|
TAHARA
MAANA
YA TAHARA
1.
Katika lugha tahara maana yake ni:
kuwa msafi na uchafu wowote ambao unauhisi na kuuona kwa macho, na usafi wa moyo
kutokuwa na machafu yeyote yale.
2.
Katika sheria ya kiislamu maana yake
ni: Kuondosha uchafu wowote ule kwa kutumia maji.
UMUHIMU
WA MTU KUWA TAHIR (MSAFI):-
Tahara katika uislamu ni kitu
dharuri katika
kutekeleza ibada ambayo ndio sababu ya sisi kuumbwa. Na kama tunavyojua kuwa
sala ni nguzo muhimu katika uislamu haiwezekani kusimamishwa isipokuwa mtu awe
msafi wa mwili na wa moyo, basi hivyo hivyo ibada zoote kama vile Saumu, Hajj,
kusoma Quraan n.k. ni lazima mtu awe msafi wa kiwiliwili na msafi wa moyo
kutokuwa na machafu ambayo yanamghadhibisha Mola.
“HAKIKA M.
MUNGU ANAWAPENDA WENYE KUTUBIA NA ANAWAPENDA WENYE KUJITAHIRISHA(KUJIWEKA WASAFI)
albaqra#222.
ADABU
ZA KUFANYA HAJA NDOGO AU KUBWA:-
Yeyote yule mwenye kutaka kusali basi ni lazima ajizoweshe kwenda chooni ili
atoe choo kidogo au kikubwa kabla ya kusali. Ili asije mtu akajishughulisha
wakati ameshaanza kusali na ‘khushuu’ isije
ikatoweka wakati wa kusali.
Kasema Mtume Moh’d(SAW): “Asisali mmoja wenu na huku anazuwia choo kidogo ndani
ya kibofu cha mkojo”.
Na Bwana Mtume(SAW): amekataza mtu asisali ikiwa anajaribu kuzuwia haja ndogo au
kubwa kutoka katika njia zake.
Basi
anaetaka kwenda chooni basi afuate adabu zifuatazo:-
1.
Atayarishe kitu kinachoweza kusafisha
choo kidogo/kikubwa. Mfano maji n.k.
2.
Asichukuwe chooni kitu chochote
chenye aya za Quraan au jina la M.Mungu.
3.
Asifanye mtu haja yake mbele ya watu,
na kama atafanya haja yake mahali palipo wazi (porini,
jangwani) basi ni lazima ajitahidi kwendambali ili watu wasimuone anapofanya
haja yake. Pia inapendezewa kuwa mtu asiinue nguo yake mpaka awe ameshachuchumaa.
4.
Ikiwa mtu atafanya haja yake chooni
basi ni lazima atangulize mguu wa kushoto, na
akiaanza kuingia aseme “
BISMILLAH, ALLAHUMA INNI AUDHU
BIKA MINA ALKHUBTH WALKHABAAITH”.
5.
Asifanye mtu haja yake huku amesimama.
6.
Akitaka mtu kufanya haja yake mahali
palipo wazi (porini, jangwani) basi azingatie yafuatayo:-
I)
Asifanye mtu haja yake chini ya mti
ambao unatoa matunda au watu wanakaa chini yake kwa ajili ya kivuli. Pia katika
njia watu wanazopita.
II)
Asifanye mtu haja yake katika ardhi
ngumu ili mkojo usije ukamrukia.
III)
Asielekee upepo ili mkojo usije
kuruka katika mwili au kivazi.
IV)
Asielekeze
utupu wake wa mbele au wa nyuma QIBLA wakati akifanya haja yake.
Lakini baadhi ya wanavyuoni wamesema mtu anaweza kufanya haja yake na huku
ameelekea Qibla ikiwa mbele yake kuna ukuta, mfano Choo.
Lakini ni ubora kujitahidi kutokuelekea Qibla hata
kama umo ndani ya choo.
7.
Asifanye mtu
haja yake katika maji yaliyotwama, mfano vidimbwi au katika maji yanayotembea
ambayo watu wanayatumia kunawia au kunywa n.k. mfano falaj.
8.
Mtu
anapofanya haja asizungumze wala asiitikie salamu.
9. Akimaliza kukojoa ni lazima ajikamue
utupu wake kwa kutumia mkono wa kushoto mpaka kitone cha mwisho cha mkojo
kiondoke.
10.
Kabla ya
kujikosha na maji ni muhimu kutumia vijiwe au tissue ili kukausha mkojo, haja
kubwa au Alwadi (maji meupe yanayoteleza ambayo yanayotoka baada ya kukojoa au
wakati wa baridi na hayasafikishi kwa kutumia maji peke yake).
11.
Hairuhusiwi
kutumia mifupa , ngozi au choo cha mnyama kilichokauka kwa kujifutia haja ndogo/kubwa.
12.
Ni muhimu kuanza
kuosha utupu wa mbele kisha wa nyuma ikiwa mtu amepata choo kidogo na kikubwa.
Na ni lazima mtu ahakikishe kuwa amejisafisha vizuri tupu zake kabla ya kutoka
chooni.
13. Mtu akitoka
chooni ni lazima atangulize mguu wa kulia
na aseme ‘GHUFRAANAK’
Kuna aina
kumi za NAJASAT (uchafu) ambao ulamaa wote wamekubaliana kuhusu hivyo vitu.
Navyo ni:-
1)
Kitu chochote chenye roho ambacho
kimekufa bila ya kuchinjwa(MAITI/MZOGA).
2)
Damu
3)
Nyama ya Nguruwe
4)
Choo kikubwa
5)
Choo kidogo
6)
Mannii
7)
Al-Wadii
8)
AL-madhii
9)
Tahara za wanawake (Hedhi,Nifas, n.k.)
10)
Ulevi (Ulamaa wengi
sana wanasema si najis, kwa sababu asili yake ni chakula).
1)
Kitu chochote chenye
roho ambacho kimetoka roho bila ya kuchinjwa(MAITI/MZOGA):
Na
aina hii ya wanyama ni mbili:
a)
Wanyama wa nchi kavu.
b)
Wanyama wa baharini.
a)
Wanyama wa nchi kavu wako aina
mbili:
I)Wanyama
wenye damu inayochuruzika wanapojikata au kuchinjwa.
II)Wanyama
ambao hawana damu inayochuruzika.
I)Wanyama
wenye damu inayochuruzika wanapojikata au kuchinjwa.
Aina hii ya
wanyama wakifa ni najis (mfano, Panya, ndege, nyoka, N’gombe n.k). Ama binadamu
Muislamu si najis.
Amesema Mtume (SAW): Akifa Panya
katika samli iliyoganda basi mtoeni Panya na ile samli iliyokaribu nae kisha
itumieni, na akifa katika samli iliyoyayuka basi imwageni na msiitumie.
Baadhi ya
ulamaa hawajakubaliana kuwa je maiti ya (Chawa(Ni NAJIS),
Mbu, Kunguni,Viroboto n.k) ni NAJIS au SI NAJIS. Baadhi ya wanavyuoni wanasema
ikiwa (Chawa, Mbu, Kunguni,Viroboto n.k) amekufa mwenyewe bila ya sababu juu ya
mwili wa mtu na huku mtu huyo ameshatia udhu/ameshasali basi udhu ule
haujatenguka wala sala haijaharibika, ama ikiwa mtu atamuua kwa mkono wake
mwenyewe basi udhu/salaa itakuwa imeharibika.
Lakini ni bora kuchukulia kuwa hawa wadudu
ni najis kwa ajili tusije tukaingia kwenye shaka wakati tunafanya IBADA.
NOTE:
Sehemu yeyote ya mnyama (mfano, Mguu, Paja n.k) ikiwa imekatwa kwa sababu yeyote
ile na hali ya kuwa mnyama bado yuhai. Basi hiyo sehemu huwa ni NAJIS (MAYYITA)
haifai kuliwa.
II)Wanyama
ambao hawana damu inayochuruzika.
Aina hii ya
wanyama wakifa au wakiingia ndani ya chakula na wakafa ndani yake si najis wala
hicho chakula hakiwi najis.( mfano, N’zi, Sisiminzi, Sqaat, N’ge n.k)
Amesema Mtume
(SAW): Akidumbukia N’zi kwenye chombo ambacho kina (maji,maziwa) basi mzamisheni
ndani kisha mumtoe nje na munywe(maji,maziwa) hayo. Hakika bawa moja linamaradhi
na jengine linadawa(shifaa), basi N’zi anatanguliza bawa lenye maradhi kabla ya
bawa lenye dawa(shifaa).
b)
Wanyama wa baharini.
Aina hii ya
wanyama(Samaki) wamekubaliana Ulamaa kuwa si najis na ni tahir kuwala bila ya
kuchinjwa na pia damu yao SI NAJIS.
Amesema Mtume
(SAW): Mmehalalishiwa vitu viwili vilivyokufa na damu aina mbili. Ama viwili
vilivyokufa ni: (Samaki na N’zige). Na ama damu aina mbili ni: (Maini na Wengu
la Mnyama anaeliwa).
Ama Samaki
wanaokufa wenyewe bila ya kuvuliwa, baadhi ya Ulamaa wanasema ni HALALI kuwala.
Na ikiwa wameanza kuharibika basi ni MAKRUH(haipendezewi) kuwala.
Wanasema
Ulamaa kuwa wanyama halali wa baharini ambao wanaweza kuliwa bila kupigiwa
“BISMILLAHI” ni Samaki tu, ama Nyangumi ni
lazima apigiwe “BISMILLAHI” wakati anapovuliwa ndio huwa halali.(ALLAHU A’ALAM).
2)
Damu Masfuh:
Ni damu
inayotoka kwa wingi kwenye wanyama(mfano, N’gombe, Mbuzi, Bin Aadam n.k), kwa
kuchijwa au kuumia. Basi damu hii huwa ni NAJIS na haifai(haijuzu) kunywa na
hutengua udhu.
Baadhi Ulamaa
wamekhitalifiana katika damu chache ambayo ikikusanywa kwenye (ngozi ya mtu au
nguo) haiwezi kuchuruzika kuwa SI NAJIS wala
HAITENGUI UDHU. Damu hiyo ni ile inayotoka kwenye mnyama ambae hajachinjwa (mfano,
damu chache inayotoka kwenye mabawa ya kuku yakivutwa au damu chache inayotoka
kwenye ngozi ya mnyama akiumia au binadamu akijitumbua jipu dogo).
Ama tone
dogo la damu ya Mwanadamu au damu ya N’zi,
Chawa(NAJIS) , kunguni, kiroboto n.k. akiuliwa juu ya mwili wa mtu
likaganda kwenye nguo imeruhusiwa kuwa SI NAJIS na damu hiyo haitengui udhu.
Lakini ni bora kuchukulia kuwa hawa wadudu
ni NAJIS na damu yao pia ni NAJIS. Kwa ajili tusije tukaingia kwenye shaka
wakati tunafanya IBADA.(ALLAHU A’ALAM).
3)
Nyama ya Nguruwe:
Bila ya shaka
chochote kinachotoka kwenye Nguruwe (ngozi,maziwa,mifupa,nyama n.k) ni haramu
kukitumia na kukila. Kwa dalili ya Quraan na Sunna.
Amesema Mtume
(SAW) : Nimetumwa kuvunja misalaba na kuuwa nguruwe.
Ama Nyani na
Tembo wamewekwa katika kundi la Nguruwe kuwa ni NAJIS. Kwa hiyo haifai kutumia
chochote kinachotokana na wanyama hawa.
(ALLAHU
A’ALAM).
NOTE: Kuhusu
ndovu ya Tembo Ulamaa wamekhitalifiana kuwa je ni najis au si najis.
4)
Choo Kikubwa(Mavi) & (
5) Choo Kidogo(Mkojo):
Bila Shaka
wamekubaliana Ulamaa wote kwa dalili ya Quraan na Sunna kuwa choo Kikubwa na
kidogo cha Mwanadamu ni NAJIS. Na wanasema Ulamaa kuwa chochote kinachotoka
kwenye njia ya choo kikubwa au kidogo ni NAJIS ( mfano, Kijiwe au Mdudu)
Anasema M.
Mungu : (AU AKIJIWA MMOJA WENU NA CHOO KIKUBWA) Al-nisaa43.
Amesema Mtume
(SAW) : (Asisali mmoja wenu na huku anazuwia choo kikubwa na kidogo).
Ama kuhusu
Choo Kikubwa cha wanyama walioruhusiwa kuliwa SI NAJIS.
Dalili ni
kwamba Mtume (SAW) aliwaamrisha watu wa AL-JANIIN kutumia choo kikubwa cha
wanyama kuwa ni chakula cha wanyama. Watu wa AL-JANIIN wakamwambia Mtume(SAW) :
Ewe mtume lakini Wanadamu wanatia NAJIS choo hicho kwa kujisafishia uchafu
wao(Mavi, Mkojo), ndio Mtume akakataza watu wasijisafishie uchafu wao kutumia
mifupa pamoja na choo kikavu cha wanyama. Lakini kuhusu MKOJO wa Wanyama
walioruhusiwa na wasioruhusiwa kuliwa ni NAJIS.
Kwa dalili
kuwa Mtume (SAW): Ameuita mkojo kuwa ni kitu Khabith.
NOTE:
1) Kuna hadithi kuwa Mtume (SAW):
Aliwaambia watu wa ARNAIN wanywe Mkojo wa Ngamia pamoja na maziwa yake
walipomshitakia kuwa wamepata maradhi.
Lakini Ulamaa wanasema kuwa hii ruhusa ni khasa kwa hao
watu peke
yao.
2)
Kuna hadithi kuwa Mtume (SAW)
ananasema: ( Ikikukuta Salaa na uko ndani ya zizi la mbuzi sali, na ukiwa ndani
ya zizi la Ngamia usisali) (ALLAHU A’ALAM).
Kuna vitu Vinatoka puani au
tumboni kwa njia ya koo ambavyo ni NAJIS na vinatengua udhu:-
1)
AL-QAY(kucheuwa) kitu mpaka kikafika
mdomoni.
2)
AL-QALAS(kucheuwa) kitu na kikafika
kwenye koho peke yake.
3)
AL-RUAAF(damu inayotoka puani).
Amesema Mtume (SAW): ( Atakae cheuwa kitu mpaka kikafika
mdomoni,au kwenye koho au akatoka damu puani, au akatoka Al-MADHII. Na aende
akatawadhe. Ama kuhusu vitu vinavyotoka kwenye mwili wa mtu ,mfano: uchafu
unaotoka kwenye vidonda au Hab shabaab (Weupe), usaha unaotoka kwenye jipu ambao
ni mwingi kushinda damu, mafua, kamasi na makohozi wanasema Ulamaa kuwa si najis
na havitengui udhu. (ALLAHU A’ALA)
6) AL-MANII:
Ni
maji meupe mazito yanatoka kwenye Dhakar ya Mwanamume kwa kutamani na kumwaga.
Manii yanaharufu mbaya. Ama kwa mwanamke Manii ni maji mepesi.
7) AL-MADHII:
Ni
Maji yanayoteleza na hayana rangi yanatoka kwenye Dhakar ya Mwanamume kwa ajili
ya matamanio.
8) AL-WADII:
Ni maji meupe yanatoka kwenye Dhakar ya Mwanamume bila ya
matamanio baada ya mkojo, au kwa sababu ya baridi au maradhi.
9) Tahara za Wanawake:
a)
Damu ya Hedhi:
Ni damu inayotoka kwenye faraj(Uchi) wa mwanamke, nzito,
nyeusi, na inaharufu mbaya. Na damu hii ni kawaida kwa wanawake wote kuwatoka
katika kila mwezi kwa wakati maalumu.
b)
Damu ya Nifas:
Ni sawasawa na damu ya Hedhi, lakini inatoka baada ya Mwanamke kuzaa mtoto.
Amesema Mtume (SAW) : ( Al-manii, na Al-madhii, na Al_wadii,
na damu ya hedhi, na damu ya nifas ni NAJIS. Asisalie mtu nguo iliyoingia kitu
chochote katika hivi mpaka akoshe nguo hiyo na ipotee athari yake).
c)
Damu ya Istihadha:
Ni damu nyekundu nyepesi inamtoka
mwanamke akiwa na maradhi.
Amesema Mtume (SAW) : ( Damu ya Istihadha ni najis, na
inatengua udhu, kwasababu ni damu inayotoka kwenye mifupa ya damu,)
d) Uchafu unaofuatilia
Hedhi au Nifas, mfano: (Umanjamanjano)
e) AL-QASSAT AL-BAIDHAA:
Ni maji meupe
sana yanatoka baada ya hedhi au nifas. Haya maji ni dalili ya kuwa mwanamke
ameshasafishika na hedhi au nifas. Haya maji ni najis kwa ajili yanatoka kwenye
njia inayotoka najasa(Uchafu).
10)
Ulevi:
(Ulamaa wengi
sana wanasema si najis, kwa sababu asili
yake ni chakula).
Ulamaa wote wamekubaliana kwa dalili ya Quraan na
Sunna kuwa ulevi ni najis. Na haifai kutumia ulevi au siki yake au uchafu
uliotengenezewa ulevi kuwa ni dawa ya kuponesha maradhi yeyote yale.
Amesema Mtume
(SAW): ( Nimetumwa kumwaga “kuondosha” ulevi).
Lakini kuna
baadhi ya ulamaa, wanasema kuwa ulevi ni TAHIR si NAJIS. Sababu ni kuwa ulevi ni
najasa MAANAWIYA(najasa ambayo haionekani na haiondoki mpaka kwa nia, na kwa
kukoga janaba,na kwa kuondoka athari ya hicho kitu) na si najasa HISIYA( najasa
ambayo inaonekana mfano: Choo kikubwa/kidogo). Kwa ajili asili ya kitu ni tahir
isipokuwa kile kilichosimama dalili juu yake kuwa ni najis. Na pia kitu
kilichoharamishwa si lazima kitu hicho kiwe najis, kwani bangi ni haramu lakini
si najis. (ALLAHU A’ALAM)
KUNA BAADHI
YA VITU ULAMAA WAMEKHITALIFIANA KUWA JE NI NAJIS AU SI NAJIS.
VITU HIVYO
NI KAMA IFUATAVYO:
1)
Wanyama waliokuwa na meno marefu (Simba,
Chui n.k)
2)
Ndege wenye makucha marefu (Eagle,
kunguru n.k)
3)
Paka.
4)
Mbwa anelelewa na kufundishwa vitu.
5)
Mtu Mushrik (Kafiri)
6)
Jasho la Mlevi.
1)
Wanyama waliokuwa na
meno marefu (Simba, Chui n.k) :
Wamesema baadhi ya ulamaa kuwa nyama zao na vyote vinavyotoka mwilini mwa mnyama
huyo (maziwa, jasho,choo chake) ni haramu.
Amesema mtume (SAW): ( Kula mnyama yeyote mwenye meno marefu
na makucha marefu ni haramu). Na pia Mtume(SAW): Amekataza watu kunwya maji
yaliyobakishwa na wanyama hao ikiwa kiwango cha maji ni chini ya 200Litre.
Amesema Mtume (SAW): Yakiwa maji ni QILATAIN(200Litre), basi
hayanajisiki.
Pia kuna Ulamaa waliokhitalifiana kuhusu kula nyama ya Farasi,
Punda na Bighaal. Je inajuzu au haijuzu? Na watu wamechukia kula nyama zao baada
ya Mtume (SAW): Kukataza kula nyama ya Punda anaetumiwa katika mambo ya
kimaisha(Kubeba mizigo n.k). Na wengine wanasema kuwa haifai kula nyama za
wanyama hawa kwa ajili ndio wanaotumiwa wakati wa vita.
Anasema
Jabir(R.A): (Amekataza Mtume (SAW) wakati wa vita vya Khaibar kula nyama ya
Punda wanaotumiwa na akaruhusu watu wale nyama ya Farasi). (ALLAHU A’ALAM)
2)
Ndege wenye makucha
marefu (Eagle, kunguru n.k):
Wamesema baadhi ya ulamaa kuwa nyama zao na vyote
vinavyotoka mwilini mwa Ndege hawa (majimaji yanayotoka mwilini mwake,choo
chake) ni haramu.
Amesema mtume
(SAW): ( Kula mnyama yeyote mwenye meno marefu na makucha marefu ni haramu).
Kuna Ulamaa
wanasema kuwa inachukiza kuuwa aina sita ya ndege na wanyama. Kutokana na
Hadithi iliyopokew kutoka kwa Mtume (SAW) kuwa Amesema: Musiuwe vitu sita: 1.
CHURA hakika sauti mnayoisikia ya chura ni TASBIH NA KUMTUKUZA M.MUNGU, na
aliporushwa Nabii Ibrahim kwenye moto, waliomba wanyama wa nchi kavu na ndege
wauzime moto usimuunguze Nabii Ibrahim. M.Mngu akawapa ruhusa Vyura na
wakajirusha kwenye moto, na thuluth(1/3) ya moto ikazimika, na thuluth(1/3)
iliyobakia M.Mungu akabadisha joto la moto kuwa baridi ya maji. Na wala musiuwe
mdudu Maji Moto(AL-NAMLA), hakika Nabii Suleman amekwenda pahali ili akanywe
maji, akamuona mdudu Maji Moto(AL-NAMLA) ameinua mikono anasema: “EWE MOLA SISI
NI VIUMBE KATIKA VIUMBE VYAKO WALA HATUWEZI KUKOSA FADHILA ZAKO, TUNAKUOMBA
UTULETEE MVUA ILI MIMEA IOTE”. Akasema Nabii Suleman: Rudini mumekwisha
nyweshwa maji. Na wala musiuwe Nyuki, hakika wanawahifadhia vizuri na
wanawalisha vizuri. Na wala musiuwe HUDHUD , kwani wao walikuwa wakipenda sana
kumuabudu MOLA wakati palipokuwa hakuna ABDU wa kuabudu. Na wala musiuwe AL-SARD
ndie aliekuwa akimuonyesha njia Nabii Adam kutoka peponi mpaka ardhini kwa muda
wa miaka arubaini. Na walamusiuwe AL-KHATTAF, hakika huko kuzunguka kwake
mnavyokuona ni sehemu ya Masjid AL-AQSA ulipounguzwa moto.
(ALLAHU
A’ALAM)
Wametilia
mkazo AS’ HAAB( Ulamaa wa Kiibadhi). Kuhusu kuuwa wanyama hawa mpaka wakaweka
kuwa, atakae wauwa wanyama hao ni lazima alipe fidia ya DIRHAM MBILI kwa kila
mnyama. Ama fidia ya Chura ni MBUZI.
(ALLAHU A’ALAM)
3)
Paka:
Ipo
khilaf kuhusu Paka, Lakini lililo sahihi ni kuwa Paka ni Tahir si najis. Kwa
sababu Paka ni mnyama ambae daima anaishi katika nyumba za wanadamu.
Anasema Abi Qatada. Amesema Mtume (SAW), kuhusu Paka : (Paka
si najis, hakika Paka ni mwenye kuzunguka baina yenu.)
Na wako waliosema kuwa Paka ni najis. Kwa sababu Paka ni
katika wanyama wenye meno marefu na wao ni najis. (ALLAHU A’ALAM)
4)
Mbwa anaelelewa na
kufundishwa vitu:
Wamekhitalifiana Ulamaa, na wakasema baadhi yao si najis. Kwa sababu Mbwa huyo
amezuiliwa kula vitu vichafu(KHABAITH). Lakini lenye nguvu ni kuwa Mbwa ni najis,
kwa dalili ya hadithi ya Mtume(SAW).
Amesema Abi Huraira (R.A), Amesema Mtume (SAW) : Ikiwa Mbwa
atakunywa/atakula katika chombo cha mmoja wenu, basi akoshe chombo hicho mara
saba mwanzo wake kwa kutumia mchanga na mwisho wake pia kwa kutumia mchanga.
5)
Mtu Mushrik (Kafiri):
Wamekubaliana Ulamaa kuwa Mtu Mushrik ni najis.
Amesema M.Mungu : (HAKIKA WASHIRIKINA NI NAJIS) al-tauba27.
Na Mtume (SAW): Ameamrisha ikiwa Muislamu atahitajia chombo
alichotumia AHLU AL-KITAAB, basi ni lazima akioshe. Hii ndio ikawa ni dalili ya
wao kuwa ni najis.
Ama baadhi ya Ulamaa wanasema ikiwa Mushrik ni katika Ahlu
Al-Kitaab, basi majimaji yanayotoka katika mwili wake ni tahir.
NOTE:
Baadhi ya Ulamaa wanasema ukiwa umetawadha, na ukaamkiana na
Mtu Mushrik na huku wewe au yeye ana majimaji katika mkono wake. Basi ni lazima
utawadhe tena.
(ALLAHU A’ALAM).
Ama chakula cha AHLU AL-KITAAB ni halali juu yetu.
Amesema M.Mungu : ( NA CHAKULA CHA WALIOPEWA KITABU NI
HALALI JUU YENU)al-maaida5. (ALLAHU A’ALAM)
6)
Jasho la Mlevi:
Ama
kuhusu jasho la mlevi, na maziwa ya mwanamke anaekunywa ulevi, wanasema Ulamaa
kuwa ni bora na kujiepusha na jasho lao lisikuguse kwa muda wa siku nzima na
usiku wake. Na hii ni makadirio kuwa chakula kinabaki ndani ya mwili wa mtu siku
nzima na usiku wake.
(ALLAHU
A’ALAM).
NOTE:
Wanasema
Ulamaa ikiwa wanyama walioruhusiwa kuliwa, wakila kitu najis(Mzoga,Damu n.k),
basi li lazima
wakae siku maalum ndio wachinjwe: Mfano,
a) Ngamia
ni lazima apewe chakula kisafi kwa muda wa siku kumi mpaka arubaini ndio achijwe.
b)
Ama N’gombe ni lazima apewe chakula
kisafi kwa muda wa siku saba mpaka thalathini ndio achijwe.
c)
Ama kuku ni lazima apewe chakula
kisafi kwa muda wa siku mmoja mpaka siku tatu ndio achijwe.
NOTE:
“NI LAZIMA TUFAHAMU KUWA MAMBO HAYA YA
FIQH NI MAMBO MUHIMU KATIKA MAISHA YA MUISLAMU. NA PIA MAMBO HAYA YANAKHITILAFU
NYINGI SANA KWA HIYO BORA MTU KUCHUKUWA LILE AMBALO HALINA SHAKA NA LILE AMBALO
ULAMAA WAMELIKUBALIANA, NA HALIWEZI KUHARIBU IBADA YA MTU.
AINA ZA MAJI
Baada ya
kuzungumzia aina tafauti za vitu ambavyo ni Najis katika durus zilizopita. Hivi
sasa ni lazima tuzungumzie vitu ambavyo vinaweza kuondosha hiyo Najasa ikimpata
Mwanadamu.
Kama inavyojulikana kuwa MAJI ndio
kitu ambacho Mwenyezi mungu amekijaalia kuwa ndio kinachoweza kuondosha najasa
kwenye mwili/nguo ya Mwanadamu.
Anasema Mola katika Surat Al-Anfaal#11
: “ Na anawashushieni kutoka mbinguni maji ili yakutahirisheni(yakusafisheni).
Lakini maji huwenda yakabadilika
tabia yake(yakanajisika), kwasababu ya kuchanganyikana na vitu vingine.
Kwasababu hiyo, maji yanagawanyika
katika makundi matatu katika kuwa tahir au sio tahir:-
1)
MAJI MUTLAQ
(TAHUR) :- Nayo ni maji yaliyobakia katika asili yake, na hayajapoteza rangi
yake wala utamu wake wala rangi yake. Na hukumu ya maji haya ni tahir
yanaondosha najasa na yanafaa kutawadhia( yanafaa kuogea janaba nk na pia
yanafaa kutawadhia udhu wa salaa nk). Mfano wa maji haya ni:- maji ya mvua, maji
ya barafu, maji ya bahari, maji ya
mito , na maji ya falaj.
2)
MAJI TAHIR:-
Nayo ni maji yaliyopoteza usafi wake kwa kuchanganyikana na kitu tahir. Hukumu
ya maji haya ni kuwa yanaweza kutumiwa kuondosha uchafu kwenye mwili, lakini
hayawezi kutumiwa kwa kuogea Hedhi, Nifas wala Janaba, na pia kutawadhia udhu
wowote ule. Mfano wa maji haya ni :- maji yaliyotiwa kitu ndani yake mfano
sabuni au zaafarani au maji yanayotolewa kwenye miti.
3)
MAJI NAJIS:-
Nayo ni maji yaliyoingia najasa. Na hukumu ya maji haya ni najis yakibadilika
rangi,utamu, na harufu. Basi maji haya hayafai kutumiwa na muislamu kufanyia
chochote kile (kuogea, kusafishia vitu na kutawadhia).
UDHUU:-
FADHILA ZA KUTAWADHA NA UMUHIMU
WAKE:
Udhu ni alama(sifa) katika alama za
waislamu hapa duniani na kesho akhera. Ameulizwa Bwana Mtume(SAW): “Vipi
utawajuwa watakao kuja baada yako. Akasema Mtume(SAW): Mnaonaje akiwa mtu ana
farasi mwenye alama nyeupe kwenye kipaji cha uso na miguu yake, akiwa
amechanganyika na farasi wengine wengi. Je ? mtu huyo hatamtambua farasi wake?
Wakajibu Masahaba; ndio Bwana Mtume atamjua. Akasema Mtume(SAW): Basi watu hao
watakuja siku ya kiyama wana alama nyeupe kwenye vipaji vyao vya uso na kwenye
miguu yao, kwa ajili ya athari ya udhuu”.
Udhu huwa ni usafi wa kusafisha
vitu vya mwilini kwa nje. Lakini udhu pia huwa ni usafi wa kusafisha vitu vya
mwili kwa undani. Kwani udhu husafisha na kuondosha uchafu na vumbi kwenye:-
mdomo, pua, uso, mikono , masikio, miguu na kichwa. Pia udhu husafisha viungo
hivi na madhambi ambayo viungo hivyo vimefanya, mfano: mdomo kusema mambo mabaya,
pua kunusa harufu ya manukato ya mwanamke ajnabii, macho kutizama mambo
yaliyokatazwa, mikono kugusa vitu ambavyo imekatazwa kugusa, kama vile kumgusa
mwanamke ajnabii mwili wake, masikio kusikiliza machafu kama vile nyimbo, na
miguu kwenda kwenye haramu. Basi udhu ni tahara ya vyote hivyo. Ama madhambi
ambayo yanafutika kwa ajili ya kutawadha ni madhambi madogo ama madhambi makubwa
hayafutiki mpaka kwa tauba ya kweli.
Amesema Mtume (SAW):- “ Je
niwaambieni yale ambayo MOLA humfutia mja madhambi yake na humuinulia daraja
yake? Kutia udhu kwa ukamilifu katika viungo, kuzidisha kwenda msikitini na
kungoja salaa baada ya sala. Basi huu ndio mshikamano, kasema hivyo Mtume mara
tatu.”
Na kutawadha kabla ya sala ni wajib,
kwa dalili ya Quraan.
Anasema Mola:- “ ENYI AMBAO
MMEAMINI, MKIINUKA KWENDA KUSALI, OSHENI NYUSO ZENU NA MIKONO YENU MPAKA KWENYE
VIGANJA, NA PANGUSENI VICHWA VYENU NA MIGUU YENU MPAKA KWENYE VIFUNDO” Al-maaida#6.
Kasema Mtume(SAW):- “ hana imani
ambae hasali, na wala hana sala ambae hana udhu, na hana mtu saumu isipokuwa kwa
kuacha mambo haramu aliyoyakataza M.Mungu.”
NAMNA YA KUTAWADHA:-
Inatakiwa mtu
kabla ya kutawadha, ajisafishe na uchafu wowote ule kwenye mwili/nguo. Na
atawadhe kwa kutumia maji masafi.
Basi Mtu akianza kutawadha ni
lazima afuatilie mambo yafuatayo:-
a)
Atie NIA
kwenye moyo wake kuwa anatawadha kwa ajili ya ibada.
b)
Aanze
kutawadha kwa kusema “BISMILAHI RAHMANI RAHIM”
c)
Akoshe
mikono yake mpaka kwenye kifundo
mara 3.
d)
Atie maji
mdomoni
mara 3.
e)
Atie maji
puani
mara 3.
f)
Akoshe uso
wake
mara 3.
g)
Akoshe
mkono wa kulia kuanzia vidoleni mpaka juu ya kifundo
mara 3.
h)
Akoshe
mkono wa kushoto kuanzia vidoleni mpaka juu ya kifundo
mara 3.
i)
Apanguse
kichwa chake kwa maji
mara 3.
j)
Akoshe
masikio n’nje na ndani
mara 3.
k)
Akoshe mguu
wa kulia pamoja na vidole na chini ya nyayo mpaka juu ya
kifundo
mara 3.
l)
Akoshe mguu
wa kushoto pamoja na vidole na chini ya nyayo mpaka juu ya kifundo
mara 3.
NOTE:- Inatakiwa mtu akimaliza
kutawadha asome duaa ifuatayo :-
“ASH’ HADU
AN LAA ILAHA ILA ALLAH, WA ASH’ HADU ANNA MUHAMMADAN ABDUHU WA RASULUH. ALLAHUMA
IJ’ ALANI MINA AL-TAWABINA WAJ’ ALANI MINA AL-MUTA’ TTAHIRIN”
FARIDHA ZA UDHUU:-
1)
NIA:- Nayo
ni lazima kabla ya kufanya ibada yeyote ile. Nia hutiwa ndani ya moyo kuwa hivi
sasa mimi nina anza kutawadha kwa ajili ya salaa.
Amesema Mtume (SAW):- “ Hakika
kila AMAL ni NIA”
2)
Kuosha Uso.
3)
Kuosha
mikono miwili pamoja na vifundo vya mikono.
4)
Kupangusa
kichwa.
5)
Kuosha
miguu miwili pamoja na vifundo vya miguu. Na ni lazima mtu ahakikishe kuwa
atasafisha baina ya vidole vyake vya miguu kwa kutumie vidole vya mikono, sio
mtu aweke mguu wake kwenye bomba huku maji yanamwagikia bila ya kutumia mkono
kwa kusafisha miguu.
Amesema Mtume(SAW):- “Safisheni
baina ya vidole nyenu vya miguu, kabla hamjasafishwa na misumari ya moto”
SUNNA ZA UDHU:-
1)
Kusema
“BISMI LAHI RAHMANI RAHIM” unapoanza kutawadha.
Amesema Mtume(SAW):- “ hana udhu
ambae haja taja jina la M.Mungu”
2)
Kukosha
Mdomo
3)
Kukosha pua.
4)
Kukosha
masikio n’nje na ndani.
5)
Kutawadha
kila kiungo
mara
3.
6)
Kufuatilia
mpangilio uliokuja kwenye sunna ( usitangulize kutawadha kiungo kabla ya
kinachofuatilia, mfano: kuosha uso kabla ya pua)
7)
Kutawadha
viuongo vyote wakati mmoja ( sio utawadhe baadhi ya viungo kisha baada ya muda
ukamilishe vingine)
8)
Kusafisha
ndevu kwa kupitisha vidole wakati wa kuosha uso.
MANDUBAAT
AL-UDHUU:- Ni mambo
yanayopendezewa kufanywa wakati wa kutawadha na yakiwanchwa hayatengui udhu:-
1)
Kupiga
mswaki kabla ya kutawadha. Amesema Mtume (SAW):- “Ningalikuwa si waogopei umma
wangu, lingaliwaamrisha kupiga mswaki katika kila salaa na kila udhuu.
2)
Kutumia
maji kiasi si kwa israfu.
3)
Kuomba duaa
baada ya kutawadha.
MAMBO YANAYOCHUKIZA KUFANYA WAKATI
WA KUTAWADHA:-
1)
Kumwaga
maji kwa wingi.
2)
Kuzidisha
kutawadha viungo zaidi ya mara tatu.
3)
Kuzungumza
wakati wa kutawadha, isipokuwa kuomba dua au kumdhukuru M.Mungu.
4)
Kutawadha
chooni.
5)
Kutawadhia
chombo cha dhahabu au fedha.
6)
Kutawadha
na hali uko uchi hata
kama
uko chooni peke yako au kutawadha na huku nguo yako iko juu ya magoti, na ikiwa
mtu kakuona uchi wako, basi udhu utakuwa umetenguka.
MAMBO YANAYOTENGUA UDHU:-
1)
Chochote
kitakachotoka kwenye tupu mbili ( utupu wa mbele au wa nyuma)
2)
Kutoka damu,
ikiwa kutoka mdoni, au puani, au mwilini.
3)
Kuingia
najasa mwilini au nguoni.
4)
Kutizama
mambo yaliyoharamishwa,
kama
vile nywele au mwili wa mwanamke ambae unaweza kumuowa.
5)
Kugusa
mwili wa mwanamke ambae unaweza kumuowa, ikiwa kwa kumuamkia nk, au kugusa utupu
wako au wa mkeo.
6)
Kusikiliza
nyimbo, na maneno machafu.
7)
Kusema
maneno baatil(mabaya):- kusengenya mtu, kufitinisha watu, kudanganya, kulaani
mtu na kutukana mtu nk.
8)
Kupotewa na
fahamu(akili):- kwa kuzimia, kuwa kichaa, kulewa. Kwa maradhi, au kwa kulala
ubavu, ama kulala huku umekaa bila ya kuegemea kitu udhu unakuwa haujatenguka.
9)
Aina zote
za maasi(madhambi), mfano kula riba nk.
10)
Kuacha
lolote lile la faridha au sunna za udhu, mfano: kutawadha juu ya socks bila ya
kuzivua
HUKUMU YA KUTAWADHA JUU YA P.O.P AU
JUU YA BENDEJI IKIWA MTU AMEUMIA ( MAS’H ALA JABIRA):-
Ikiwa mtu ameumia pahali na huku
amefungwa P.O.P. au bendej juu ya pahali alipoumia, basi anatakiwa anapotawadha
atie mkono wake maji kisha aukumute ndio kisha apanguse juu ya P.O.P au bendej
hilo.
INAMUAJIBIKIA MTU AWE KATIKA UDHU (ATAWADHE)
AKITAKA KUFANYA YAFUATAYO:
1)
Akitaka mtu
kusali sala yeyote ile ya faridha au sunna. Na udhu wa salaa ni wajib.
2)
Akitaka mtu
kutufu katika AL-KAABA. Amesema Mtume (SAW):- “ Tawaf ni salaa, isipokuwa
M.Mungu ameruhusu watu kuzungumza.” Na udhu wa tawaf ni wajib.
3)
Akitaka mtu
kulala. Amesema mtumu(SAW):- “ Ukitaka kulala, basi tawadha udhu wako wa salaa.”
Na udhu wa kulala ni sunna.
4)
Akitaka mtu
kusoma Qur’aan na kugusa msahafu. Kuna hadithi ya Mtume (SAW) kuwa amesema:- Juu
ya watu wenye janaba na hedhi na wote ambao hawako katika udhu kuwa wasisome
Qur’aan wala wasi ishike kwa mikono
yao mpaka wawe wametawadha”. Na
udhu wa kusoma Qur’aan au kuigusa ni sunna na ulamaa wengine wanasema kuwa ni
wajib
Imeadikwa na:
Ahmed Saif Al Harth
|