Neno AIDS maana yake nini?

AIDS ni kifupi cha maeneo manne ya Kiingereza: Acquired Immune Deficiency Syndrome.

Sydrome:  Maana yake ni matokeo, au kikundi cha dalili, au kikundi cha mambo yanayojitokeza pamoja.

Acquired: Maana yake ni kukumbwa na au kupatikana na

Immune: Maana yake ni uwezo wa mwili wa kujihami dhidi ya magonjwa.

Deficiency: Maana yake ni upungufu, au dosari, au kuwa duni.

Tafsiri ya Kiswahili ya maneno hayo ya Kiigereza "The Syndrome of Acquired Immune Deficiency" ni:  Dalili au Matokeo ya  Kukumbwa na Upungufu wa  Kujihami Mwilini. Kama tunavyofahamu kujihami kunahitaji kuwa na silaha. Ndio kusema basi kwamba mwili wenye Hali Duni ya Kujihami ni mwili ambao silaha zake za kujihami zimedhoofika. Kwa hiyo tafsiri nyingine ya Kiswahili kilicho rahisi zaidi kuelezea maana inayofanana na maneno hayo ya Kiingereza "The Syndrome of Acquired Immune Deficiency" ni Matokeo ya Hali ya Kuporomoka  Silaha za mwili, na kifupi chake kinaweza kutupatia neno UKIMWI.

 U         =     Upungufu wa

  KI        =      Kinga.

 MWI    =     Mwilini.

Neno hili UKIMWI licha ya kuwa tafsiri ya AIDS, linasaidia sana kutoa picha sahihi ya mtu mwenye ugonjwa huo. Kama tutakavyoona hivi punde, mtu mwenye UKIMWI (AIDS) ni sawa na askari ambaye amenyang'anywa silaha, hawezi kujitetea.

 

Copyright ©2004-2005  www.uislam.net