Utangulizi:                                                           

Kila Desemba Mosi ya kila mwaka Tanzania hujiunga na nchi nyingine duniani kuadhimisha siku ya Ukimwi duniani. Lengo kuu la siku hii ni kuwakumbuka waliokufa kutokana na UKIMWI na pia kuwaunga mkono walioathirika na ugonjwa huu ili waendelee kuishi kwa matumaini.

Kwa mujibu ya Ripoti ya Hali Watu Duniani ya 2000, UKIMWI unaongoza kama chanzo cha vifo barani Afrika wakati unachukua nafasi ya 4 ya sababu ya vifo duniani. Inasadikika kwamba zaidi ya watu 35 milioni, wakiwemo watu wazima na watoto, wanaishi na UKIMWI au na virusi vya UKIMWI. Maambukizo mapya yanakadiriwa kuwa zaidi ya milioni 5.4 kila mwaka. Bara la Afrika ndilo lina ongoza kwa kasi za maambukizo ya UKIMWI.

     Hali ya ukimwi Zanzibar:

Zanzibar ikiwa ni visiwa vilivyopo katika mgongo wa dunia, pia inakutana na vikwazo katika kupambana na maambukizo ya maradhi ya UKIMWI. Maambukizo ya VVU hupelekea kupunguwa kwa maisha ya watu na kupunguza nguvu  za kazi hasa kwa vijana wa kike na kiume ambao ni tegemeo la taifa.

Baada ya kugundulika kwa wagonjwa watatu katia mwaka 1986, idadi hiyo imeongezeka siku hadi siku na kuvifanya visiwa vya Unguja na Pemba mpaka 2002 kuwa na watu 3,287 waliogundulika kuwa na VVU na wakati kasi ya maambukizo ni asilimia 0.6% idadi inaonesha kuwa wanaambukizika zaidi kwa mara 4-6  kulingana na wanaume.  Kuna idadi ya watu 600 wamesharipotiwa kufa kutokana na UKIMWI na familia hizo zimeacha mayatima 500 walosajiliwa na kuna idadi ya watu 6000 wanaoishi na VVU hapa Zanzibar.

Copyright ©2004-2005  www.uislam.net