HUKUMU ZA USIKU WA KUAMKIA TAREHE 10 DHUL-HIJA

 

 

  Kulala Muzdalafa baada kuondoka Arafaat.

  Katika sunna ni kuchanganya sala mbili: ya magharibi na isha huko Muzdalafa kutokana na hadithi ya Mtume - rehema za Allah na amani zimshukie: “Kuwa yeye - rehema za Allah na amani zimshukie - alifika Muzdalafa akachanganya magharibi na isha kwa adhana moja na iqama mbili na hakusali cho chote baina yao.”Ameipokea Nasaaiy, Abu Daud, Ibnu Maajah na Ibnu Abi Shaiba.

  Muzdalafa yote ni pa kusimama isipokuwa ‘Waadi Muhas-sir’, kutokana na kauli yake - rehema za Allah na amani zimshukie: “Muzdalafa yote ni pa kusimama na msikae kwenye Muhas-sir.” Imepokewa na Ahmed. Muhas-sir ni njia ya maji bina ya Muzdalafa na Mina na ni karibu zaidi na Muzdalafa (ni eneo alipofikwa na adhabu Abraha).

  Imeruhusiwa kwa wanawake, watoto na wachungaji kuondoka Muzdalafa usiku baada ya kutua kwa mwezi.

  Ni lazima kulivuka bonde la Muhas-sir kabla kuchomoza kwa jua ila kwa dharura.

  Kuomba dua kwenye ‘Al-mash-ar Al-haram’ (Muzdalafa) ni wajibu, na inatosheleza dua yo yote au kutamka ‘Laa ilaha illa LLah’ au kuhimidi au kutamka talbia. Akifanya lo lote kati ya hayo wajibu umeshamuondokea, na asipofanya lo lote kabisa itamuwajibikia kuchinja.

 

 

 

Copyright ©2004  Uislam.net