BIBI HAAJIR (I)

  MAMA YAKE SEYYIDNA ISMAAIIL ( A. S )

 

Bibi Saara, Mke wa Seyyidna Ibraahiim (Khalilu Rrahman, Alaihi Ssalam),  alikaa na mumewe miyaka mingi sana bila ya wawo kuruzukiwa mtoto : kwa vile alivyokuwa ni tasa. Alikuwa akimpenda mumewe hadi na akitamani aruzukiwe mtoto.

 Baada ya kuchemsha bongo lake sana aliyoneleya ni bora amtunukiye mumewe huyu mjakazi wake alyetoka naye katika safari zake za Misri na kwengineko. Hii ilikuwa ni hatuwa iliobarikiwa kikweli, kwani ndiwo iliokuwa sababu ya kizazi kitukufu kuja hapa duniyani.

 Seyyidna Ibraahiim alipokeya tunza hii kwa furaha kuu na kwa moyo mkunjufu, na hakuchukuwa muda ila Haajir alishika mimba na Seyyidna Ismaaiil akazaliwa.

 Kedi ya kike haishindiki na mwanamke asiyekuwa na wivu juu ya kitu si mwanamke aw kimeshachujuka kitu hicho. (Nyuki mkali kwa asali yake).

 SAARA BIBIYE, KAKAA NA MUMEWE MIYAKA NENDA MIYAKA RUDI BILA YA KUZAA.LEWO HICHI KIJAKAZI UKURUTU KIMEWEZA KUPATA KITU ALICHOKUWA AKIKITAMANI AKIPATE YEYE PAMOJA NA MUMEWE. MAISHA GANI HAYA...!  HERI YA KUWISHI MOTONI KULIKO MAISHA HAYA..!

 Nani awezaye kustahamili madhila kama haya ? HAPANA

Bibi Saara wivu ulimfunika vitanga vya macho na akasahawu kuwa yeye mwenyewe ndiye aliyemtunukiya mwenye Seyyidna Ibraahiim huyu bibi Haajir na akazaliwa Seyyidna Ismaaiil (AS), Saara alimsimamiya mumewe kidete ili kumhamisha Haajir pamoja na mwanawe. Hila zake zote Ibraahiim (AS) zilikwisha. Hapana salama ila tulipomuona Seyyidna Ibraahiim (AS) anaondoka huko L- Khaliil Filastin (Palestine) na kuyelekeya kusini na nyuma yake kufuatwa na Bibi Haajir kabeba mtoto wake mgongoni. Safari yawo hii ya kwenda msitu na nyika ilisita walipofika Makka. Makka wakati huwo hapakuwa na kitu cho chote ila jangwa lisiloota kitu.

Pahala hapa palikuwa pakipitiwa wakati fulani na wachunga wanyama na wakati mwengine maharamiya wakipita huku na huko.

Seyyidna Ibraahiim (AS) alipokuwa anakwenda zake Haajir ilimjiya hofu akawa anampembejeya asimuwache peke yake hana mtu ila hichi kitoto kichanga tu kati ya jangwa lenye wingi wa vitisho kwa vile halina kitu aw watu.

 Mwanamume ana sifa ya ukatili na kutokuwa na huruma. Hatukumuwona Seyyidna Ibraahiim (AS) ila kageuza uso na kakaza mwendo bila ya kugeuka nyuma ili isije roho yake ikalayinika na kuonesha huruma pindi akiwatazama usoni. Uso umeumbwa na haya. Kumjibu piya hakuweza kwa vile isije sauti yake ikawonesha kitetemeshi, na kwa hivyo Haajir huenda akafichuwa ile siri iliyomo moyoni mwake ; na ni kuwa Ibraahiim (AS) hafanyi hivi kuwa yeye hampendi. Yeye anafanya hivyo kwa sababu nyengine kabisa.

 Katika kukaza kwake mwendo huku alimsikiya Haajir akisema:"Je!!, Mwenye enzi Mungu ndiye aliyekuamrisha haya..?  Kwa wingi wa majonzi yaliyomjaa yeye alimjibu bila ya kufikiriya aw kuhisi aw kuzingatiya nini kasema, "Naam..!.

 Kusikiya hivi, Bibi Haajir ilimtoka :- "Kama ni hivyo, basi Mungu si mtovu". Hapo aliyinama chini kimya na vile ilivyokuwa kayinama hakuweza kumuwona Seyyidna Ibraahiim (AS) kanyanyua mikono juu kwa unyenyekevu mkuu na huku akiomba du`aa na mwili mzima umeelekeya kwa Muumba viumbe vyote.

æóÅöÐú ÞóÇáó ÅöÈúÑóÇåöíãõ ÑóÈøö ÇÌúÚóáú åóÐóÇ ÇáúÈóáóÏó ÂãöäðÇ æóÇÌúäõÈúäöí æóÈóäöíøó Ãóäú äóÚúÈõÏó ÇáúÃóÕúäóÇãó (35) ÑóÈøö Åöäøóåõäøó ÃóÖúáóáúäó ßóËöíÑðÇ ãöäú ÇáäøóÇÓö Ýóãóäú ÊóÈöÚóäöí ÝóÅöäøóåõ ãöäøöí æóãóäú ÚóÕóÇäöí ÝóÅöäøóßó ÛóÝõæÑñ ÑóÍöíãñ (36)

Rabbi J-`al haathaa L-Balada Aaminaan, Wa Jnuubni wa baniyya ana Na`abuda L-Asnaama. Rabbi Innahunna Adhlalna Kathiiran Mina Nnaasi, Faman Tabi`any Fainnahu Minniy, Wa man `Asaany Fainnaka Ghafurrun R`ahiim.

" ............ Mola wangu !  Uujalie mji huu ( wa Makka) uwe wa amani.  Na uniepushe mimi na wanangu kuabudu masanamu. Mola wangu !   Hakika (masanamu) hawa wamepoteza watu wengi. Basi aliyenifuata ni wangu mimi (utamlipa mema kama ulivyotuahidi) ; na aliyeniasi (unaweza kumsamehe na usimtese) kwani Wewe ni Mwingi wa msamaha na Mwingi wa Rehema"  (Quraan, Surat Ibraahiim 35-36).

 "Ewe Mola nimewaweka baadhi ya vizazi vyangu mahali pasipoota kitu katika nyumba Yako Tukufu. Yaa, Rabbi wajaalie wawe wakidumisha `Salaa na uzifanye baadhi ya nyoyo zinavutika kwawo. Bwana wangu, piya uwaruzuku baadhi ya vyakula na matunda ili huenda wakakushukuru."  aw kama inavyoeleza aya ifuatayo :-

ÑóÈøóäóÇ Åöäøöí ÃóÓúßóäÊõ ãöäú ÐõÑøöíøóÊöí ÈöæóÇÏò ÛóíúÑö Ðöí ÒóÑúÚò ÚöäúÏó ÈóíúÊößó ÇáúãõÍóÑøóãö ÑóÈøóäóÇ áöíõÞöíãõæÇ ÇáÕøóáóÇÉó ÝóÇÌúÚóáú ÃóÝúÆöÏóÉð ãöäú ÇáäøóÇÓö Êóåúæöí Åöáóíúåöãú æóÇÑúÒõÞúåõãú ãöäú ÇáËøóãóÑóÇÊö áóÚóáøóåõãú íóÔúßõÑõæäó  (37) ((ÇÈÑÇåíã -37)).

Rabbana inni askantu mindhurriyyatii biwadin ghairi dhii zarain `inda baitika l Huharrami. Rabbanaa liyuqiimuu `Ssalaata ; faj`al af-idatan mina nnasi tahawii ilaihim Warzuqhum mina ththamaraati la`allahum yashkuruun (Ibrahiim : 37 )

Baada ya hapo akaongoza njiya ya kwenda zake kwa mkewe wa pili : Saara.

Hapo Bibi Haajir akawa anajishughulisha na mwanawe ili apate kujipumbaza na kujitowa majonzi aliyonayo. Kwa njiya hii hakuhisi ule upweke aliokuwa akiishi ndani yake.

Starehe hii ya mbwa kukaliya mkiya wake iliendeleya kwa muda tu. Taabu ilikuwa imemkaliya meno wazi. Baada ya kumalizika chakula tu na maji, na hasa ule wakati Ismaaiil (AS) mchanga aliposhikwa na kiw ndipo alipoiyona duniya nyeusi.

Haajir hakuwa na jambo jingine wakati huu ila ni kunyanyuka tu na kuhangayika kutafuta maji. Alipochoka bila ya yeye kupata kitu alioneleya ni bora apande juu ya jabali, asaa akawona maji aw dalili ya maji. Kutazama akawona hapana jabali lililo karibu naye ila lile la `Safaa. Akenda mbiyo na kurudi bondeni mbiyo na akijiuliza, " Jee pana mtu ? aw nasikiya sauti ya mtu  “Baada ya kuwona hapana. Kenda mbiyo Marwa, kwa tamaa yakuwa hapo ataona alama yo yote ile ya maisha na uhayi. Kumbe : Ng`ngoo ! ! !

Kusita hapasitiki, kukaa hapakaliki kwa kukiyona kijitoto kichanga namna kinavyochachatika na kuhaha kwa wingi wa kiw. Jambo hili lilimfanya Haajir ayende mbiyo na kurudi baina ya `Safaa na Marwa mara saba ; mbiyo ya mtu aliyeishiwa na kuemewa hajuwi nini la kufanya. Zilipomkaa na kumpaa pumzi, alianguka juu ya mchanga mbele ya mwanawe Ismaaiil (AS) huku akingojeya matokeyo ya mwisho yenye wingi wa huzuni.

ÑóÈøóäóÇ Åöäøóßó  ÊóÚúáóãõ ãóÇ äõÎúÝöí æóãóÇ äõÚúáöäõ æóãóÇ íóÎúÝóì Úóáóì Çááøóåö ãöäú ÔóíúÁò Ýöí ÇáúÃóÑúÖö æóáóÇ Ýöí ÇáÓøóãóÇÁö (38) ÇáúÍóãúÏõ áöáøóåö ÇáøóÐöí æóåóÈó áöí Úóáóì ÇáúßöÈóÑö ÅöÓúãóÇÚöíáó æóÅöÓúÍóÇÞó Åöäøó ÑóÈøöí áóÓóãöíÚõ ÇáÏøõÚóÇÁö(39) ÑóÈøö ÇÌúÚóáúäöí ãõÞöíãó ÇáÕøóáóÇÉö æóãöäú ÐõÑøöíøóÊöí ÑóÈøóäóÇ æóÊóÞóÈøóáú ÏõÚóÇÁö(40) ÑóÈøóäóÇ ÇÛúÝöÑú áöí æóáöæóÇáöÏóíøó æóáöáúãõÄúãöäöíäó íóæúãó íóÞõæãõ ÇáúÍöÓóÇÈõ(41)   ((ÇÈÑÇåíã 38-41))

Rabbanaa Innaka Ta`alamu Maa Nukhfii, wa maa Nu`ulinu, Wa Maa Yakhfaa `Ala Llaahi Min Shay-in fil Ardhi Walaa fis Samaa: Al`Hamdu Lillaahi Lladhii Wahaba Lii `Alaal Kibari Ismaa`iila wa Is-Haaqa; Inna Rabbi Samii`u Ddu`aa. Rabbi J`alnii Muqiima S`salaati Wa Min Dhurriyatii. Rabbanaa Taqabbal Du`aa. Rabbaanaa Ghfir Lii Wa Liwaalidayya Wa Lil Mu`uminiina Yawmma Yaquumu L-Hisaab.

"Mola wetu ! Hakika Wewe unajuwa siri yetu na tunavyodhihirisha. Na hapana kifichikacho Kwako, cha ardhini aw cha mbinguni. Namshukuru Mwenye enzi Mungu kunijaaliya juu ya uzee wangu kuwapata Ismaaiil na Is-haaq,  Hakika Mola wangu ni Mwenye kusikiya du`aa. Ewe Mola !  Nijaaliye nidumishe `Salaa na vizazi vyangu, Bwana wetu tupokelee du`aa zetu. Mola wetu ! Nighufirie mimi na wazee wangu na Waislamu wote siku ya Qiyama"  (Ibraahiim 38-41).

ÑóÈøóäóÇ æóÇÌúÚóáúäóÇ ãõÓúáöãóíúäö áóßó æóãöäú ÐõÑøöíøóÊöäóÇ ÃõãøóÉð ãõÓúáöãóÉð áóßó æóÃóÑöäóÇ ãóäóÇÓößóäóÇ æóÊõÈú ÚóáóíúäóÇ Åöäøóßó ÃóäúÊó ÇáÊøóæøóÇÈõ ÇáÑøóÍöíãõ (128) ÑóÈøóäóÇ æóÇÈúÚóËú Ýöíåöãú ÑóÓõæáðÇ ãöäúåõãú íóÊúáõæ Úóáóíúåöãú ÂíóÇÊößó æóíõÚóáøöãõåõãú ÇáúßöÊóÇÈó æóÇáúÍößúãóÉó æóíõÒóßøöíåöãú Åöäøóßó ÃóäúÊó ÇáúÚóÒöíÒõ ÇáúÍóßöíãõ (129) (( ÇáÈÞÑå 128-129))

Rabbanaa Wa J-`Alnaa Muslamayni Laka, Wa Min Dhurriyatinaa Ummatana Muslimatan Laka, Wa Arinaa Mnaasikanaa; Wa Tub `Alaynaa, Innaka Anta Ttawwaabu Rra1hiim. Rabbanaa Wa B`Ath Fiihim Rasuulan Minhum, Yatluu `Alaihim Aayaatika Wa Yu`Allimuhumul Kitaaba Wal-Hikmata Wa Yuzakkiihim Innaka Anta L-Aziiza L-`Hakiim

"Mola wangu ! Tufanye tuwe wanyenyekevu sisi wawili pamoja na baadhi ya vizazi vyetu,utuongoze njiya njema na utusamehe. Ewe Mola ! Uwaletee Mtume kutokana nawo awafunze Kitabu Chako na dini Yako na ilimu nyengine, ili wajitakase na kila baya ".  (Al Baqra : 128.........129 ).

 Hapakumuweka hapo ila tunamuwona kasimama, kama aliyechagawa, kwa wingi wa zile kelele za kitoto zilizokuwa zikimkata maini na kuwona maisha ya mwanawe yanatoweka. Hapo alijikusanya kusanya na kusema " Sitakaa na kuwona kwa macho yangu kifo cha mwanangu na niliyemuoneya machungu . " Ya Allah !!" Hapo mandhari hayisemeki namna ilivyokuwa ikitisha. Kila kitu hapo kilikuwa kimesita, sauti haisikilizani, upepo hauvumi na hata pumzi hazikuwa zikisikika. Vitu vyote vikingoja dakika ya mwisho. Pahala hapo hapakuwa na kiumbe cho chote ila wanyama wa mwitu tu. Labda wawo waliharakisha hii dakika ya mwisho ili wapate kunufaika.

Haajir kasema kweli :- " Mungu si mtovu "   uokovu Wake papo hapo ukaja kwa kupasuka  MAJI YA ZAMZAM.  Kuwona Haajir maji haya alikuwa na nguvu za zayidi ya simba. Alijiyona sasa yeye anaweza kuichukuwa duniya nzima kwa mkono mmoja tu. Nani kama Haajir? Mungu kamrehemu mja Wake kwa kumteremshiya maji kutoka mbinguni. Neema ilioje hii ! Hapana tena.

 Kwa nini Haajir asiwe hivyo na hali Quran inasema wazi na kwa kinywa kipana :-

                        ( æÌÚáäÇ ãä ÇáãÇÁ ßá ÔÆ  Íí )

   { Waj`alanaa mina l maai kulla shaiin hayyi }       

“Tumejaaliya uhayi wa kila kitu uwe unatokana na maji "

 Mishipa ya maisha iliyanza kidogo kidogo kupiga pembezoni mwa Zamzam. Kama vile ujuwavyo kila msafiri kuwa dalili ya kukurubiya pahala penye maisha ni kuwona ndege. Kwa hiyo basi, wote wale waliyokuwa wakipita karibu na Makka waliduwaa kuwona ndege kati ya hili jangwa.Baada ya kupagunduwa mahali patokapo hayo maji wengine walitaka ruhusa ya kuwishi hapo . Haajir aliyapokeya maombi yawo kwa ule moyo wake mkunjufu. Inasemekana wakaazi mwanzo walikuwa ni wa kabila ya Jurhum.

Kidogo kidogo watu wakawa wanakuja kuwishi hata lewo ikawa Makka ina wakaazi wengi sana, na ndipo wayelekeyapo Waislamu wa duniya nzima wakati wa Salaa. Piya kwenda mbiyo za `Safaa na Marwa ni kazi mpaka hii lewo ifanywayo na kila Muislamu aendaye kuhidji Makka aw kufanya Umrah kwa ajili ya kule kutekeleza nguzo ya tano ya Uislamu.

Copyright ©2004  Uislam.net