|

ISRAFU KATIKA
MWEZI WA RAMADHANI
Assalaamu
'alaykum warahmatullah wabarakaatuh
Wapenzi katika Imaan:
Baada ya kuwaombea kila la
kheri na baraka katika mwezi huu mtukufu uliojaa baraka na thawabu za bure kwa
mwenye kutaka, napenda kutoa mchango wangu katika masaail mbalimbali
yanayohusiana na mwezi huu wenye ukarimu usio na mfano.
Katika neema
kubwa za Allah kwa waja wake ni kutuneemesha neema za kila aina ambazo
hatutaweza kuziihisabu, kati ya neema hizo ni huku kuweza kupta chakula
cha aina tofauti katika maladhati ya Dunia, ili kiwili wili nacho kitape nguvu
ya kutenda manufaa na kumuabudu Mwenyezi Mungu. Na Uislamu umetuwekea kiwango
anachotakiwa mtu ale ili siha yake isije ikamuharibikia, Subhanallah kila kitu
kikipindukia mipaka basi huwa kinaleta madhara hata cha halili kama chakula.
Mtume S.A.W katueleza katika Hadithi iliyotolewa na Imam Atirimidhiy kasema:
"ما ملأ آدمي وعاءا شرا من بطنه، حسْب ابن آدم
لقيمات يقمن صلبه، فإن كان لا محالة فثلث لطعامه، وثلث لشرابه، وثلث لنفسه"
"Hakujaza mwanadamu chombo kibaya kama tumbo
lake, inamtosha binadamu tonge kidogo zikamsaidia uhai wake, kama hakuna budi
basi aweke nafasi ya thuluthi chakula na thuluthi maji na thuluthi aweke
za pumzi".
Waislamu, mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni mwezi wa
Ibada na kuomba maghfira, ni mwezi wa kujikaribisha kwa Allah na kuutumia wakati
katika mambo ya kheri, kwani thawabu hizidishwa mara nyingi kama mnavyofahamu.
Lakini leo hii watu wengi wanadhani kuwa
Ramadhani ni mwezi wa mavyakula na hupikwa vyakula ambayo hata havijulikani wala
havina jina, marangi tofauti na ndio watu baada ya kutoka ramadhani na siha
njema kama inavyotakiwa, basi wengine hutoka matumbo yanawauma na weshazidisha
uzito kilo fulani.
Mwenyezi Mungu kakataza Israfu katika maisha yote,
kwa hivyo kufanya israfu katika mwezi wa Ramadhani dhambi hizidi, kama vile
thawadu zinapozidishwa. Leo hii kuna watu vyakula hawana, wala nguo za kuvaa za
siku kuu hawajapata, laiti pesa hizi za maakulati wanapewa masikini bisi
zingaliwafaa katika mambo yao. Lakini mtu ana khiyari kutupa chakula katika jaa,
jirani yake masikini hajui nini anachokila.
Na Allah (SW)
amekataza kutumia mali kuliko haja ya mtu kwa kusema:
( وكلوا واشربوا ولا تسرفوا إنّه لا يحبّ
المسرفين )
“ Na kuleni (vizuri)
na kunyweni (vizuri) lakini msipite kiasi tu. Hakika yeye (ALLAH) hawapendi
wapitao kiasi”.
Waislamu sisi tuwe ni
mfano mwema kwa waliobakia, ili wasihisi kwamba uislamu ni Dini ya Israfu na
kutumia mali katika mambo yasiyokuwa na haja.
والــســلام عـلـيـكـم ورحـمـة اللّه وبـركــاتــه
|