NJIA, MBINU NA UTARATIBU WA KINGA DHIDI YA VVU:
1.
Kila mwenye ndoa kuilinda na kuheshimu mipaka na taratibu za ndoa.
2.
Kuacha kujiingiza na mambo yote yanayochochea maambukizi ya VVU.
3.
Kutumia vyombo vya habari na vya mawasiliano kwa kuelimisha.
4.
Kulinda walioathirika na VVU na kuwafariji.
5.
Kuepuka na kuacha kufanya tendo la ndoa/kujamiana kusikokuwa na usalama
na uhalali.
6.
Kutumia vifaa safi na salama katika kutoa huduma kukatia (kutia tohara)
au kutobolea (kupiga sindano), kunyolea na kutia damu.
7.
Kuwashughulikia na kuwasimamia wanawake kwa kuwapatia maisha yao badala
kuachiwa kuhangaika na kupelekea kufanya mambo yasiyo kuwa na faida.
8.
Vijana waelimishwe kuhusu njia bora za kupambana na maisha na kujiepusha
na mambo ya anasa na kupeleka kupata maambukizo ya VVU.
9.
Mama mwenye VVU asipokee ujauzito ikibidi ili kuepusha maambukizo kwa
mtoto?
10.
Kuzuia uenezwaji wa VVU inawezekana pindi mikakati iliopo itatiliwa
mkazo, kwa kushirikishwa jamii yote na katika ngazi zote za kifamilia na
kiutawala.
UKIMWI bado ni tatizo, hakuna tiba wala chanjo
lakini inawezekana kuzuia usambazaji wa maambukizo mapya ya VVU.
Kubadilisha tabia za watu zinazohatarisha afya ni njia muhimu. Watu wote
waelimishwe wajue kwa uwazi kuhusu UKIMWI bila ya kuoneana haya, lakini
pia bila kuvuruga mila na heshima kwa wahusika na kukiuka sheria na
mafunzo ya Allah S.W. |