HIJAAB YA MWANAMKE

 

Ndugu zangu watukufu, kwanza kabla hatujaingia ndani ya mikondo ya maelezo na mafahamisho kuhusu umuhimu wa Hijaab kwa mwanamke wa Kiislamu, nitapendelea kukuulizeni suali moja. Iwapo utaona chakula kimewekwa juu ya meza ambayo juu yake kuna sahani mbili, na zote sahani hizo mbili chakula ni kile kile isipokuwa sahani moja imefunikwa, na sahani ya pili iko wazi ambayo chakula hicho haikufunikwa toka kilipopakuliwa.

Njaa imekushika na mwenyeji kishasema muanze kula. Na una hiyari ya kukaa upande wowote kati ya zile sahani mbili. Jee! utachagua sahani gani upunguze chakula… sahani iliokuwa imefunikwa au iliokuwa wazi?

Nafikiri sote tutachaguwa chakula kilichofunikwa ambacho kimestirika na kuhifadhika kwa kufunikwa, kwani sahani iliyo wazi haitaacha kukaribisha nzi, mende, vijidudu katika hewa, wadokozi na waonjaji waliokuwa hawakukosha mikono yao. Kwa hivyo tunakubaliana kuwa chakula kilichositirika ndicho chakula cha kuridhisha moyo na kisichokuwa na ulakin ndani yake.

Chanzo cha maelezo haya ni kuhusu stara na hifadhi, ikiwa stara hiyo ni ya chakula, ya mavazi au mwili, stara ya malazi, stara ya makazi, stara ya kuwa mke wa watu au mume wa watu na mengineyo. Natumai kuwa sote tunaamini na kukubali kuwa stara na hifadhi katika maisha ya Muislamu akiwa mwanamume au mwanamke ni jambo la lazima na muhimu sana katika mazingara ya maisha ya Kiislamu.

Uchi wa mwanamke ni mwili mzima, isipokuwa viganja vyake na uso wake ndio si uchi kwake, yaani kwa shida anaweza kuonekana hizo sehemu tulizozitaja kwa watu waliokuwa si mahram wake. Kwa umuhimu huu wa hishma na hifadhi na matukuzo aliyopewa mwanamke itabidi  maelezo yanayofuatia yawe kuhusu hifadhi na utunzo wa mwanamke katika kivazi.

Kwa nini Mwanamke wa Kiislamu anavaa mavazi ya stara?

Mwamke wa Kiislamu anavaa kivazi chema na kujisitiri kwa sababu zafuatazo:

1-Kutii amri na maamrisho ya Dini yake tukufu.

2-Kuhifadhi nafsi yake na kutunza hadhi yake.

3-Kujitukuza nafsi yake na hishma yake.

4-Kujiepusha na shari za wadokozi.

5-Kujiepusha na macho maovu.

6-Kujiepusha na kuvunjiwa hishma.

7-kujistiri kwa kuvaa kivazi chema

Aya inayofuatia Mwenyeezi Mungu anamuamrisha Mjumbe wake Mtume Muhammad (SAW) awapelekee ujumbe waja wake wafuate tabia njema, na kivazi cha hishma na kujilinda na kujihifadhi na wasioneshe mapambo yao ambayo yanaweza kuleta fitna na matamanio maovu.

æóÞõá áøöáúãõÄúãöäóÇÊö íóÛúÖõÖúäó ãöäú ÃóÈúÕóÇÑöåöäøó æóíóÍúÝóÙúäó ÝõÑõæÌóåõäøó æóáóÇ íõÈúÏöíäó ÒöíäóÊóåõäøó ÅöáøóÇ ãóÇ ÙóåóÑó ãöäúåóÇ æóáúíóÖúÑöÈúäó ÈöÎõãõÑöåöäøó Úóáóì ÌõíõæÈöåöäøó æóáóÇ íõÈúÏöíäó ÒöíäóÊóåõäøó ÅöáøóÇ áöÈõÚõæáóÊöåöäøó Ãóæú ÂÈóÇÆöåöäøó Ãóæú ÂÈóÇÁ ÈõÚõæáóÊöåöäøó Ãóæú ÃóÈúäóÇÆöåöäøó Ãóæú ÃóÈúäóÇÁ ÈõÚõæáóÊöåöäøó Ãóæú ÅöÎúæóÇäöåöäøó Ãóæú Èóäöí ÅöÎúæóÇäöåöäøó Ãóæú Èóäöí ÃóÎóæóÇÊöåöäøó Ãóæú äöÓóÇÆöåöäøó Ãóæú ãóÇ ãóáóßóÊú ÃóíúãóÇäõåõäøó Ãóæö ÇáÊøóÇÈöÚöíäó ÛóíúÑö Ãõæúáöí ÇáúÅöÑúÈóÉö ãöäó ÇáÑøöÌóÇáö Ãóæö ÇáØøöÝúáö ÇáøóÐöíäó áóãú íóÙúåóÑõæÇ Úóáóì ÚóæúÑóÇÊö ÇáäøöÓóÇÁ æóáóÇ íóÖúÑöÈúäó ÈöÃóÑúÌõáöåöäøó áöíõÚúáóãó ãóÇ íõÎúÝöíäó ãöä ÒöíäóÊöåöäøó æóÊõæÈõæÇ Åöáóì Çááøóåö ÌóãöíÚðÇ ÃóíøõåóÇ ÇáúãõÄúãöäõæäó áóÚóáøóßõãú ÊõÝúáöÍõæäó

Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe uzuri wao isipo kuwa unao dhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, au wana wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenzao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, au wafwasi wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yaliyo khusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajuulikane mapambo waliyo yaficha. Na tubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa.

An Nur-31

Yaani tunafunzwa tabia njema na Mola wetu, tunaongozwa katika kheri na tunaepushwa na shari, kwa hivyo ikiwa hatufuati basi inakuwa tunampinga Mola wetu, Mtume wetu na wazee wetu. Sasa huo Uislamu wetu utakuwa na msimamo gani?

Mwanamke wa Kiislamu aliyejitunza na kujitukuza nafsi yake kwa kuvaa kivazi cha stara huwa amepata malezi mazuri ya Kiislamu, na anaongozwa na imani yake. Muislamu huyo havai nguo za stara kwa sababu ni kivazi cha mila na utamaduni alichokirithi kutoka kwa wazee wake, bali anatii amri ya Mola wake na kutimiza wajibu wake.

Na hii hijaab ilivyokuwa ni amri ya Mwenyeezi Mungu, basi hapana shaka Watume waliopita waliamrishwa vile vile kuwa wanawake wajistiri na kujihifadhi kwa kivazi cha stara ambacho kitawatunzia hishma yao na kuwaepusha na kuudhiwa majiani.

Tukichukuwa mfano wa wanawake wanaotumika Makanisani (Christian Nuns) utawakuta vivazi vyao vinakaribiana na vivazi vya wanawake wa Kiislamu, kwa sababu hiyo ni amri kutoka kwa Mola wao, ambayo imepotea kote na kubakia Kanisani tu.

Kulikuwa na mwanafunzi mmoja wa kike ambaye alipelekwa kusoma katika Yunivasiti huko Syria. Tabia ya mwanafunzi huyu na kivazi chake kilikuwa kikipendwa na wengi. Alikuwa akivaa nguo za stara kila siku na alikuwa akipewa hishma na wanafunzi wenzake na walimu wake.

Siku moja alikuja muandishi wa magazeti katika hiyo Yunivasiti, macho yake yakavutiwa na kupendekezewa na kivazi kizuri cha stara cha huyu mtoto wa kike. Akamuuliza “mbona wewe peke yako katika hii klasi unavaa nguo za aina ya peke yako” akaendelea kumuuliza “hizi nguo hazikufanyii joto katika joto kali hili la kiangazi”

Yule mtoto wa kike akamjibu kwa Aya ya Qur’ani:

äóÇÑõ Ìóåóäøóãó ÃóÔóÏøõ ÍóÑøðÇ áøóæú ßóÇäõæÇ íóÝúÞóåõæäó

“Moto wa Jahannam una joto zaidi laiti (watu) wangelifahamu!”

At Tawba-81

‘Wa naam’Aina hii ya chipukizi za wanawake ndio watakaojenga msimamo madhubuti wa nyumba zao na jamii zao, aina hii ya wanawake ndio watakaokuwa katika msitari  wa mbele wa kuunyanyua Uislamu kwa kuonesha mfano mzuri na kuwapa malezi mema watoto wao na kusimama imara katika jihadi ya kujilinda na kila sababu itakayompelekea kuteleza na kumuasi Mola wake.

Copyright ©2004  Uislam.net