|
|
HUKUMU ZA
SIKU YA 10 DHUL-HIJA |
Ataondoka Muzdalafa
kabla kuchomoza jua kuelekea Mina.
Akifika mwenye kuhiji
Mina ataanza kwa kulipiga Jamra la Aqaba, ambalo linaitwa Al-Jamratu L-kubra
(jamra kuu).
Kupiga jamra kunakuwa
kwa vijiwe vidogo kama punje ya dengu, na huwa
kwa vijiwe saba.
VIPI KUPIGA JAMRA:
ý
Jamra la Aqaba hupigwa kutokea ndani ya
bonde liliopo hapo kwa kuifanya Maka iwe kushotoni na Mina kuliani, kijiwe
kimoja kimoja mpaka vitimie vijiwe saba pamoja na kukabir kwa kila kijiwe.
Imepokewa kutoka kwa Jabir: “Kwamba Mtume wa
Mwenyezi Mungu - rehema za Allah na amani zimshukie - alikuwa akikabir kwa
kila kijiwe.” Imepokewa na Muslim.
ý
Wakati wa kulipiga jamra
hili huwa baada ya kuchomoza jua siku ya idi hadi kupindukia jua (adhuhuri).
ý
Inaruhusiwa kupiga jamra
hili hadi kuchwa kwa jua la siku ya idi kwa dharura na kwa wenye udhuru.
ý
Mwenye kuhiji atasita kutamka talbia
akitupa kijiwe cha kwanza kulipigia jamra la Aqaba, kutokana na hadithi ya
Al-fadhlu ibnu Abbaas: “Niliendelea kumsikia
- rehema za Allah na amani zimshukie - akitamka talbia mpaka akalipiga Jamra
la Aqaba.” Imepokewa na Rabiu.
MAZINGATIO:
Kupiga
Jamra la Aqaba ni siku ya mwanzo ya kuchinja (10 Dhul-hija) kuanzia baada
kuchomoza jua na kuendelea, na kupiga jamra zote tatu ni katika siku za
Tashriq kuanzia kupindukia kwa jua (adhuhuri) na kuendelea.
Haitoshelezi kuvifunga
vijiwe kwenye mfuko na kuvirembea bali lazima kila kijiwe kitupwe peke yake.
Hakuna
ubaya kwa mwenye kuhiji kumwakilisha mtu mwengine ampigie jamra anaposhindwa
kufanya hilo mwenyewe.
Ni
lazima kuhakikisha kuwa vijiwe vinavyorembewa vimelipata jamra, vinginevyo
atakuwa katika hukumu ya asiyepiga, na imeruhusiwa kwa dharura iwapo
vimeangukia kwenye hodhi la jamra.
|