Burundi.
Vile vile Isiqama husaidia kupeleka walimu katika sehemu za mbali ili
kupeleka mbele masomo ya Dini, watoto husomeshwa Quraan na Hadithi na
Fiqhi pamoja na Lugha ya Kiarabu.
|
Mashekhe na Walimu
kutoka Omani hutembele vyuo vya Istiqama na kufuatilia taasisi na
misingi ya kusomesha watoto.
Ndugu Muislamu: Yote
haya yanahitajia misaada yenu katika ujenzi wa vyuo hivyo na
matayarisho yake.

 |
| |
|

KUJENGA
MISIKITI
Kujenga Misikiti ni
moja katika jambo la muhimu nilalotangulizwa na Jumuiya ya Istiqama.
Zaidi ya Misikiti 50 imejengwa na Jumuiya au husaidiwa kifedha katika
kusimamisha msingi wa mwazo, kuanzia unguja zanzibar kisiwani Pemba na
sehemu nyengine tulizozitaja hapo nyuma. |
Ndugu Muislamu:
Wallahi ungelikuwa unajua furaha ya Waislamu wenzako pale wanapoona
Msikiti unajengwa katika kijiji chao basi ungelitamani na wewe mali
yako imeunga mkono pamoja na mali za Waislamu wanaojitolea katika kazi
hii ya kuimarisha Nyumba za Mungu.
 |
| |