BIBI MARYAM

MAMA YAKE NABII IISAA (AS)

 

ÞóÇáóÊú Ãóäøóì íóßõæäõ áöí ÛõáóÇãñ æóáóãú íóãúÓóÓúäöí ÈóÔóÑñ æóáóãú Ãóßõäú ÈóÛöíøðÇ(20)  ÞóÇáó ßóÐóáößö ÞóÇáó ÑóÈøõßö åõæó Úóáóíøó åóíøöäñ æóáöäóÌúÚóáóåõ ÂíóÉð áöáäøóÇÓö æóÑóÍúãóÉð ãöäøóÇ æóßóÇäó ÃóãúÑðÇ ãóÞúÖöíøðÇ(ãÑíã 20-21)

Qaalat Annaa yakuunu li ghulaamun walam yamsasni Basharun walam aku baghiyyaa?! Qaala kadhaaliki qaala Rabbuki huwa `Alayiya hayyimun , wa linaj-`alahu  aayatan linnasi wa Rahamatan Minnaa, wa kaana amran maqdhiyya. (Surat Maryam : 20-21 )

Mwanamke ye yote, hata mnyama aw mti, hawezi kuzaa bila ya mwanamume. Hapana ubishi. Kwa qudra Yake Mwenyewe Mola, Nabiya Llaahi Iisaa (AS) kazaliwa bila ya baba wa aina ye yote ile itakavyomkinika. Bibi Maryam katukuzwa na kusifiwa na Muumba kutokana na kila aina ya uchafu. Huku kumzaa Iisaa (AS) ni miongoni mwa miujiza Yake Mwenyewe Mwenye enzi Mungu.

 Kazaliwa Maryam katika nyumba ya dini na ya utawa sana. Mama yake aliposhika mimba aliweka nadhiri kuwa hicho kitakachozaliwa kutoka tumboni mwake atakitowa kitumikiye dini huko katika Sinagongi  (Msikiti wa Kiyahudi na wala si kanisa la Kinasara). Alipozaa akanena, :Ewe Mola wangu nilichozaa ni mtoto wa kike na mwanamke si sawa sawa na mwanamume ; na mimi nimemwita Maryam. Nakuomba Mola wangu umuwepushe yeye na vizazi vyake na shetani. " Mola akamtakabaliya, aw kama vile ilivyoeleza Quran Tukufu.

ÅöÐú ÞóÇáóÊú ÇãúÑóÃóÉõ ÚöãúÑóÇäó ÑóÈøö Åöäøöí äóÐóÑúÊõ áóßó ãóÇ Ýöí ÈóØúäöí ãõÍóÑøóÑðÇ ÝóÊóÞóÈøóáú ãöäøöí Åöäøóßó ÃóäúÊó ÇáÓøóãöíÚõ ÇáúÚóáöíãõ(35) ÝóáóãøóÇ æóÖóÚóÊúåóÇ ÞóÇáóÊú ÑóÈøö Åöäøöí æóÖóÚúÊõåóÇ ÃõäúËóì æóÇááøóåõ ÃóÚúáóãõ ÈöãóÇ æóÖóÚóÊú æóáóíúÓó ÇáÐøóßóÑõ ßóÇáúÃõäúËóì æóÅöäøöí ÓóãøóíúÊõåóÇ ãóÑúíóãó æóÅöäøöí ÃõÚöíÐõåóÇ Èößó æóÐõÑøöíøóÊóåóÇ ãöäú ÇáÔøóíúØóÇäö ÇáÑøóÌöíãö(36)ÝóÊóÞóÈøóáóåóÇ ÑóÈøõåóÇ ÈöÞóÈõæáò ÍóÓóäò æóÃóäúÈóÊóåóÇ äóÈóÇÊðÇ ÍóÓóäðÇ æóßóÝøóáóåóÇ ÒóßóÑöíøóÇ ßõáøóãóÇ ÏóÎóáó ÚóáóíúåóÇ ÒóßóÑöíøóÇ ÇáúãöÍúÑóÇÈó æóÌóÏó ÚöäúÏóåóÇ ÑöÒúÞðÇ ÞóÇáó íóÇãóÑúíóãõ Ãóäøóì áóßö åóÐóÇ ÞóÇáóÊú åõæó ãöäú ÚöäúÏö Çááøóåö Åöäøó Çááøóåó íóÑúÒõÞõ ãóäú íóÔóÇÁõ ÈöÛóíúÑö ÍöÓóÇÈò (37) ((ÇáÚãÑÇä 35-37))

Idh Qaalat Mraatu `Imraana Rabbi inni nadhartu laka maa fii batni muharraran, fataqabbal minnii innaka Ssamii`u L`aliim. Falammaa wadhaathaa untha qaalat Rabii Inni wadha `utuhaa unthaa wa Llaahu A`alamu bima waghaat-ha wa Laisa dhdhakaru Kal unthaa wa inni samaituhaa Maryam.  Wa Inni U`idhuhaa bika wa Dhurriyyatahaa mina Sh-shataani Rrajiim. Fataqabbalahaa Rabbuhaa biqabuulin hasanini. Waanbatahaa nabaatan hasanan………(Surat aali `Imraan : 35-37).

Baada ya kifo cha baba yake, Bwana `Imraan, na Maryam yungali mtoto mchanga, hapa palikuwa pata shika nguwo chanika. Ugomvi uliyendeleya juu ya nani wa kumleya Maryam. Kutaka kukomesha ugomvi wakakubaliyana, na kura ikapigwa pale pale. Matokeyo yake, ilikuwa kura ilimuangukiya Bwana Zakaria, mume wa haloo yake ; mama yake mdogo : Maryam.

Maryam alitumiya utoto wake katika Sinagogi akiyhabudu na kutumika. Haya yalikuwa kwa ajili ya kutekeleza ile nadhiri ya mama yake ya kukitowa kiliomo tumboni mwake, wakati alipokuwa na mimba, kitumikiye sinagongi- yaani msikiti wa Mayahudi.

MARYAM ALIFANYA KAZI HII NA KUYENDELEYA NAYO KWA BIDII HADI ILE DAKIKA YA MWISHO, WAKATI AMBAWO YEYE ALIPOCHAGULIWA NA MUABUDIWA NA KUPEWA ILE SIRI KUBWA KABISA,YA HIZO SIRI KUBWA.IMEZIDI SIRI ZOTE.  APAKUCHAGULIWA MWANAMKE MWENGINE YE YOTE YULE WA KUPEWA SIRI HIYO ILA YEYE TU MWENYE YALE MALEZI TULIYOYATAJA HAPO JUU.  KALELEWA KIDINI NA YEYE KALELEKA. NANI TENA ALIYELELEKA KAMA YEYE, HATA AACHWE MARYAM NA KUPEWA HUYO MWINGINE. SIRI HII HAWEZI KUYICHUKUWA MTU ILA MWENYE MALEZI MEMA NA YA DINI.

Bibi Maryam akiwa kakaa peke yake akitafakuri hapo alisikiya sauti ikitoka ndani huku ikinena : "Mweye enzi Mungu akuleteya maneno ya bishara na ya matumaini mema; nayo ni utazaa YESU BIN MARYAM ambaye ndiye atakayekuwa mtu mtukufu hapa duniyani na kesho Akhera; naye atakuwa miongoni mwa hawo L- Muqarabiina "Kusikiya maneno haya Maryam alisituka bila ya kiyasi na alipigwa na mshangao usio na kifani. Kinyume nasi lewo. Mtu lewo angeliona fahari.

Baada ya kuchemsha bongo na kuvuta fikira Maryam aliuliza na kuhoji ili apate kujuwa. Hoja yake ilikuwa vipi yeye ataweza kuzaa na hali hakuwonana na mtu wala hakuwa mtu mchafu..? Akajibiwa :- "Amri ya Allah hayifutiki. Hivi ndivyo atakavyo Mola na ndivyo aamrishavyo. Vyengine hayiwezi kuwa. Na huyu mwanawe atakuwa ni miyujiza na piya ni rehema kutokana na Mwenye enzi Mungu ; aw kama vile.

Hapo Maryam hakuwa na njiya ila kusalimu amri na kukaa kungoja hiyo amri ya Mola:-

                     æÃÐÇ  ÞÖì ÃãÑÇ ÝÇäãÇ íÞæá áå ßä Ýíßæä       

Alikaa hata akahisi kuwa mtoto tumboni naye anataharuki humo tumboni. Aliyona ayibu gani hii, mwari kuzaa ! Akakimbiya na kutafuta mahali mbali pa kujificha na kujisitiri.

Wakati wa uchungu wa kuzaa ulipomjiya, aliyomba du`aa akatike vipande vipande na afilie mbali ili asahauliwe, astirike na asiayibike katu. (wakati wetu huu wa lewo mtu angelikamatiwa ye yote akabandikwa mimba hiyo, japo watu wanajuwa kuwa hii si mimba yake. Kwa kutaka kujidanganya- eti wawo wanajistiri kumbe wamo huwogeleya katika bahari ya haramu).

Inafika hadi maadui si wa Unasara tu bali wa dini zote kujusurisha na kunena : Kwanza lazima nistghafiru kabla sijasema nini wa wanamsingiziya Mtume wa Mwenye enzi Mungu Iisaa (AS). Wanasema (Astaghfiru Llaah) kwamba Bibi Maryam alitembea na Yusuf Seremala - Najjar (Carpenter) ndiwo akazaliwa Nabii Iisaa (AS). Huu ni mwisho wa ujeuri kumsingiziya Mtume kuwa ni mtoto wa haramu.

Barnabas anasema katika Biblia yake (The Gospel of Barnabas).

"Alikuwepo mwanamke bikira mtakatifu jina lake Maryam anayetokana na Daud, aliogopa alipojiwa na Malaika Jibril aliyemwambia, "Usiogope Mola wako kakupenda na kukuchaguwa wewe uwe mama wa Mtume atakayepelekwa kwa Mayahudi ili awawongoze katika njiya ya Mungu. Msichana Maryam akauliza :-

"Vipi itayumkinika nizaye na hali ya kuwa simjuwi mwanamume ? " Jibril akajibu :-

"Ewe Maryam, Mungu kaumba mtu bila ya mke, Yeye anaweza kumfanya ndani yako mtu bila ya mume, kwani hapana kitu muhali kwake Yeye".

Maryam kuogopa wakati mimba itakapokuwa kubwa, watu wakijuwa watampiga mawe kama ni adabu ya uzinifu, hapo atamtaka Yusuf amuwowe. Yusuf alipoona mimba pevu aliogopa lawama ya Mungu akamtenga mkewe. Usiku akajiwa na Malaika kumwambia :- Usiogope huyu bikira atazaa mtoto jina lake Iisaa naye hatakunywa mvinyo na vinywaji vikali na wala hatakula nyama isiyokuwa safi, kwani yeye ni mtakatifu wa Mungu kutoka katika tumbo lake. Yeye ni Mtume wa Bani Israaiil (Mayahudi).

Kukaa Yusuf akakaa na mkewe milele.*

Tukisoma Agano Jipya tutawona Luka (Luke) na Matthayo (Matthew) wananasema maneno karibu sawa na ya Barnabas. Ama Marko (Mark) na Yohana (John) hawataji kitu kuhusu uzazi wa Iisaa (AS). Matthayo anasema:-

"Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi :- "Yesu, mama yake alipokuwa anaposwa na Yusuf kabla hawajakaribiyana, aliyonekana ana mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Naye Yusuf, mumewe kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumuayibisha, aliazimu kumuacha kwa siri. Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama Malaika wa Bwana alimtokeya katika ndoto akisema : "Yusuf mwana wa Daud, usihofu kumchukuwa Mariamu mkewo, maana mimba yake ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu."

Hayo tuliyonukulu hapo juu yanaonesha wazi namna gani Uislamu unavyokubaliana na baadhi ya mafunzo ya Unasara. Si ajabu hayo kwani Mayahudi wanamuamini Mtume Muusaa (AS) tu na Wanasara wanamuamini Iisaa (AS) na Muusaa (AS), ama Uislamu unawaamini Mitume ya Allah yote laki moja na kitu bila ya ubaguzi. Muislamu akimbaguwa Mtume mmoja tu basi kesha koseya.

Pale aliposhikwa na uchungu alijitenda kando mbali na watu. Baada ya kupasuwa chupa aliyamrishwa autikise mtende ili tende mbichi zianguke na apate kula. (wanaume chungu nzima hawawezi kuutikisa mtende ; kwani mtende ni sawa na mnazi ; sembuze mwanamke). Kwa qudra Zake Mola akawutikisa na zikaanguka tende mbichi akala.

Kuliya kitoto ng`aa walikuja watu wake ili kumchukuwa na huku wakimmiminia wingi wa lawama ya kumlaumu kwamba jambo hili katu halikuwahi kutokeya upande wawo, juu ya kuwa wote wale wanamjuwa kuwa yeye si mchafu wala hapendi uchafu. Hapo hapakuwa na kazi ila kurembeya makombora juu ya makombora ya laana na malawama.

_________________________________________

* Uislamu unasema Maryam alikuwa bikira bila ya kuolewa.

ÝóÃóÔóÇÑóÊú Åöáóíúåö ÞóÇáõæÇ ßóíúÝó äõßóáøöãõ ãóäú ßóÇäó Ýöí ÇáúãóåúÏö ÕóÈöíøðÇ (29) ÞóÇáó Åöäøöí ÚóÈúÏõ Çááøóåö ÂÊóÇäöí ÇáúßöÊóÇÈó æóÌóÚóáóäöí äóÈöíøðÇ (30) æóÌóÚóáóäöí ãõÈóÇÑóßðÇ Ãóíúäó ãóÇ ßõäÊõ ýæóÃóæúÕóÇäöí ÈöÇáÕøóáóÇÉö æóÇáÒøóßóÇÉö ãóÇ ÏõãúÊõ ÍóíøðÇ (31)óÈóÑøðÇ ÈöæóÇáöÏóÊöí æóáóãú íóÌúÚóáúäöí ÌóÈøóÇÑðÇ ÔóÞöíøðÇ (32) æóÇáÓøóáóÇãõ Úóáóíøó íóæúãó æõáöÏúÊõ æóíóæúãó ÃóãõæÊõ æóíóæúãó ÃõÈúÚóËõ ÍóíøðÇ (33)

Fa Ashaarat Ilaihi Qaaluu: Kayfa Nukallimu Man Kaana Fil Mahdi Sabiyyaa Qalaa: Inniy `Abdu Llaahi; Aataaniuya L-Kitaaba, Wa Ja`Alaniy Nabiyyaa; Wa Jaalaniy Mubaarakan Ayna Maa Kuntu, Wa Awsaany Bi `Ssalaati Wa Zzakaati Maa Dumtu Hayyaan, Wa Barran Bi Waalidatiy Wa Lam Yaj-Alniy Jabbaran Shaqiyyaa. Wa Isalaamu `Alaiyya Yawma Wulidtu Wa Yauma Ub`Athu Hayyaan.

Bibi Maryam aliwapa ishara ili wamsemeze huyu mtoto mchanga. Wawo wakasema:

 “Vipi  tumsemeze huyu mtoto mchanga aliopo katika mlezi? Isa`a akawajibu: Mimu ni mja wa Mwenye enzi Mungu. Kanipa kitabu na kanijaaliya kuwa ni Mtume. Akanifanya kuwa ni mwenye baraka po pote pale nitakapokuwa; na akaniwusiya `Salaa na kutowa Zakaa maadamu mimi ni hayi. Na niwe mwema kwa mama yangu, wala hakunifanya niwe jeuri jabari na mwingi wa kiburi. Salama na amani ziniteremkiye mimi pale nilipozaliwa, na wakati wa kufa na pale nitakapofufuliwa ni hayi (Maryam: 29-32)

Yote haya aliyapokeya kimya, moyo shuwari, hana hila. Hii ni amri ya Mwenye enzi Mungu. Vitabu vikubwa vya Umisheni (Ukristo) vinaeleza shida alizozipata Bibi Maryam. Alistahamili ukomo wa stahamala ; na hata aliposhindwa kuvumiliya ilimjiya fikira ya kugura nchi. Alikimbiliya yeye na mtoto wake - Nabiya Llahi Iisaa (AS) na kwenda naye huko Misri ili ajiyepushe na maudhi yaliyokuwa kwa wingi.

Hata huko Misri mambo hayakuwa mazuri sana. Vipi mtoto wa kike aliyehama kwawo kwenda huko ugenini asipomjuwa mtu, huko hana mbele wala nyuma atawezaje kuleya mtoto kwa raha ? Maisha hapo, bila ya shaka yalikuwa ni ya shida, ingawa kitu kimoja nacho ni cha maudhi kilipunguwa.

Kutaka kuendesha maisha ilimbidi kufanya kazi ya kusokota katani, aw ya kuvuna mazawo ya watu kwa ujira na huku Nabii Iisaa (AS) yu mbavuni mwake. Yote haya na mengineyo aliyafanya kwa kutafuta tonge na gwanda ya chongo yake moja.

Mama ni mwenye kushughulikiya habari ya masomo ya mwanawe. Ilipofika wakati wa kupelekwa kusoma, Maryam hakuchelewa hata dakika moja, ila aliharakiza kumpeleka Iisaa (AS) kwa mwalimu ambaye alimfunza kusoma  na adabu njema. Baada ya miyaka kumi na mbili kupita, sisi tunamuwona Maryam na kijana wake Iisaa (AS) wakifunga virago vyawo na mguu nipate. Hawakusimama na mguu na njiya ila wawo wapo Baitil Maqdis. Hapo tena walisita na walituwa na kufanya mastakimu yawo kati ya mji wa Nnaasira. Sasa hapa maisha hayakuwa mabaya kama vile yalivyokuwa katika mazingira ya kabla ; kwa hivyo wawili wawo waliweza kuwishi mpaka Seyyidna Iisaa (AS) akawa mtu mzima wa kutegemewa.

Taabu zote hizo alizozipata Nabii Iisaa (AS) hazikuwa ila ni kule kutayarishwa na kupokea Risala  ya mbinguni. Alipopewa Utume, mama yake ndiye aliyekuwa msaidizi wake nyumbani na ndiye hasa aliyekuwa akimuelezea yale mambo makuu yaliyokuwa yakimfika aliokuwa akiyawona. Huruma za mama hapo ndipo mahali pake na ndiwo wakati wake wa kufanya kazi. Kazi kubwa hasa aliyokuwa nayo ni ya kumliwaza, kumtia nguvu na kumpa moyo wa kuendeleya na ile kazi yake pevu aliopewa na Muabudiwa. Jukumu hili Tukufu, lazima yule apewaye apate nguzo za kweli za kutegemewa.

Ala ! Tazameni mambo haya jamani ! Huyu kijana wa miyaka thelathini aliyesimama na huyu bibi makamo hapa juu ya hili Jabali Zaitun ni nani ? Hawa ni Bibi Maryam pamoja na Nabii Iisaa (AS). Wamekuja kuchuma zaituni yeye na mama yake, Nabii Iisaa (AS) ilimjiya Ru`yaa  na kujuwa kuwa yeye ni Mjumbe aliyeletwa kwa Bani Israaiil. Hapo hakujijuwa ila aliona anageuka kuliya kwake na kumuelezea mama yake Maryam, maneno yenye maana ifuatayo :-

"Tokeya lewo inanibidi zinifike shida mimi na taabu nyingi sana kwa ajili ya Mwenye enzi Mungu. Baada ya lewo itaniwiya vigumu na wala sitaweza tena kuwishi pamoja nawe na wakati huwo huwo niwe naweza tena kutekeleza wajibu wangu wa deni lile la kukutumikia, kwa ule wingi na ukubwa wa jukumu na dhamana nilizonazo..".

Mama mtu kusikiya haya alinena :-

"Ewe mboni ya macho yangu, mimi nalitanabahishwa juu ya hayo kabla ya kuzaliwa kwako. Mungu akubariki na piya akusaidiye juu ya hiyo dhamana yako. Amina".

Iisaa tokeya siku hiyo akatengana na mama yake ili ashughulikie mambo na mafunzo yake ya dini, baada yakuwa naye kwa muda wa miyaka thelathini. Wakati wote huwo alikuwa akitayarishwa kwa hilo jukumu Takatifu. Ingawa hapo juu tulisema kuwa walitengana lakini kwa qudra na kwa miujiza Yake Mwenyewe Mola walikuwa wakikutana na kuwonana.

 Quran imesema kwa wazi kabisa :-

æÌÚáäÇ ÇÈä ãÑíã æÃãå Âíå

Wajaalna bna Maryam wa Ummah Aayatan

Tumemjaalia mtoto wa Maryam na mama yake ni miujiza

           æÌÚáäÇåÇ æÃÈäåÇ ÂíÉ ááÚÇáãíä

          Waja`alnahaa na bnahaa Aayatan lilamiin.

Tukamjaaliya yeye na mwanawe ni mfano na aya kwa walimwengu.

 

Copyright ©2004  Uislam.net