MAMBO MENGINE YANAYO SABABISHA UKIMWI
1.
Utumiaji wa ulevi na madawa ya kulevya.
2.
Kufanya biashara ya kuuzwa mwili.
3.
Kufanya matendo ya kujamiana yasiyokuwa salama na halali.
4.
Kutafuta maisha ya kupelekea kuondoka nyumbani muda mrefu kwa
wafanyakazi wa biashara, majeshi, wasafirishaji mizigo kwa njia za
magari makubwa, wavuvi kwenda kulala dago n.k.
Kwa nini ugonjwa wa UKIMWI unatisha sana?
Ugonjwa huu unatisha sana kutokana na sababu nyingi mbalimbali, baadhi
yake zikiwa ni hizo tatu zifuatazo:
1. Unafyeka watu kama Majani:
Mpaka sasa takwimu zilizopo zinaonyesha kwamba katika kila watu
100 wanaopata ugonjwa huu 60% - 70% huwa ni wale wenye UKIMWI
Baridi, 23 - 26% huwa ni wale wenye UKIMWI Vuguvugu; 2% - 15% huwa
ni wale wenye UKIMWI Moto; na katika kipindi cha miaka miwili hadi
mitano hao wenye UKIMWI Moto wanaweza kupoteza maisha.
2. Hautibiki:
Mpaka sasa wataalam hawajafaulu kugundua dawa za kuchanja ama
njia nyingine za kuzindika watu ili wasiugue UKIMWI.
3. Hauna Kinga:
Ijapokuwa ugonjwa umelipuka katika miaka ya hivi karibuni tu
lakini tayari umeshaenea sehemu nyingi sana duniani. Kutokana na
kuambukizana, takwimu zinaonyesha kwamba idadi ya watu wenye UKIMWI
imekuwa ikiongezeka mara mbili kila baada ya miezi sita hadi mwaka mmoja.
4. Unaambukiza:
Ijapokuwa wataalam katika sehemu nyingi duniani wanaendelea kujitahidi
sana kutafuta dawa za kuponyesha UKIMWI, lakini mpaka sasa
hayajapatikana mafanikio yenye matumaini makubwa.
5. Ni ugonjwa wa maisha:
UKIMWI hauimaliziki mwilini. Ukishaambukizwa utabaki nao mpaka
ufe. Viini (virus) vya ugonjwa huu vikishaingia mwilini mwako
vitaendelea kubana humo na kuzaana humo katika maisha yako yote; na kwa
vile mpaka sasa haijagunduliwa dawa ya kuweza kuviua basi ni dhahiri
kwamba ukiambukizwa ugonjwa huu utakuwa ni mtu mwenye wasiwasi maisha
yako yote kwani japo UKIMWI wako uwe ni wa baridi hujui ni lini utaweza
kubadilika na kuwa wa vuguvugu au wamoto.
Isitoshe licha ya kuwa ni ugonjwa wa maisha, kama wewe ni
msichana, ugonjwa huu utaweza kuendelea kuonekana kwa baadhi ya watoto
wako kwa miaka mingi baada ya wewe mwenyewe kutoweka.
|